New Dar Master Plan to render millions homeless

New Dar Master Plan to render millions homeless

Kama ni hivyo...majengo yote yale ya posta na kkoo yanatakiwa ground floor ziwe parking laking mbadala yake ni maduka na ofisi tena zingine za serikali... nayo yavunjwe...
 
Utaratibu huo ni mzuri nilipata kuona makala moja enzi za utawala wa serikali ya awamu ya wakati rais Mkapa alipotembelea china.
Wao pia walikuwa na maeneo yasiyopimwa lakini kilichokuwa kinafanyika walikuwa wanaorodhesha wakazi wa eneo husika kisha linaboreshwa kwa kujengo majengo ya kisasa.

Wahusika walikuwa wanapewa uchaguzi wa kupewa apartment au pesa maana huwezi kuwaondoa wananchi bila ya kuwalipa fidia

Hili wazo sahihi kabisa.
Hivi ndiyo tuliozoea wakazi wa Kariakoo na maeneo ambayo ni potential kibiashara. Mwenye uwezo wa kujenga ghorofa anakwambia uchague akupe pesa mtakazokubaliana au akulipe kiasi then atakupa apartment 1 na labda frem 2, maisha yanaendelea. Lakini la kusema utahamishwa hvhv daaah itakuwa ngumu tena ngumu sana
 
jiji litakua skwata mpaka lini? lazima hatua zichukuliwe. kwanza kwa kuzuia ujenzi kwenye maeneo yasiyopimwa na kisha kubomoa skwata kwa awamu kadri pesa ya fidia itavyoruhusu.
 
They will make it practical unfortunately for many. Mimi pia naenda kufuatilia ardhi kama cha kwangu hati yake ni halali. Watu wengi walitumia udhaifu wa vipindi vilivyhopita kujunufaisha, wingine wakitoa rushwa ili wapewe maeneo yasiyostahili kwa sababu hili lilikuwa halifikiriki

It is better to be clear ( seven up)
 
Kama Magufuli anataka nchi isitawalike, basi atekeleze huu mpango. Ni rahisi kutenga maeneo mapya ya viwanda na kutengeneza master plan mpya ambayo ina accomodate the current situation.

Nafikiri hii ndo njia mbadala maana zoezi likitelezwe itakuwa ni kiyama.
 
Ifike kipindi hii nchi agawanywe kwa kugawa shughuli kuu za kila mji,kuwe na miji maalumu ya viwanda,utawala,biashara nk.

Hiyo itasaidia kupunguza mlundikano wa watu katika baadhi ya miji.
 
Mbezi for industrial purposes....Magufuli taratibu baba.
Tatizo naona si Magufuli, ni hao 'wataalam' wetu vilaza na wasio na exposure.
Ati Mbezi kuwa industrial area!!
Inahitaji mtu kutoka kijijini jana kufanya uamuzi huo, hata kama amesoma mpaka PhD,
Kwa nini industrial area isipelekwe Masaki au Oysterbay kabisa?
 
Hapa wa kulaumiwa sio wananchi,bali ni watendaji wa wizara ya ardhi kwa rushwa iliyokithiri.Katika hii fiasco nachoona hapa ni wale oppurtunist wakijaribu kuwatisha watu,na hata kuwadhulumu,na pia kuwafanyia mbaya kwasababu wanazozijua wao.
Mimi nathani,wote waliokuwa hati halaii lazima waende mahakamani wafungue lawsuit kufidia madai yao nk.
Kuna sheria na lazima zitumike.
 
Tatizo naona si Magufuli, ni hao 'wataalam' wetu vilaza na wasio na exposure.
Ati Mbezi kuwa industrial area!!
Inahitaji mtu kutoka kijijini jana kufanya uamuzi huo, hata kama amesoma mpaka PhD,
Kwa nini industrial area isipelekwe Masaki au Oysterbay kabisa?
aise nchi yetu kuna watu wamesoma lakni hawafikirr kabisa yani.Hata leo tukisema mbagala ni sehemu ya viwanda je itakuwa ni sawa? kwanini wasijenge treni itakayopitisha malighafi nk kutoka bandarini kwenda huko ndani kwani mpaka iwe dar? huko bagamoyo nako kumejaa huwezi ukaweka kiwanda pale.
 
Utaratibu huo ni mzuri nilipata kuona makala moja enzi za utawala wa serikali ya awamu ya wakati rais Mkapa alipotembelea china.
Wao pia walikuwa na maeneo yasiyopimwa lakini kilichokuwa kinafanyika walikuwa wanaorodhesha wakazi wa eneo husika kisha linaboreshwa kwa kujengo majengo ya kisasa.

Wahusika walikuwa wanapewa uchaguzi wa kupewa apartment au pesa maana huwezi kuwaondoa wananchi bila ya kuwalipa fidia

Hivyo ndivyo SMZ wanavyofanya hapa Zenji ,yle maghorofa ya michenzani Gamba na pengineko zilikuwa nyumba chovu za walala hoi zikabomolewa kila mtu akapewa apartment.
JPM kama anjiweza nae afanye hivyo ,komakoma kwa mtogole ,uwanja wa fisi kwa maguruwe kuvae sura mpya!
 
Wananchi wamekosea kujenga maeneo yasiyoruhusiwa, ni sawa adhabu yao ni kubomolewa.
Hii adhabu inabidi pia iende mpaka kwa serikali kwa kusindwa kusimamia maeneo mpaka yakavamiwa, ni suala la miaka kadhaa.

