Ndugu wa Tanzania Mnakielewa chanzo cha Misukosuko ya Nchi? (Ali H. Mwinyi)

Mimi nampenda asieruhusu uongo lakini pia simpendi asiesema kweli kama wewe.
Hili la TV (Kabla ya kuendelea ningeomba umri wako pengine hayo mambo umehadthiwa) linaukweli na aliloandika huyo unaemsuta. Naomba unijibu TV wakati huo zilikuwa zinauzwa duka gani? Kwa faida ya wanataka ukweli ni kuwa zilikuwa TV za magendo zilizoibwa Zanzibar.
Jambo la pili jee unakumbuka suwala la Wahujumu? Uliza watu watakueleza jinsi gani watu walivyotupa majalalani MaTV, sasa wakiogopa kitu gani kama ilkuwa ruksa?

TV hazikuwa zinauzwa Tanzania na kuna vitu chungu nzima ambavyo vilikuwa haviuzwi Tanzania watu waliruhusiwa kuviingiza kama walifuata taratibi zilizowekwa. Hao wote walioamua kutupa TV zao waliziingiza kwa njia za panya ili kukwepa kulipa ushuru waliostahili kulipa, hivyo walikuwa hawana documents zozote za kuthibitisha kama TVs zao waliziingiza nchini kihalali. Nakumbuka kuhusu Wahujumu na kweli kulikuwepo wahujumu wa uchumi ambao walikuwa wanakwepa kulipa kodi na kuikosesha Serikali mapato ya mabilioni. Walikuwa wanahodhi bidhaa mbali mbali adimu na kuziuza kwa bei mbaya sana ili kukidhi uroho wao wa utajiri wa haraka haraka. Walioingiza TVs zao kwa kufuata taratibu zilizowekwa ikiwa na pamoja na kulipia ushuru hawakutupa TVs zao. Wakati mwingine muwe mnaandikia ukweli badala ya kuandika uzushi ambao hauna ukweli hata kidogo.
 
TV hazikuwa zinauzwa Tanzania na kuna vitu chungu nzima ambavyo vilikuwa haviuzwi Tanzania watu waliruhusiwa kuviingiza kama walifuata taratibi zilizowekwa. Hao wote walioamua kutupa TV zao waliziingiza kwa njia za panya ili kukwepa kulipa ushuru waliostahili kulipa, hivyo walikuwa hawana documents zozote za kuthibitisha kama TVs zao waliziingiza nchini kihalali. Nakumbuka kuhusu Wahujumu na kweli kulikuwepo wahujumu wa uchumi ambao walikuwa wanakwepa kulipa kodi na kuikosesha Serikali mapato ya mabilioni. Walikuwa wanahodhi bidhaa mbali mbali adimu na kuziuza kwa bei mbaya sana ili kukidhi uroho wao wa utajiri wa haraka haraka. Walioingiza TVs zao kwa kufuata taratibu zilizowekwa ikiwa na pamoja na kulipia ushuru hawakutupa TVs zao. Wakati mwingine muwe mnaandikia ukweli badala ya kuandika uzushi ambao hauna ukweli hata kidogo.

Wewe unanikumbusha wale watu wanaojamba, halafu baada ya sekunde tano anaanza kuuliza kinanuka nini hapa.

Sasa wewe umeona ni utetezi kwenye fikra zako eti kumiliki kaTV set tu sharti kuambatane na mlolongo wa taratibu including vibali vya akina Butiku na marehemu Kolimba, ambao wakati mwingine walikua wanakataa... Kweli JF ni ukumbi wa Great Thinkers!
 
TV hazikuwa zinauzwa Tanzania na kuna vitu chungu nzima ambavyo vilikuwa haviuzwi Tanzania watu waliruhusiwa kuviingiza kama walifuata taratibi zilizowekwa. Hao wote walioamua kutupa TV zao waliziingiza kwa njia za panya ili kukwepa kulipa ushuru waliostahili kulipa, hivyo walikuwa hawana documents zozote za kuthibitisha kama TVs zao waliziingiza nchini kihalali. Nakumbuka kuhusu Wahujumu na kweli kulikuwepo wahujumu wa uchumi ambao walikuwa wanakwepa kulipa kodi na kuikosesha Serikali mapato ya mabilioni. Walikuwa wanahodhi bidhaa mbali mbali adimu na kuziuza kwa bei mbaya sana ili kukidhi uroho wao wa utajiri wa haraka haraka. Walioingiza TVs zao kwa kufuata taratibu zilizowekwa ikiwa na pamoja na kulipia ushuru hawakutupa TVs zao. Wakati mwingine muwe mnaandikia ukweli badala ya kuandika uzushi ambao hauna ukweli hata kidogo.


