Yashangaza sana anashtaki kwa nani? Ili iweje? jituuu kuubwa bure tu...kama una hoja mwenyewe ya kumpinga Kimbunga si uandike tuone na si kukimbilia ku single out oooh wewe magwanda huyu vile....grow upSoma post kwa umakini siyo unakimbilia kujibu tu. Kwa hiyo kama mimi ni magamba unashitaki kwa nani? Huu ni mtandao wa kijamii na watu tunabadilishana mawazo humu na si mtandao wa Chama chochote uwe na chama usiwe na chama unaingia tu huulizwi!!
Bunge lililopita (namaanisha lile ambalo Sitta alikuwa speaker) lilivutia sana na sikupenda kupitwa na mijadala iliyokuwa inaendelea mule ndani. Tofauti na leo ambapo kila siku ya Mungu kuna kituko. Bunge limekuwa kama primary school vile ambapo mbabe anaweza kumkaba mwenziye,, kisa.....yeye mtemi.
Sasa sijui sababu ni speaker kuzidiwa, au wenyeviti nao kuzidiwa? Lakini pia pengine tuliamini kuingiza vijana bungeni kwa vyama vyote kungeleta tija na kasi ya haraka kuelekea mageuzi ya kweli ya maendeleo?? Nadhani hali imekuwa kinyume,, tuliyoyashuhudia kipindi hiki, ni aibu kuu na ni utovu wa nidhamu kutoheshimu kanuni za Bunge. Bunge linaendeshwa kwa kanuni na si kiholela kama wengine wanavyotaka liende. Nilitamani siku za mbele nigombee lakini sasa sitaki tena, nafsi imeingia jivu, bora niendele na umachinga tu.