Neno La Leo: Mti Mmoja Mrefu Haufanyi Msitu!


si kweli ushindi wa narc ya kenya mwaka 2002 ulitegemea influence na sheer personality ya raila odinga bali ukweli ni kuwa vyama vikuu vya upinzani vya dp ya mwai kibaki na kile cha raila, cha bi charity ngilu na vyama vingine viliunganisha nguvu kwa kushirikiana na vigogo waliojiengua toka kanu akiwemo makamu wa rais george saitoti na waziri musalia mudavadi na kuweza kuitoa kanu madarakani!!
 

Kadogoo.
Nashukuru sana, hoja hiyo iliyopingana na yangu niliiona tangu siku ya kwanza nilipoanzisha mjadala huu. Kuna waliokimbilia kuiunga mkono kwa kunikejeli na kuhoji upeo wangu wa kufikiri. Nilichelea kuijibu nikihofia mjadala huu ungeelekezwa njia nyingine kama wachangiaji wa awali walivyotaka iwe. Nilijenga uvumilivu kusubiri mwingine afanye kazi hiyo. Nilikuwa na moja au mawili ya kuchangia katika dhana hii ya " Mti mmoja" na demokrasia yetu. Ngoja nitulie kwanza, labda wengine watasema niliyotaka kusema.
 

Kichuguu,

Unachoandika si sahihi. Sitamzungumzia Colonel Mjengwa. Sijakulia kwenye CCM, bali nimekulia kwenye siasa. Na wengine wanadhani tukiandika haya tunafikiria vyeo. Asubuhi hii nimetoka kumjibu mwenzetu huyu;

Originally Posted by Sir R

JK akishinda Mjengwa utakuwa DC

Majibu yangu;


Hata nikipewa dhamana ya U-RC nitasema; " Mheshimiwa, Asante sana, lakini HAPANA kwa sasa". Ndio, nina mke, na watoto wanaonihitaji zaidi katika makuzi yao. Kibarua ninachokifanya sasa na kipato changu, japo kidogo, kinaniwezesha kujikimu. Mimi ni mjamaa, na kamwe sijawahi kuupenda ubepari. Tatizo letu Watanzania ni hulka yetu ya kuangalia ' vyeo' na vyote vyenye kuambatana na vyeo hivyo, kama vile gari la fahari, safari za ndani na nje na posho. Badala ya kuangalia zaidi dhamana inayoendana na vyeo hivyo.

Ni ujinga pia, kudhani kila mtu anayefikiri tofauti , basi, ni fisadi au kanunuliwa na mafisadi.
 
Hiyo dhana yako unayozungumzia ya wapinzani kuungana haina maana yeyote ndungu Mjengwa. Kwanza kabisa kufananisha Kenya na Tanzania ni sawa na kufananisha Kunguru na Meza, hivi vitu havifanani hata kidogo. Siasa za Kenya zimejijenga katika Ukabila zaidi, kwa hiyo watu wa Kisumu wanavyomchagua Raila awachagui sera bali wanachagua kabila lao. Ndio maana inakuwa ni rahisi kuuunganisha wapinzani katika Kenya kwani unajua kabisa ukipata makabila matano makubwa basi nafasi ya kushinda inakuwa kubwa. CHADEMA haiwezi kupoteza muda kujiunga na vyama ambavyo viko on the verge of dying, vyama kama NCCR, TLP viko katika life support. Chama cha CUF kinafahamika ya kuwa graph yake inashuka chini kwa kasi sana huku bara. Trust me, vyama vingine vya upinzani with exception of CHADEMA vinaweza visipate hata mbunge mmoja mwaka huu, huku Bara.
 
Ni ujinga pia, kudhani kila mtu anayefikiri tofauti , basi, ni fisadi au kanunuliwa na mafisadi.
..but your timing of doing 'different thinking' is meticulously impeccable like an angel of death, isn't it?

Dude u can't fool us bana.
 
Mkuu, reality itabakia kwamba hao wote walikuja jiunga Narc kwa sababu ya ushawishi wa Raila Odinga kama ulivyo ushawishi wa Dr.Slaa isipokuwa tu hapa Tanzania bado watu wanafikiria CCM ni mama yao mzazi. Laukama Kibaki angekwenda KANU, bado KANU wangeshindwa na wameshindwa kurudi hata baada ya kupata watu wengine maarufu...