Naendelea kusema tena kuwa sipendi wasiosema kweli.
Kama ulisikia suala la wahujumu basi waulize walioona na watakwambia ukweli wa yaliyotokea wakati huo. Ni aibu tupu kuielezea hali hiyo. Pengine huko mlikokuwepo hayo hayakutokea kwani kulikuwa hakufiki sabuni ya manukato au kitu chochote kilichoitwa "cha anasa"
 
Mzee mwinyi hawezi kulaumiwa kwa kila kitu alipokea nchi ikiwa imekwama kwa hiyo alicho weza kufanya alijitahidi.

Tatizo la mkapa ni kweli alileta mabadiriko ktk utawala na ukusanyaji wa kodi lakini ameiba sana.

Kikwete amejaribu kuwa neutral kwa maana kwamba anaogopa kufanya baadhi ya maamuzi akihofia kutumbukia alikokuwa mkapa lakini sasa amekuwa mwoga kupindukia.

Kwa sasa kama kikwete anataka kufanikiwa ktkawamu ijayo basi amteue Dk. Magufuli kuwa waziri mkuu.
 
sijakuelewa eti sera ya soko huria ilipitishwa 1984 lakini nyerere akaamuwa angatuke? Hakuwa na ubavu wa soko huria?
Bado alisimamia sera hiyo!

Acheni kumsifia Mwinyi bana! Mwinyi nae ni fisadi tu, kwenye utawala wake ndiko ambako kina Aaga.bacholi kabila la RA walikoibukia.

Mnajua kitu kinaitwa Structural Adjustment Programme?

Mwinyi ni fisadi tu, Sitti ndo alizidi, kampiga bao hadi mke wa BWM
 
aCHENI KUMSIFIA mWINYI BANA! mWINYI NAE NI fISADI TU, Kwenye utawala wake ndiko ambako kina Ma********* kabila la RA walikoibukia.

MNAJUA KITU KINAITWA STRUCTURAL ADJUSTMENT pROGRAMME?


Muungwana hamnyimi haki anaestahiki! Tanzania ni nchi na wala si mchezo wa kuigiza. Ni miaka 48 sasa tangu tuanze kutawaliwa na wananchi wenzetu na tumeongozwa na watu mbali mbali. Viongozi hao ni binaadamu na wana mabaya yao na mazuri yao lakini mtu husifika kwa yale yalio mazuri. Huo ndio utaratibu wetu binaadamu lakini kwa vile sote hatukutimia wapo wenye mushkeli kama nyinyi ambao hamfuati mkondo wa tabia ya binaadamu. Pengine kwa udhaifu huohuo wa kibinaadamu wapo wasiojuwa mambo lakini wakajifanya wanajuwa> Pengine u moja wa makundi hayo juu. Poleee!
 
Black Jesus unaufahamu msemo wa 'Shukurani za Punda mateke?' Basi ndio baadhi yenu nyinyi.

Enzi zile kila kitu ilikuwa foleni foleni foleni - sabuni ya mawingu kwa foleni, vitenge TZ yote inavaa aina moja nayo ni kwa foleni. Watu walifikia hata kuvaa mifuko ya unga ngano (enzi zile mifuko ya kg 50 ilikuwa ya vitambaa), kuwa na TV au friji ni haramu, gari kuendesha mwisho saa nane mchana siku za jpili, kuwa na dola za kimarekani au foreign currency yo yote ni uhaini.

Sera ya ujamaa na kujitegemea ni nzuri kinadharia lakini kiuhalisia haifanyi kazi. Na huo ni ukweli nyinyi vijana wa leo mubaki kuimba tu na kukumbuka mabaya badala ya kushukuru kwa yale maendeleo yaliyofanyika kwa kubadilisha sera zile.

You are taking too many things for granted.

You must be out of your mind??? ndiyo auze loriondo??? ache wehu
 
Huyo huyo Great Thinker ndiye aliyeuza mbuga zetu za Loliondo kwa Waarabu. Alaaniwe!
Ufike wakati tuwe wakweli na tumuogope mungu !! Hawa wazee Nyerere na Mwinyi binafsi nawaheshimu nikilinganisha na waliowafuatia. Sababu ni kwamba kila binadamu ana makosa yake, lakini watu (viongozi) huhukumiwa sio kwa makosa waliyo yafanya ila nia wakai wa kufanya makosa hayo. Kazi ya kiongozi ni kuamua. Kuna nadharia inasema bora kuamua vibaya kuliko kushindwa kutoa maamuzi, kama kiongozi kushindwa kuamua ni kushindwa kuwajibika.

