Ndoto yangu ni kuajiriwa na CRDB

Mm mwenyewe kuna kampuni nilikuwa nafanya nayo kazi nikaapa sito apply tRNA kazi mahala pengine bali nikitoka pale nitajiajiri mwenyewe......kweli sikuwahi kuapply kazi yeyote nikiwa nafanya nao kazi......weee!.... Dude LA magufuri likaikumba kampuni hatimaye kampuni inaenda kufa....watu tukapewa tubarua mdogo mdogo kwamba tuanze kuangalia shughuri zingine....na tupo huku tunaangalia ahughuri zingine...usijipe matumaini makubwa hivyo!!!!!!!!
Umeona eeee flexibility muhimu sana
 
Maisha ya kuwa na shauku ya kutimiza ndoto ni udanganyifu wa ulimwengu na kumuasi Mungu.

Hatupo kutimiza ndoto zetu katika hii Dunia. Hatukujiumba na wala Dunia si mali yetu hata tupange mambo yetu binafsi.

Maisha halisi ni kumtumainia Mungu pekee. Ndoto zako ziwe ni kumpendeza Mungu na kufuata maelekezo yake kama Kitabu chake (BIBLIA) Kinavyoelekeza kuishi. Kitabu hiki chenye maelekezo ya Mungu kinasema" Bali utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake, na hayo yote mtazidishiwa". Hayo yote ikimaanisha chakula, mavazi n.k (Kiufupi ni mahitaji ya mwili).

Maisha ya kufuata ndoto zetu(Wanadamu) si mpango wa Mungu. Ni uasi wa Wanadamu kwa Mungu. Kuishi kwa kutimiza ndoto binafsi ni kumuasi Mungu, kwa sababu inakufanya kufanya lolote hata lililo kinyume na Mapenzi ya Mungu ili kufikia ndoto zako.

Maisha sahihi ni kumjua Mungu. Kumuabudu yeye. Baada ya hapo sasa unamwambia haja zako na unasubiri mapenzi yake yatimizwe na siyo kulazimisha maono yako binafsi yatimie au kufanyika. Huko ni sawa na kumpangia Mungu kazi. What if kama siyo mapenzi ya Mungu kwako kufanya kazi CRDB? . Simaanishi ukae bila kufanya kazi. Namaanisha kumtanguliza Mungu kwanza katika mapito yako. Kisha kumsikiliza Mungu kuhusu mpango wake kuhusu maisha yako.

Ukimfuata Mungu sawa na neno lake, hutakosa namna ya kula wala kuvaa. Maana yeye hufanya njia pasipo na njia. Ni hayo tu ndugu. Kubali kubadilika. Ujanja wa mwanadamu wa Fikra ikiwemo mafundisho mapotofu ya kutimiza ndoto zetu yasikufanye mpofu na kudhani hayo ndiyo mpango wa Mungu katika maisha yako. Huu ni ushauri tu, ushauri hukubaliwa au kukataliwa. Siyo lazima ukubali nilichosema. Ila kweli ya Mungu itabaki paleplae siku zote. Hautobadilika.!
 
Kwa sasa ukiji ajiri kuna uwezekano mkubwa sana wa kufanikiwa kwa mda mfupi.
LAZIMA NIJIAJIRI kwasababu na uchu wa mafanikio.....lakini kusoma kwangu mpaka chuoo nilikua na ndoto ya kufanya kazi katika bank ya CRDB...NDIO MAANA nikaenda IFM kusoma banking and finance baada ya kufauru vizur form six...nilibahatika kufanya field katika branch moja...
Kwa sasa ni muda tu tangu nipeleke aplication letter lakin hawajawahi niita...ROHO INANIUMA SANA sababu ndo ilkua ndoto yangu .

Naamini wapo wakurugenzi wa pale....naomba mnisaidie kukamilisha ndoto yangu(NITAFURAHI MAISHA YANGU YOTE)

Baada ya hapo naweza nikawa happy hata kujiajiri pia ntajiajiri

[HASHTAG]#SAIDIA[/HASHTAG] KUFANYA NIISHI KWENYE NDOTO ZANGU##
wewe sio mchaga?
 
...kama vipi anzia hata Access ujenge network mnyalu!
.simamia ndoto yako,itatimia inshaAllah!
 
Kweli maisha yanatofautiana sana,me binafsi sipendi kabisa kazi za bank.
Ume apply NMB imeshindikana ,Kazi huna, Umewapikia ndugu zako Nyumban wanaofanya kazi umechoka, Umezurula kila ofisi Posta Dar imeshindikana, Sasa umeapply CRDB unaogapa ushindani ubaki Peke yako interview utasubiri miaka 20
 
Crdb ni Benki ya WACHAGA na wakristo..kma una hvo vgezo viwili na sura yako inalipa jiongezeeeee...otherwise its a dream unlikely to be true!
 
Apply ufanye kazi ya kujitolea bila malipo kwa kuanzia,badae mambo yatanyooka,..ni kweli ndoto zipo ila pia kuna hali halisi, Usikate tamaa endelea kutafuta
 
una GPA ya ngapi nikufanyie mpango hapo CRDB pia unapenda ufanyie kwenye region ipi kwa hapa Tanzania. Ukinijibu hayo maswali mawili nitakupa mengine mawili ili niweze kukusaidia
Nyiie ndo matapeli humu JF Kuna mmoja anaitwa Katerero kawalia mpunga watu wanataka kwenda kwa Mzee Trump hawanahamu
 
Back
Top Bottom