Maajabu hapa ni pale serikali inaposema kwamba maamuzi yanayofanywa na serikali za mitaa sio sahihi bali yale yanayofanywa na serikali kuu kipitia wizara ndio sahihi. Hiki ni kichekesho kikubwa na aibu kuu kwa nchi yetu kwa kutuaminisha kuwa serikali ni litaasisi lisilohusiana na watu linaowatawala maana serikali za mitaa ndizo grass roots za serikari kwa maana hiyo huu ni mwendelezo wa kulalamika na kulialia pale mambo yanaposhindikana. Lakini pia hawa wizara waache kusema tu Dar es Saalam bali ukweli uangalie miji yote ya Tanzania imejengwa kiholele japo Dar es Salaam inaweza kuwa imezidi kulingana na ukweli kwamba rushwa nyingi kuanzia ndogo hadi kubwa zinafanyikia hapo.
Hii makala ukiisoma mac honi inaelekea ni nzuri sana lakini kimatendo haiwezi kutekelezeka. Na sote tukumbuke haya mambo yote yametokea chini ya sewrikali ya ccm, hakuna chama wala mtawala mwingine tofauti na ccm aliyewahi kuitawala nchi hii.
Kwa maana hiyo tukubaliane na amneno ya Mch. Msigwa (MB) aliyoyakopa kutoka kwa Albert Einstein kuwa "Tatizo kamwe aliwezi kutatuliwa na aliyelisababisha na akili iliyotenmgeneza tatizo haiwezi kulitatua". CCM ni ile ile!
 
Mimi ni mmoja wa watu ambao natamani Miji iwe imejengekaa vzr, ingawa Magufuli anakazi nzito kuujenga huo mji, ila hakuna namna.

Lawama zote zielekee kwa mwinyi, mkapa na JK.
Enzi za nyerere nyumba zilikuwa zimepangwa vzr, kila nyumba umbali wa mita 6

Hata Oysterbay kumebafilika nakuwa na majengo ya biashara kama vile mahoteli badala ya nyumba za makazi. Binadamu gani sisi tunaopenda kuishi bila utaratibu. Kwa mfano kwenye maeneo ya nyumba za kawaida mtu anajenga ghorofa; mtu anathubutu kuziba mto ili aongeze nafasi ya nyumba ya biashara zake au makazi; nk. Lakini humu jamvini tunatetea hali hiyo!!! Kesho yakitokea mafutiko tunaikaba koo serikali.

Kabla ya hizo nyumba kuvunjwa, waliohusika kutoa vibari vya ujenzi wasakwe na kuwajibishwa kulingana na sheria za nchi hata kama watakuwa wamestahafu. Naamini huko waliko wanaishi kama wako peponi kwa fedha za rushwa. Wenye hizo nyumba pia hawawezi kukwepa mkono wa sheria kwa kuwa watakuwa wamehusika katika kuvunja sheria za mipango miji.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
Tubanda twenyewe tutakua labda 500,000.
So 500,000x$100,000=50,000,000,000/=
Hivi kagesi ketu hakatoshi kulipia hili zoezi?
Mbona ni tujisent tu huto jamani?
Mkuu ukipigia gharama ya 500,000 kwa kibanda nadhani utakuwa umejisaulisha gharama za ujenzi au umeamua kudharau.
Mfano; 1. tofali za watu wa kawaida kama sisi ni 800 - 1,000 @ jiulize kibanda kinachukua tofali ngapi na shimo la choo tu kwingine makuti.
2. Cement & mchanga + labour power
AMKA.
 
Licha ya kwamba wengi tunataman jiji la dsm lionekane vizuri ila gharama ya kulifumua ni kubwa sana na sidhani kama ni dhamira yao kufanya hivyo! Wanachofanya sasa ni kuondoa wote waliojenga kwenye mabonde ya maji, maeneo ya wazi na kwenye fukwe!! Haya mengine sidhani kama watavunja!
Sio Dar tu,mipango miji inabidi uwe nchi nzima bila kujali ni mjini au kijijini...Maana kuna maeneo yanayofaa kwa kilimo huko vijijini watu wamejenga,sehemu inayofaa kwa mifugo,watu wanalima yaani vurugu sana,mpango huu utekelezwe nchi nzima ila kwa haki na kulinda Raia kwani serikali ndio iliokuwa na makosa labda mabondeni na maeneo ya wazi
 
Hii kitu si ya kufanyia masikhara, itatugharimu wengi sana maana naona ni wakazi wachache sana hapa Dar wanaoishi maeneo yaliyopimwa. Sasa angalia mfano hiyo mbezi beach kwamba ni industrial area hapo ni balaa
 
Sometime unashindwa kuamini hivi vitu! Magu anatafuta kupinduliwa. Aliyepaswa kuupanga huu mji ni nani? Nasmini wana mabilioni ya kutosha kulipa fidia!

hakuna wa kumpindua rais nchi hii. ka kitu huwa tunamwachia Mungu kana kwamba ndo aliyewatuma wanaotuonea. watuvunjie tu maana tumewapa ikulu sisi wenyewe. tuisome namba
 
mmh, hii si habari njema hata kidogo, kwanini kuwaweka watu roho juu!!!
 
Back
Top Bottom