Nyerere kwa mfano kaitoa nchi hii huko alikoitoa hakuwa na mfano mbele yake unaambiwa nchi ilikuwa na madokta wasiozidi wanne nchi nzima, engineers pia na wataalamu wengine. Utaona jinsi mambo yalivyokuwa magumu. Ndio maana hata mtu akiharibu kazi watu wakimlalamikia alikuwa anahamishiwa sehemu nyingine, hii ilikuwa busara ya wakati utafukuza wote na wote bado wanajifunza utatoa wapi wengine?

Tukija kwa mzee wetu Ruksa, yeye kwa wakati wake alikuja kusolve lililoonekana tatizo kubwa kwa wakati ule. Ambalo lilikuwa ukosefu mkubwa wa bidhaa muhimu kuliko tokana na mdororo wa uchumi baada ya athari ya vita vya Uganda. Hiyo ndiyo ilikuwa vision ya wakati kwangu mimi anastahili pongezi kwa wakati wake.

Kulikuwa na kashfa hatuwezi kukataa lakini hazikuwa za wazi na za kijinga kama tuonavyo sasa. Mikataba mingi ya upotevu wa rasilimali zetu kama taifa zimeingiwa wakati wa mkapa. Kuhusu mashirika ya umma ndio usiseme. NBC inaniuma hadi leo ni hivyo cha kufanya tu ndio sina.

Tunajaribu kuwasamehe wazee wetu hawa kutokana na wakati na nia njema walizokuwa nazo kwa taifa hili. Nyerere angekuwa mwizi tusingekuwa na kitu chochote hapa. Hata kiwira isinge kuwepo.
 
Acheni kumsifia Mwinyi bana! Mwinyi nae ni fisadi tu, kwenye utawala wake ndiko ambako kina Aaga.bacholi kabila la RA walikoibukia.

Mnajua kitu kinaitwa Structural Adjustment Programme?

Mwinyi ni fisadi tu, Sitti ndo alizidi, kampiga bao hadi mke wa BWM
Anayebisha ni nani kwamba wakati wa mwinyi hakukuwa na ufisadi wa hali ya juu?
Nchi mpaka iliishiwa na pesa za kutumia!
Ni kwenye utawala huu dhahabu ilikuwa inavushwa kwa ndee bila aibu mcha kweupeeeeeeeeee!
hata mwinyi alikuwa fisadi na aliwafanya watanzania wengi wawe mafisadi kwa kuwapa ruksa ya kufanya ufisadi.
 
Huyo huyo Great Thinker ndiye aliyeuza mbuga zetu za Loliondo kwa Waarabu. Alaaniwe!

Nilijua tu utaleta udini acheni mambo yenu

Nyerere alileta hujumu uchumi kwa ajili gani kama si nchi kumshinda
Maduka ya ushirika mwisho kununu kilo moja sukari duh

Kwani wewe sasa hivi unaweza kukataliwa kununua zaidi ya kilo Moja?

Hiyo ni faida iliyoanzia kwa Mzee wetu mwiniyi angefuata sheria hizo za aliye pita usingekuwa hopo ulipo
 
Anayebisha ni nani kwamba wakati wa mwinyi hakukuwa na ufisadi wa hali ya juu?
Nchi mpaka iliishiwa na pesa za kutumia!
Ni kwenye utawala huu dhahabu ilikuwa inavushwa kwa ndee bila aibu mcha kweupeeeeeeeeee!
hata mwinyi alikuwa fisadi na aliwafanya watanzania wengi wawe mafisadi kwa kuwapa ruksa ya kufanya ufisadi.

Sio wakati wa mwinyi tu Hata wakati wa nyerere ulikuwepo tu tafuta hotuba ya waganda walioitowa wakati wa mazishi ya Simba wa Vita ukweli mtupu umemwagwa wa choko choko za vita
 
Ama kweli, tunasahau mno upesi! Sera ya soko huria ilipitishwa 1984, Mh Alhaji Mwinyi alichaguliwa kuongoza nchi 1985! Uamuzi wa watanzania wa au kuwa na sera ya vyama vingi ama la ulipigiwa kura (referandum) na wengi wakataka wabaki na chama kimoja, Nyerere akalazimisha pamoja na haja ya kuheshimu demokrasia, nchi haikuwa na budi walau wakati ule kuupa uzito uamuzi wa wachache yaani kuchagua kuwa na sera ya vyama vingi. Ni pale Zanzibar tu ambako hatujui kilichojiri, hakuna sera yeyote iliyowekwa wazi pale, ni vurugu tu! Sasa wewe Bimkonge na wengine, mnawezaje kudhani Mwinyi ndiye aliyeboresha sera wakati unaona kabisa Nyerere akiwa ni kinara wa kuleta soko huru (1984) na sera ya vyama vingi(1991)?