Wapo viongozi wengi sana ndani ya CCM wanamkubali Dr.Slaa lakini wameshindwa kujiunga naye tofauti na Kenya ambao viongozi wa Union na vyama walikubali kuungana.

Pengine yawezekana tungepata Muungano kama wa Kenya kama Chadema wangempendekeza Dr.Slaa mapema, lakini bado nina mashaka makubwa na ufahamu wa Mtanzania ktk maswala ya mustakabali wa Taifa letu kwani wengi wanafikiri bado hii ni dhamana ya CCM walorithi kutoka kwa mwalimu.
 
Kumbe mnalumbana?
Mi nlidhani mnashindana hoja
acid ndugu yangu,

ni nani alikwambia kuwa mimi ni mwandishi wa habari?
Au ni wapi nilipowahi kuandika kuwa mimi ni mwandishi wa habari?
Kama huna majibu ni vema ukapima mwenyewe kama uendelee na malumbano au la.
 

That's what separates you from me mkuu lol: I am a pure capitalist (not a socialist).I am Pro-environment, anti-Makamba and Lowassa (because I think they are very, very bad people); and most of all, I am a proud Tanzanian with elitist traits lol
 
Hivi nani bado anaamini kwa kuunganisha vyama ndipo ushindi dhidi ya sisi m ungewezekana? Nyie watu.......................... Nenda Iringa walikojaribu kuunganisha nguvu tena vyama vyote including sisi m dhidi ya Chadema kisha uje uniambie.
Vyama vyetu havijawa na utashi huo na umebaki ni wimbo mzuri ambao tune yake imeimbwa na sisi m miaka yote as if tunatakiwa kujifunza muungano wa vyama toka sisi m......na watu hapa wanataka kuingia mkenge. Shauri yenu...........
 
That's what separates you from me mkuu lol: I am a pure capitalist (not a socialist).I am Pro-environment, anti-Makamba and Lowassa (because I think they are very, very bad people); and most of all, I am a proud Tanzanian with elitist traits lol

Very interesting wajina. Lakini sijui wapi linakuja suala la usoshalist na u-capitalists, hakuna ubaya ukiwa capitalist au socialist ni sawa na kuwa mkrosto au mwislamu, la muhimu ni Tanzania yetu. Tunatakiwa kuipenda Tanzania kuliko hizo systems, Lowassa is a capitalist as well, Kingunge is aethist communist (as he said himself) but look at them, no one is mzalendo no one loves Tanzania. Yes, let us be proud of Tanzania, and more imprtant let us love it.
 
Hii dhana ya miti na mashamba ya Maggid inaweza kuwa-refuted kama tukiangalia nchi ya Rwanda kama case study yetu. Sio siri uchumi wa Rwanda unakuwa katika pace ya ajabu, uadilifu katika serikali ni mkubwa. Swali la kujiuliza, jee haya ni matokeo ya chama chenye makada wengi au kiongozi ambaye ni mwona mbali (visionary) na anayeweza kuweka maslahi ya taifa mbele.
 
..lakini CCM ni msitu wa mafisadi, na JK ndiye fisadi mkuu. sasa kwanini tuchague chama kilichosheheni mafisadi na kutegemea mabadiliko?

..kila aliye msafi akiingia huko CCM anaiga tabia ya ufisadi iliyokithiri ndani ya chama hicho.

..kama unaridhika na maendeleo tuliyofikia baada ya miaka 49 ya uhuru, pigia kura CCM. kama huridhiki basi chagua upinzani.
 
Magidd Nyerere aliitwa mwandishi mahiri wa vitabu na mfasiri kwa sababu ilikuwa hobby yake. Wewe pia ni mwandishi wa habari kwani huweka habari katika blog yako, you are blog journalist.. Ni kweli usikikwepe kivuli chako
Usemacho ni kwelije CCM inafuata nyayo za TANU? Kama ndivyo iwekje kampeni kuwa family issue. Hivyo hata hawa wakongwe pia wantaka tuamini msitu wa mti mmoja. It is mathematically correct but not in political science.
 

Asenti..

Huku ndio kukata mzizi wa fitna...hamna haja ya kuzunguka msituni kutranslate watu kuwa msitu na miti, and then back to watu wakati we have a job to do. Tuwaache njiani wale wasioona umuhimu wa kazi iliyopo mbele yetu, historia itawahukumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…