kikoozi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2015
- 2,030
- 2,930
Habari zenu ndugu zangu,
Mimi ni kijana wa miaka 37 kwetu tumezaliwa 2 tu, ila kuna ndugu zangu kama wanne (4) walilelewa na baba yangu mzazi katika makuzi yao, baada ya baba yangu kunifukuza nyumbani miezi 5 sasa imepita kisa tu nilimbembeleza kujiunga na chama changu cha mapinduzi, vile vile kupelekea kumfukuza na mama yangu pia ambaye alikuwa mara kwa mara uenda kudhuria vikao vya chama chetu cha mapinduzi, mimi nilimshauri mama yangu aende mahakaani kudai taraka ili waachane na baba wagawane mahari ili mimi na mama tukatafute sehemu yetu tukae tuepukane na manyanyaso ya baba
Mama baada ya kuondoka kwa baba alikuwa akikaa kwa dada yake ambaye anaishi maeneo ya Kijichi, sasa siku ya Jumamosi mama alinipigia simu kuwa anaenda kwa baba kudai taraka, baba akikataa kumpa taraka moja kwa moja anaenda mahakamani, siku ya Jumapili mama alienda moja kwa moja nyumbani kwa baba kudai taraka, ila kilichotokea ni kuwa mama tangu aende kwa baba pale nyumbani hajanijulisha chochote kile na nilikuwa nikipiga simu hapokei, jana jioni ndio aliniambia kuwa basi ameghailisha mambo ya taraka, ndugu zangu niliishiwa nguvu sana maana mama huwa ananisikiliza sana kwa kila kitu, nikahisi ndugu zangu watakuwa wanamchezea kiuchawi
Kumbukeni ndugu zangu sina kazi wala kibarua nahishi kwa marafiki tu, nimetafuta sana kazi bila mafanikio yeyote yale nina degree ya marketing nimesoma pale UDSM-UDBS, nilitegemea hiyo hela ya mama akigawana mali na baba baada ya kupewa taraka na mimi nipate mtaji, nimeumia sana ndugu zangu, mpaka kupelekea ndugu wa upande wa baba kuniita mimi mchawi
Naombeni mwenye kazi yeyote anisaidie ndugu zangu napitia hali ngumu sana kimaisha na baba hanitaki kabisa kwake kisa tu nipo chama cha mapinduzi na alinitimua wakati mimi ni mtoto wa pekee wa kiume kwake, nilishamshtaki ofisi za kata ila kata wakasema mimi sina akili timamu, na najua baba aliwapa pesa wale viongozi wa ofisi ya kata ili kunikomoa na kuto kunisikiliza malalamiko yangu
Kwa sasa nipo Dar es Salaam Boko. Mwenye connection anisaidie
Mimi ni kijana wa miaka 37 kwetu tumezaliwa 2 tu, ila kuna ndugu zangu kama wanne (4) walilelewa na baba yangu mzazi katika makuzi yao, baada ya baba yangu kunifukuza nyumbani miezi 5 sasa imepita kisa tu nilimbembeleza kujiunga na chama changu cha mapinduzi, vile vile kupelekea kumfukuza na mama yangu pia ambaye alikuwa mara kwa mara uenda kudhuria vikao vya chama chetu cha mapinduzi, mimi nilimshauri mama yangu aende mahakaani kudai taraka ili waachane na baba wagawane mahari ili mimi na mama tukatafute sehemu yetu tukae tuepukane na manyanyaso ya baba
Mama baada ya kuondoka kwa baba alikuwa akikaa kwa dada yake ambaye anaishi maeneo ya Kijichi, sasa siku ya Jumamosi mama alinipigia simu kuwa anaenda kwa baba kudai taraka, baba akikataa kumpa taraka moja kwa moja anaenda mahakamani, siku ya Jumapili mama alienda moja kwa moja nyumbani kwa baba kudai taraka, ila kilichotokea ni kuwa mama tangu aende kwa baba pale nyumbani hajanijulisha chochote kile na nilikuwa nikipiga simu hapokei, jana jioni ndio aliniambia kuwa basi ameghailisha mambo ya taraka, ndugu zangu niliishiwa nguvu sana maana mama huwa ananisikiliza sana kwa kila kitu, nikahisi ndugu zangu watakuwa wanamchezea kiuchawi
Kumbukeni ndugu zangu sina kazi wala kibarua nahishi kwa marafiki tu, nimetafuta sana kazi bila mafanikio yeyote yale nina degree ya marketing nimesoma pale UDSM-UDBS, nilitegemea hiyo hela ya mama akigawana mali na baba baada ya kupewa taraka na mimi nipate mtaji, nimeumia sana ndugu zangu, mpaka kupelekea ndugu wa upande wa baba kuniita mimi mchawi
Naombeni mwenye kazi yeyote anisaidie ndugu zangu napitia hali ngumu sana kimaisha na baba hanitaki kabisa kwake kisa tu nipo chama cha mapinduzi na alinitimua wakati mimi ni mtoto wa pekee wa kiume kwake, nilishamshtaki ofisi za kata ila kata wakasema mimi sina akili timamu, na najua baba aliwapa pesa wale viongozi wa ofisi ya kata ili kunikomoa na kuto kunisikiliza malalamiko yangu
Kwa sasa nipo Dar es Salaam Boko. Mwenye connection anisaidie