Lakini yote tisa, sera na mfumo sio miliki ya mtu mmoja!!! Hata huko Marekani, hakuna kinachobadilika eti tu kwa kuwa yupo Obama, yale yale yanaendelea, ni harafu tu ya juu tunayoona kama kihalalisho cha kuwepo aliye katika madaraka....habari ndio hiooo

Nilipoona hii topic nilikpata mawazo kama yako. Watu wamesahu kwa nini Salimu A Salimu ana historia. Soko za sera hulia zilikuja na 1984 wakati SA Salim akiwa waziri mkuu baada ya ya Sokoine (RIP). Tukubali tukatate wakati wa Mwinyi mambo yalikuwa ya chukua chako mapema. Watu wanasahau mapema!!!
 
Naendelea kusema tena kuwa sipendi wasiosema kweli.
Kama ulisikia suala la wahujumu basi waulize walioona na watakwambia ukweli wa yaliyotokea wakati huo. Ni aibu tupu kuielezea hali hiyo. Pengine huko mlikokuwepo hayo hayakutokea kwani kulikuwa hakufiki sabuni ya manukato au kitu chochote kilichoitwa "cha anasa"

Sasa wewe ulitaka wakati nchi inakosa mapato kutokana na wahujumu wa uchumi kuhodhi bidhaa adimu zikiwemo vyakula na kuikosesha Serikali mapato chungu nzima kiasi ambacho cha kukaribia kushindwa kujiendesha, ulitaka tuagize sabuni za manukato au vitu vya anasa! na wewe hayo unayaona ni maendeleo! Kweli vipaumbele vyako vimekaa kushoto sana. Wakati wa Nyerere hakukuwa na viongozi wenye uroho wa utajiri wa haraka haraka kama tunavyoona leo ambao wanatumia nafasi zao kuifisadi nchi kwa mabilioni ya fedha na kuziweka nchi za nje. Nchi iache kuagiza chakula na madawa bali iagize sabuni za manukato! unachekesha kweli! Ungekula sabuni za manukato kama ungekuwa huna chakula?
 
Wewe unanikumbusha wale watu wanaojamba, halafu baada ya sekunde tano anaanza kuuliza kinanuka nini hapa.

Sasa wewe umeona ni utetezi kwenye fikra zako eti kumiliki kaTV set tu sharti kuambatane na mlolongo wa taratibu including vibali vya akina Butiku na marehemu Kolimba, ambao wakati mwingine walikua wanakataa... Kweli JF ni ukumbi wa Great Thinkers!

Ndiyo nyie ambao mnasimama na kumtetea mwinyi kwa sababu tu ni muislamu mwenzenu na wengine mkidai eti wakristo wanataka kumweka mkristo mwenzao ndiyo maana wanampiga vita Kikwete! Kwa maana nyingine mnaridhika na utendaji ZERO wa Kikwete kwa kuwa tu ni muislamu mwenzenu! Nyerere alipendelea wakristo wenzake. Makubwa haya!
 
mimi sikuelewi mshikaji unapomlaumu Ali Hassan kwa azimio la Zanzibar. Kwani azimio ndio linalosababisha watu kuiba?. Au ni hulka za watu tu?. Matatizo ya Tanzania yalianza pale Julius aliposhika hatamu na kuleta siasa za ujamaa ndani ya nchi ambayo siyo ya ujamaa. Sisi waafrika tulikuwa na namna zetu za kuendesha mambo yetu wala sio ukosefu wa siasa potofu za ujamaa. Nitakueleza mengi lakini kwa sasa nakwambia tena, wakulaumiwa yuko kaburini na jina lake ni Julius Kambarage Nyerere.
 
Until now there are two types of Tanzanians. First, there are those who blame Nyerere, ujamaa and Azimio la Arusha for our current economic woes. And then there are those who lament Mwinyi, Rukhsa and Azimio la Zanzibar for ethical decay of effective leadership and widespread corruption.

The truth is what Nyerere and Mwinyi preached weren’t engraved on stones by the finger of God and then placed into a golden box. Therefore, you have the right to change course.
 
Sasa wewe Ujengelele naona hayo mambo umehadithiwa paukwa pakawa. Nani alisema anamtetea Mwinyi kwa sababu ni muislamu? Na nani alisema kwamba Mwinyi amefanya mazuri kwa asilimia mia moja au Nyerere amefanya mabaya yote? Acha hizo lete hoja usilete udini.

