Neno la leo

Neno la leo

Naona akaunti ya huyu mshikaji imekuwa hacked! Mods liangalieni hili sio kwa mahubiri haya..
 
Naona akaunti ya huyu mshikaji imekuwa hacked! Mods liangalieni hili sio kwa mahubiri haya..
Ikumbuke siku ya Bwana Mungu wako kuitakasa...unajua ni amri ya ngapi hii?
 
šŸ™
 
Mwambie huyo.. hapo bado hujakutana na pisi kali mtoto jicho jicho! Bado hujakutana na kale ka balimi a.k.a kaondoa seteresi..! Na dhambi zilivyo huwa zinaalikana ukianza unzinzi itamualika uongo! Ikija pombe itamleta uzinzi n.k..
Vidimbwi vingi sana..🤣
Aaah nyingine tunazitakasa wenyewe kuwa siyo dhambi maana ni hitaji la muhimu kabisa.
 
KARIBU TUTAFAKARI PAMOJA NENO HILI

Watu wawili walikuwa wanakunywa pombe baa.

Wakati wanakunywa wakaanza kubishana na baadaye ule ubishi ukawa ugomvi.

Mmoja akamrukia mwenzake akaanza kumpiga.

Baada ya kumpiga kwa muda mrefu akagundua kuwa mwenzake hapumui tena.

Kumbe amemwua mwenzie.

Ndipo alipoanza kukimbia huku shati laki likiwa limechafuka sana na damu.

Wale waliyokuwa wanauangalia ule ugomvi wakaanza kumfukuza.

Huyu mwuaji akakimbilia kwenye nyumba ya mtu mmoja mcha Mungu na akamwomba yule mtu amfiche maana ameua mtu na watu walikuwa wanamfukuza.

Yule mcha Mungu akasema nitakuficha wapi wakati mimi nina chumba kimoja tu?

Yule mwuaji akamjibu akamwambia acha kuendelea kupoteza wakati fikiria tu mahali pa kunificha.

Yule mcha Mungu akavua shati lake safi akampa yule mwuaji alafu yeye akachukua lile shati la muaji lililojaa damu akalivaa.

Akampa sharti yule mwuaji na kumwambia tunza shati langu usilichafue.

Yule mcha Mungu alipofungua mlango wa chumba chake wale watu wakamvamia na kumpiga sana wakijua yeye ndo mwuaji huku mwuaji akiondoka salama na kurudi kwake.

Baada ya kumpiga sana yule ndugu akapelekwa polisi na baadaye akapelekwa mahakamani na akahukumiwa kunyongwa kwa kumwua mtu mwingine.

Yule mwuaji halisi akiwa kule nyumbani alijisikia vibaya sana akaenda mahakamani akajisalimisha akasema yeye ndiye aliyeua, yule ndugu aachiwe huru.

Hakimu akamwambia umechelewa, yule ndugu kesha nyongwa.

Alilia sana na kujiambia kuwa yule mtu amekufa kwa kosa ambalo sio lake.

Akakumbuka maneno ya mwisho ya yule ndugu "LITUNZE SHATI LANGU USILICHAFUE."

Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zako na zangu.

Alichukua vazi letu lililochafuliwa na uchafu wa dhambi zetu akatupa vazi Lake takatifu la haki.

Yesu aliuawa kwa kosa lako na langu.

Akatupa haki Yake na kutuambia tusichafue tena maisha yetu.

Kuendelea kutenda dhambi baada ya yale ambayo Yesu ametufanyia ni kuidharau sana kazi ya msalaba na kuikanyagia chini Damu Yake ambayo tumesafishwa kwayo.

Ni kushindwa kuthamini kuwa kuna mtu alishakufa kwa ajili yetu.

Ni kushindwa kutambua uthamani wa wokovu ambao tumeupokea.

Tutapataje kupona tusipojali wokovu mkuu namna hii.

