Ndoto za mabinti wengi ni harusi

Ndoto za mabinti wengi ni harusi

Na ndio maana ndoa zinavunjika sana kwa sababu akili zao zinaishia kwenye vazi jeupe na suti ya bwana harusi, ukitongoza tu binti siku hizi unaanza kuitwa mume wangu inaniboa sana hiyo tabia.
It mean , wanaoishi bila harusi wana long survival kuliko waliopitia tukio la harusi
 
Wengi wetu tunapenda show off na kwa utafiti katika jamii niliyopo tunapenda sana sherehe ndo maana ndoa za kileo zimejaa malumbano yasiyoisha

Na kwa akili hizo ndo yaleee harusi leo baada ya mwaka wameachana

Wengi waliobariki ndoa naona kama wanayaishi maisha halisi ya ndoa
 
Unaweza kufunga ndoa isiyo na gharama yeyote na still ndoa isidumu.na unaweza pia funga ndoa ya gharama sana na ikadumu.hakuna guarantee. Kama kuna pesa let them wish big for their big day.wacha wacomplicate wacha movie icheze vichwani mwao.but wahakikishe tu KWAMBA THEY REAL LOVE EACH OTHER KABDA YA KUSEMA I DO NA KUKEEP THAT WEDDING VOW.
 
Nimekuelewaa sana mkuu na umetusaidia sana,pia kujiuliza hayo maswali.

Lakini sehemu mija sikubalian na ww.sijui kukopi ila naandika.nakunukuu "Ukoo wao uwe wangu,ndugu zake wawe wangu,mungu wao awe wangu.

~Hapo penye mungu wao awe wangu akiwa JEHOVA sawa,ila km sio hicho kipengele kwangu sita kubaliana nacho maisha yote.
 
Umezungumzia Mabinti na mimi nitazungumzia mabinti.
Ni kawaida kwa Binti kuwa na ndoto za siku yake ya harusi na wengi hii ndoto huwa nayo tokea wakiwa wadogo, kwenye miaka 10,11,12, na kuendelea.

Sababu ziko nyingi na kila Binti anayo yake ya kipekee, wengine hizi ndoto zinatokana na kusoma vitabu na wengine kuhudhuria harusi wakiwa angali watoto na kuona jinsi gani BIBI HARUSI anavyopendeza na kupewa attention katika siku hiyo. Na mpaka hiyo siku itimie bado atakuwa ndoto yake haijakamilika.

Sababu nyingine ni kupenda sherehe tu na kuona fahari jinsi gani atakavyo kusanya watu wakusherekea naye.
Kitendo cha kuvuka daraja na kuitwa mke wa mtu nayo inaweza kuwa sababu, na kile kitendo cha kuweka ahadi mbele ya kadamnasi kuwa huyu ndio kipenzi changu wa kufa na kuzikana ina mpa faraja hakuna wa kumnyanganya tena.

Msiwakimbie MAbinti kwa sababu hizo, maana mabinti wengi hii ndoto wanayo sema sio wote wanaiweka wazi wazi, sitashangaa kusikia na kina Kaka pia wameanza kuwa na ndoto hizi maana hakuna mtu asiyependa siku yake ya Harusi.
 
Wengi wetu tunapenda show off na kwa utafiti katika jamii niliyopo tunapenda sana sherehe ndo maana ndoa za kileo zimejaa malumbano yasiyoisha

Na kwa akili hizo ndo yaleee harusi leo baada ya mwaka wameachana

Wengi waliobariki ndoa naona kama wanayaishi maisha halisi ya ndoa
Kuna ndoa ilidumu miezi 3 jamaa kasema cwez kuishi na mwanamke km wewe n zaid ya mnyama
 
Wanawake hasa hawa wa kileo wanasahau kuwa ndoa si harusi, ndoa ni baada ya harusi kuisha.

ndipo hapo baada ya harusi wakianza kuishi uhalisia wa ndoa wanaanza kukutana na challenge za ndoa... badala ya kupambana nazo,wanazikimbia. mwishowe ndoa hazidumu.
 
Back
Top Bottom