Neno 'Mhudumu' lasababisha kifo cha mmiliki wa baa

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
MMILIKI wa baa ya Tale mjini Njombe, Jackson Mgeni (35), mkazi wa Mji Mwema mjini hapa, amefariki dunia kutokana na kuchomwa kisu tumboni na anayedaiwa mteja wake, Emmanuel Shiwa (32).

Mfanyabiashara wa madini na mkazi wa eneo la Uwanja wa Ndege mjini Njombe, anadaiwa kutenda ukatili huo baada ya kutokea ugomvi kati yao alipomwita Mgeni, akitumia neno 'mhudumu'.

Ni tukio hilo lilitokea Novemba jana saa nane usiku katika baa hiyo ya mjini Njombe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Kamishna Msaidizi Mahamoud Banga alithibitisha kutokea kwa tukio hilo. Alisema mtuhumiwa ni mteja mzoefu katika baa hiyo.

"Katika hali ya kupata huduma, mtuhumiwa alimwita Mgeni kwa jina la mhudumu. Sasa kile kitendo cha kuitwa mhudumu, ninafikiri kilimuudhi.

"Akaanza kugombana na yule mteja na yule mteja ninafikiri aliona hatoweza kupigana naye kawaida. Hivyo alitoka nje," alisema Kamanda Banga.

Aliendelea kusimulia, akisema: "Mtuhumiwa huyo baada ya kutoka nje alipanda gari lake, akaenda nyumbani kwake.

"Mashuhuda wanasema ni maeneo ya Uwanja wa Ndege, lakini baada ya muda alirudi na kisu na kumvizia yule jamaa na kumchoma nacho tumboni."

Kamanda Banga alisema kuwa baada ya kufanya tukio hilo, wananchi ambao ni wateja wa baa hiyo walikuwapo eneo la tukio, walimdhibiti mtuhumiwa na kutoa taarifa kituo cha polisi.

"Polisi walifika na kumkamata, majeruhi alikimbizwa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Njombe (Kibena), lakini kabla ya kuanza kupatiwa matibabu alifariki (dunia)," alisema Kamanda Banga.

Njombe ni miongoni mwa mikoa yenye matukio mengi ya mauaji nchini. Hata hivyo, matukio mengi yanahusishwa na imani za kishirikiana na wivu wa mapenzi.
 
Sijajua kwanin hapa nchini kwetu mtu akichimwa kisu cha tumbo kupona ni 30% au hawez kupona kbsa hta akiwahishwa hospital.. nmesikia vifo vingi san vya namna hii, nahisi madaktar wetu hawan ujuzi na hizi ajali kulinganisha na nchi zingine kupona ni 70%
 
Aliendelea kusimulia, akisema: "Mtuhumiwa huyo baada ya kutoka nje alipanda gari lake, akaenda nyumbani kwake.

"Mashuhuda wanasema ni maeneo ya Uwanja wa Ndege, lakini baada ya muda alirudi na kisu na kumvizia yule jamaa na kumchoma nacho tumboni."
MAONI YA BUSH LAWYER ON JF :D :D :D :D :D :D :D :D:D:D:D

Muaji ya kukusudia, defence ya "in heat of passion" haipo tena! Alipata muda wa kwenda nyumbani, akatafuta kisu kilipo, akapanda gari, akarudi, akamtafuta alipo....akamchoma! basi alikusudia KUUA...MALICE AFORETHOUGHT

Heat of passion is a mitigating factor that may be raised by an accused criminal, claiming to have been in an uncontrollable rage, terror, or fury at the time of the alleged crime, especially one provoked by the victim. Heat of passion defense is used to negate the element of malice in a murder prosecution.
 
Sijajua kwanin hapa nchini kwetu mtu akichimwa kisu cha tumbo kupona ni 30% au hawez kupona kbsa hta akiwahishwa hospital.. nmesikia vifo vingi san vya namna hii, nahisi madaktar wetu hawan ujuzi na hizi ajali kulinganisha na nchi zingine kupona ni 70%
Hii ni dondoo nzuri kwa wataalamu wa afya kuifanyia tafiti ili waje na namna ya kuboresha huduma kama inavyofanyika katika maeneo mengine yenye changamoto ikiwemo vifo vya wajawazito
 
MAONI YA BUSH LAWYER ON JF :D :D :D :D :D :D :D :D:D:D:D

Muaji ya kukusudia, defence ya "in heat of passion" haipo tena! Alipata muda wa kwenda nyumbani, akatafuta kisu kilipo, akapanda gari, akarudi, akamtafuta alipo....akamchoma! basi alikusudia KUUA...MALICE AFORETHOUGHT

Heat of passion is a mitigating factor that may be raised by an accused criminal, claiming to have been in an uncontrollable rage, terror, or fury at the time of the alleged crime, especially one provoked by the victim. Heat of passion defense is used to negate the element of malice in a murder prosecution.
bush lawyer nitakutafuta
 
Sijajua kwanin hapa nchini kwetu mtu akichimwa kisu cha tumbo kupona ni 30% au hawez kupona kbsa hta akiwahishwa hospital.. nmesikia vifo vingi san vya namna hii, nahisi madaktar wetu hawan ujuzi na hizi ajali kulinganisha na nchi zingine kupona ni 70%

Maeneo ya tumbo kuna organ muhimu nyingi kama Ini, figo, kongosho, .. hivyo ikitokea kisu kimegusa organ hizo kifo kinamkuta mchomwaji.
 
Maeneo ya tumbo kuna organ muhimu nyingi kama Ini, figo, kongosho, .. hivyo ikitokea kisu kimegusa organ hizo kifo kinamkuta mchomwaji.
1700644569757.png


Most likely kilitua kwenye nini hapo?
 
MAONI YA BUSH LAWYER ON JF :D :D :D :D :D :D :D :D:D:D:D

Muaji ya kukusudia, defence ya "in heat of passion" haipo tena! Alipata muda wa kwenda nyumbani, akatafuta kisu kilipo, akapanda gari, akarudi, akamtafuta alipo....akamchoma! basi alikusudia KUUA...MALICE AFORETHOUGHT

Heat of passion is a mitigating factor that may be raised by an accused criminal, claiming to have been in an uncontrollable rage, terror, or fury at the time of the alleged crime, especially one provoked by the victim. Heat of passion defense is used to negate the element of malice in a murder prosecution.
Ndivyo mlivyo fundishwa first year mmekariri
 
Hata ukimsikiliza kamanda wapolisi anatoa taarifa kama ni mauji ya kutokusudia,yaani unaona kabisa inajengwa ajenda ya Jamaa kuachiwa Kwa kigezo Cha manslaughter na behind the scene imeshaonekana Kwa Jamaa ipo Hela.Ile kwenda home,kuingia ndani kutafuta Beto na Kurudi pale pale kumvizia na kuchoma nimakusudi.
 
Back
Top Bottom