LITUNZE SHATI LANGU USILICHAFUE.
Siamini kabisa km Leo hii Mshana umetoa ujumbe huu,yaani nimesoma mara mbili mbili kuthibitisha km ndio Wewe Kweli?.Aisee Mungu akubariki Sana Mshana Jr.
 
Siamini kabisa km Leo hii Mshana umetoa ujumbe huu,yaani nimesoma mara mbili mbili kuthibitisha km ndio Wewe Kweli?.Aisee Mungu akubariki Sana Mshana Jr.
Ni mimi mwenyewe kabisa...Neno linasema ikumbuke siku ya Bwana Mungu wako UITAKASE... Naheshimu sana neno la Mungu
 
Nimelipenda neno lako na Mungu akubariki. ninasema Amen. Yesu amenichukulia dhambi zangu na sasa ninaimba Halleluya.

Isa 1:18 SUV​

Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.
 
Nimelipenda neno lako na Mungu akubariki. ninasema Amen. Yesu amenichukulia dhambi zangu na sasa ninaimba Halleluya.

Isa 1:18 SUV​

Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KARIBU TUTAFAKARI PAMOJA NENO HILI

Watu wawili walikuwa wanakunywa pombe baa.

Wakati wanakunywa wakaanza kubishana na baadaye ule ubishi ukawa ugomvi.

Mmoja akamrukia mwenzake akaanza kumpiga.

Baada ya kumpiga kwa muda mrefu akagundua kuwa mwenzake hapumui tena.

Kumbe amemwua mwenzie.

Ndipo alipoanza kukimbia huku shati laki likiwa limechafuka sana na damu.

Wale waliyokuwa wanauangalia ule ugomvi wakaanza kumfukuza.

Huyu mwuaji akakimbilia kwenye nyumba ya mtu mmoja mcha Mungu na akamwomba yule mtu amfiche maana ameua mtu na watu walikuwa wanamfukuza.

Yule mcha Mungu akasema nitakuficha wapi wakati mimi nina chumba kimoja tu?

Yule mwuaji akamjibu akamwambia acha kuendelea kupoteza wakati fikiria tu mahali pa kunificha.

Yule mcha Mungu akavua shati lake safi akampa yule mwuaji alafu yeye akachukua lile shati la muaji lililojaa damu akalivaa.

Akampa sharti yule mwuaji na kumwambia tunza shati langu usilichafue.

Yule mcha Mungu alipofungua mlango wa chumba chake wale watu wakamvamia na kumpiga sana wakijua yeye ndo mwuaji huku mwuaji akiondoka salama na kurudi kwake.

Baada ya kumpiga sana yule ndugu akapelekwa polisi na baadaye akapelekwa mahakamani na akahukumiwa kunyongwa kwa kumwua mtu mwingine.

Yule mwuaji halisi akiwa kule nyumbani alijisikia vibaya sana akaenda mahakamani akajisalimisha akasema yeye ndiye aliyeua, yule ndugu aachiwe huru.

Hakimu akamwambia umechelewa, yule ndugu kesha nyongwa.

Alilia sana na kujiambia kuwa yule mtu amekufa kwa kosa ambalo sio lake.

Akakumbuka maneno ya mwisho ya yule ndugu "LITUNZE SHATI LANGU USILICHAFUE."

Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zako na zangu.

Alichukua vazi letu lililochafuliwa na uchafu wa dhambi zetu akatupa vazi Lake takatifu la haki.

Yesu aliuawa kwa kosa lako na langu.

Akatupa haki Yake na kutuambia tusichafue tena maisha yetu.

Kuendelea kutenda dhambi baada ya yale ambayo Yesu ametufanyia ni kuidharau sana kazi ya msalaba na kuikanyagia chini Damu Yake ambayo tumesafishwa kwayo.

Ni kushindwa kuthamini kuwa kuna mtu alishakufa kwa ajili yetu.