Hizo za miaka ile upungufu wa mafuta ulikuwa Tanzania tu? Na hao wahujumu uchumi ndio walikuwa wanaomiliki TV na friji? Sera za wakati ule zilionesha dhahiri kwamba zimefeli na ikabidi zibadilishwe. Angalia wenzetu wa Malaysia na Indonesia ambao tulipata uhuru katika kipindi kimoja, sasa kimaendeleo wako wapi?
 
Sio wakati wa mwinyi tu Hata wakati wa nyerere ulikuwepo tu tafuta hotuba ya waganda walioitowa wakati wa mazishi ya Simba wa Vita ukweli mtupu umemwagwa wa choko choko za vita
Sikiliza bwana we! Nyerere alikuwa mtu anayechukua maamuzi magumu. Waliokuwa wakijaribu kufanya hivyo walifanya kwa woga sana na alipowagundua aliwashughulikia kikweli.
Watu walifikia mahala wanajenga nyumba kwa majina ya marafiki zao. Wanafungua biashara kwa majina ya jamaa zao tu, kama ilivyofanywa kwa wakina Gachuma.
Sio hawa wanaomuuliza Mr President "wewe umeshatengeneza shiling ngapi toka uingie madarakani?"
 
Anayebisha ni nani kwamba wakati wa mwinyi hakukuwa na ufisadi wa hali ya juu?
Nchi mpaka iliishiwa na pesa za kutumia!
Ni kwenye utawala huu dhahabu ilikuwa inavushwa kwa ndee bila aibu mcha kweupeeeeeeeeee!
hata mwinyi alikuwa fisadi na aliwafanya watanzania wengi wawe mafisadi kwa kuwapa ruksa ya kufanya ufisadi.



Wacha kujidandanganya kuwa katika historia ya Tanzania kuna wakati hakukuwa na ufisadi.
Tuanze na wakati wa Nyerere tulipopata uhuru tulikuwa na rasimali nyingi na nchi ilikuwa na vitega uchumi vingi. Viwanda vya kila bidhaa, mashamba yenye kuzalisha vizuri, migodi iliyokuwa na neema na vingi vyenginevyo. Vitu hivi vyote vilipotea hadi kufikia kuwa ombaomba na kufa kwa njaa. Ni nani alivihujumu hivi? (Kwa wale Kiswahili kidogo kina tabu kwao ni kuwa Hujuma ni sawa na ufisadi) Jee si Nyerere mwenyewe aliyekubali kuwepo kwa Wahujumu? (Kumbukeni vita vya Wahujumu, fyagio la Chuma na hatuwa nyengine ambazo hazikuzaa matunda.

Tukija wakati wa Mwinyi mbona mwenyew amekuwa akikiri kuwa jitihada zake pia ziliingiliwa na ufisadi ( Sasa ndio awe yeye chanzo wakati hata utawala wa mwanzo walikiri ufisadi?)

Tawala zilizofuata nafikiri hakuna haja ya kuzijadili kwa hilo kwani zinanuka kwa ufisadi. Kwa vile Thread hii inazungumzia chanzo cha ufisadi na matatizo ya nchi nafikiri hatumtendei haki kati ya waasisi yaani Mwinyi na Nyerere kuwalaumu na si haki kumpamba mmoja na kurushia lawama mmoja.
 
Sikiliza bwana we! Nyerere alikuwa mtu anayechukua maamuzi magumu. Waliokuwa wakijaribu kufanya hivyo walifanya kwa woga sana na alipowagundua aliwashughulikia kikweli.
Watu walifikia mahala wanajenga nyumba kwa majina ya marafiki zao. Wanafungua biashara kwa majina ya jamaa zao tu, kama ilivyofanywa kwa wakina Gachuma.
Sio hawa wanaomuuliza Mr President "wewe umeshatengeneza shiling ngapi toka uingie madarakani?"


Naona taratibu unaanza kuachia au sivyo? Sawa umeshakubali kuwa ufisadi ulikuwepo, sasa na tuangalie huo uamuzi mgumu na mkali aliofanya Nyerere ulisaidia kiasi gani kwa maendeleo ya Tanzania? Ni kweli tulishuhudia Nyerere akitowa hutuba kali lakini hebu tujiulize nani mwenye uwezo na nafasi nzuri ya kufisadi? Sasa natujiulize wakati wake Kigogo gani tuliona akichukuliwa hatuwa za mfano kama wakati huu? Jambo jengine ni kujiuliza!Nyerere na ukali wake aliweza kuliokowa Taifa na kufilisika kulikosababishwa na ufisadi?
 
Back
Top Bottom