Au unataka tukwambie unalogwa kuna mtu anachezea nyota yako?
Maana waafrica kila kitu lazima mkirelate na wizard
Bahati mbaya au nzuri kwa anaeamini na hata asieamini masuala ya kiroho, bado atapitia tu michakato ya kiroho pale mambo yake yanapokwama.
Watu tumepoteza attachment ya mawasiliano baina ya Mwili, Nafsi na Roho ndiomaana tunashindwa kutatua masuala ya kimaisha ijapokuwa UTU wetu wa ndani unatupa ujumbe mapema.
Watu wasichokijua ni kuwa nafsi na roho Pia zina hisia na hisia zake huwa kweli hazihusu mambo ya kubashiri wala kukisia bali uhalisia wa jambo, UTU wa mtu unapoona changamoto ktk mwili wako hukupa alert ya kipi kitatokea, kilitokea ama kinachotokea na suluhisho la maamuzi hubaki ktk fikra zako za kimwili.
Machale/re yanayowapata watu kuhusu jambo fulani na likatokea kweli hizo ni hisia za Nafsi the same thing kwa ndoto wanazoota watu na zinatimia kweli, bahati mbaya ni kuwa hisia za Nafsi na Roho haziji kwa mfanano wa matukio/taswira za mambo ya mwilini bali kupitia mifano ambayo kwa wataalamu wa sayansi ya kiroho wanajua kusoma na kutambua maana ya alama hizi za ndoto.
Mtu anaota yuko shule na baadhi ya watu aliosoma nao kimaana ya kimwili haihusu shule na nafsi/roho kamwe haiwezi kukupa mfano/alama ya jambo ambalo hujawai kuliona/kulisikia bali mfanano wa jambo hilo na vitu ambavyo fikra/akili zako za mwili zinaweza kulitumia kupata maana.
Shule, marafiki, masomo, mitihani, walimu, kalamu, makaratasi, wanafunzi, adhabu, hisia za uoga, mbio, ugomvi, mapambano, majengo, makazi, au hata taswira za watu/vitu ktk ndoto zako hazina maana yake direct na vitu hivyo ktk fikra za mwili bali mfanano navyo.
Mtu anaota yuko ktk shule ya zamani (jambo la kale/chanzo cha tatizo), katika shule ya msingi(chanzo cha tatizo), akapata taarifa za ujio wa mtihani(jambo analohangaika nalo sasa) kuwa mtihani huo utafanyika ijapokuwa hajajiandaa(hauna suluhu/hujawekeza nguvu za kutatua jambo lako ktk msingi wake, iwe ndoa, masuala ya kifamilia, uchumi n.k.
Au kuna wale wanaota wapo ktk makazi yao ya zamani/nyumba ya zamani walioishi utotoni ghafla hupatwa na giza/hisia za uoga na upinzani mkali tafsiri yake ya mfanano na maisha yako ya sasa asili yake ilianza ktk....
Naishia hapa maana hata Mimi bado naendelea kuyasoma mambo ya kiroho maana ni mapana na hakuna gwiji wa mambo haya.
Nalog off.