Ni kushindwa kutambua uthamani wa wokovu ambao tumeupokea.

Tutapataje kupona tusipojali wokovu mkuu namna hii.

LITUNZE SHATI LANGU USILICHAFUE.
Sasa si aliuawa na Shetani bro yake!! kwa kuwatumia wanadamu hawahawa!! huyu!! huyu shetani ni ndugu yake waliwahi kuishi wote Mbinguni wakitanua kwenye Milki ya Bwana Mungu, wakati huo shetani akiitwa Lucifa. kawaida shetani anajua sana mitaa ya mbinguni!! !! kulivo!!!! tokea kiti cha enzi kilipo!! kimekaaje!! kuliko mimi na wewe!

Yesu na Shetani wanajuana wanapiga story sana tu!! rejea pale shetani alipo mwambia Yesu amsujudie!!! hata Mungu anapiga story sana na shetani kama pale..

Mungu alimuuliza ''shetani unatoka wapi???
shetani akajibu ''natoka kuzunguka huku na huko Duniani!!....''

Unaona sasa Mungu anaongea na kiumbe chake bila kinyongo!! but hajawahi kuongea na wewe!!

wanadamu mna wivu na chuki na kiumbe chake alikiumba kwa gharama kubwa kuliko nyie miudongo!!! Yesu si alijua atakufa? kwa nini aliuendea Msalaba?? na kuleta taharuki?? ili iweje yaani aliamua kuchezea muda??

km wachawi wanaweza chukua msukule na kuweka limgomba hapo! na watu mkaamini ndugu yenu kafa!! Yesu alishindwa nini kumuwekea shetani limgomba tu! na yey kasepa zake juu!!

Kwa nini Mungu asiseme tu Imekwisha!! na ikawa? km alivoumba mbingu na nchi? kwa jinsi tunavomsikia Mungu wa Ibrahimu!!!! Kashetani hako ni nusu dakika sifuri anakamaliza!! kwa nini Mungu anamuogopa shetani!!

Mna tugeuza juu chini chini juu!! kwa nini Mungu hakutaka tule matunda ya mti wa kujua mema na mabaya? je alikuwa mchoyo wa kutugawia maarifa?? Shetani yeye akatupatia kirahisi tu!! nani mzuri hapo anaekupa Elimu?? au anaekunyima elimu?? uendelee kuwa mjinga??? nani mbaya nani mzuri

Ni kwa vipi unaamini Mungu atamfutilia mbali mwanae mpendwa shetani wakati amemuumba kwa gharama kubwa??? wewe unadhani kwa nini Mungu amemuacha anapeta humu Duniani na huko ahera? ulisha wahi sikia anaumwa huyu shetani?? lkn wewe unakisukari ukizembea dawa wafwa!!

wanadamu wana roho mbaya wanafurahia shetani ateketezwe siku ya mwisho! shetani wa watu kajikalia kimyaaa!! anatafakari msivompenda. Mungu si mwanadamu anaweza msamehe shetani!! sijui mtajisikiaje watu ambao hamkufaudu leo!!

Mlioamini shetani wake ni moto tu!! yaani mnaweza nyie kufa kwa jinsi mlivo na roho zenu!!
 
Ukiachana na neno hili zuri na muafaka kwa kipindi hiki cha wenzetu wakristo ambao wanatafakuri mateso ya bwana Yesu kristo na kufunga, Hujawai acha kunishangaza bwana Mshana Jr, Neno unalijua, uchawi na ndumba wazijua... hakika unajua kunichanganya ndugu yangu katika yote..
AYUBU 36:21-22

²¹ Jitunze, usiutazame uovu; Kwani umeuchagua huo zaidi ya taabu.

²² Tazama, Mungu hutenda makuu kwa uweza wake; Ni nani afundishaye kama yeye?

HILO NDILO NENO LA MUNGU
 
Back
Top Bottom