Ndoto inayojirudia mara kwa mara

Ndoto inayojirudia mara kwa mara

Wasi wasi upo. Mara nyingi plan zangu zimekuwa hazikubali, na hii inatokana na most of my personal project kuishia njiani ns zinakufa
Labda kuna kitu kikubwa zaidi ya hayo.. Jaribu kutafuta nini inaleta hiyo hofu. Itachukua muda na uvumilivu wa hali ya juu. Ila Nakuhakikishia itakuwa kutoka utotoni kabisa. Nini ulikosa, au nini kilitokea.
 
Labda kuna kitu kikubwa zaidi ya hayo.. Jaribu kutafuta nini inaleta hiyo hofu. Itachukua muda na uvumilivu wa hali ya juu. Ila Nakuhakikishia itakuwa kutoka utotoni kabisa. Nini ulikosa, au nini kilitokea.
Sina kumbukumbu yoyote nitajaribu kuuliza kwa mzazi.
 
Ndoto za hivyo zinaboa sana, imagine unapitia ndoto moja hata mara 10 ndani ya mwezi mmoja.

Na asikudanganye mtu kuwa ndoto hazina maana, si kweli, na hizi zinazojirudia bila ya wewe kuweka effort ya fikra kaze ktk jambo lililopelekea upate ndoto hiyo, aina hii ya ndoto huwa na maana kubwa ktk maisha yako.

Achana na watu wasioamini mambo ya kiroho, tafuta majibu ya mambo yanayokurudisha nyuma, yanayokukwamisha, i mean mizizi ya matatizo yanayorudisha maendeleo yako nyuma.

Kuna ndoto nyingi zisizo na maana lkn hii huwatokea watu wengi na huenda kila mtu huipitia hii iwe anaamini mambo ya kiroho au haamini bado atapitia tu pale baadhi ya mambo yanapokuwa ktk kikwazo, Nafsi yako inakupa ujumbe wa mambo ambayo unapaswa kuyashughulikia ktk level ya Msingi/mzizi/chanzo/sababu/mwanzo wake.

Wapo wanao ota wakiwa shule za msingi wapo wanao ota shule za sekondari pia chuo, na hili la shule ya msingi uhusu sana maandalizi ya mitihani, somo ambalo lilikuwa changamoto ktk juhudi zako za kimasomo, ikikukumbusha kuwa tatizo ktk maisha yako lipo ktk msingi/chanzo cha jambo ulilolianzisha/unalopitia iwe kiuchumi, au hata kimahusiano.

Tafuta mzizi wa chanzo cha jambo hilo kukwama na utaona hizi ndoto zikipungua kama utalitatua au utaendelea kuota ndoto hizo ktk level nyingine ya kielimu kukujulisha kuwa unapaswa kushughulikia ktk level za juu zaidi yaani kutoka ktk mzizi mpaka shina na matawi, yaani jambo lipo ktk level ambazo si hatari sana.

Kuna ndoto za aina nyingi zisizo na maana na zenye maana, bahati mbaya tunaishi ktk jamii iliyopumbazwa kuhusu masuala ya kiroho kwa kuyahusianisha na dini/imani za hovyo ndiomaana tunashindwa kutatua mambo madogo ambayo bado tunapata viashiria kupitia Roho, Nafsi zetu.
 
Habari,

Kwanza
pole sana.

Ndoto hua ni ujumbe kutoka kwenye subconcious mind kuja kwenye your consious mind.

Unapoota kua umerudi darasani au shuleni, tafsiri yake ya haraka ni kua kuna kitu au patterns unazirudia na bado somo lake hujajifunza, hivyo unakua ni kama unajiandaa kuzivuka ila hauzivuki. Sasa katika maisha yako ya mchana ya kila siku kuna mambo unafanya yanakukwamisha au kukufanya uwe katika "stagnation", unatakiwq ujiangalie vizuri vitu unavyojua vinakukwamisha na uvivuke.

unapoota umerudi darasani maana yake unafanya jambo ambalo unatakiwa uwe umeshapata somo ila bado unalirudia sababu unatarajia majibu tofauti ilihali unajua fika mwisho wake ni upi, aidha inaweza kua kuna tabia hutaki kuziacha vile vile.

Maisha ya kila siku ni experiences zako wewe binafsi, hivyo kuna experience ambazo ukipitia hutakiwi kuzirudia tena, ila ukirudia ndio inatokea kama hivyo.

Pia, Katika hizo ndoto unahisi nini? kama unahisi uoga basi katika maisha ya kila siku kuna mambo unaweza kua unayaogopa pia na haujafikia ujasiri wa kuyavuka hvyo unajiona kua haupo tayari na kama unajiandaa kufanya mtihani.

Ndoto ni ujumbe wako kutoka nafsi yako ya ndani "higher self" kuja katika "lower self - huyu ww unaesoma hapa". Na kila unachoona kwenye ndoto ni reflection yako, hata ukimuona mtu mwingine ana reflect upande wako tu na sio mtu wa nje.

Uwe na wakati mwema, na jifanyie tathmini katika hali ya utulivu, majibu unayo ndani yako.

Alamsiki.
 
ndoto (sio zote) huelezea hali yako kiroho. Kuwa darasani ni ishara ya kupata maarifa mapya.

kuna ndoto ambazo ni lucid huwa ni nzuri sana hizi. kwamba unaota na unakuwa unajua kuwa unaota na unakuwa na uwezo wa ku-control events ila huna uwezo wa kuikata, hadi inapokatika yemyewe.
Ukiwa na awareness unaweza kuikata ndoto au hata kui pause, ukaamka kwenda chooni na ukirudi ukaendelea ulipokua umeishia, inategemea na ukubwa wa ufahamu wako.

Kurudi darasani sio kupata maarifa mapya bali unarudia kujifunza jambo ambalo unatakiwa uwe umeshajifunza ila hutaki kujifunza na kulivuka.

Maisha ya kila siku ya mwanadamu ni kujifunza kila siku na kutengeneza experience mpya kila siku.

ukiona umerudi darasani jitathmini, ukiendelea kupuuzia ulimwengu utaongea kwa vitendo mfano kupata madhara au changamoto yoyote katika maisha au shughuli za kila siku.
 
Au unataka tukwambie unalogwa kuna mtu anachezea nyota yako?

Maana waafrica kila kitu lazima mkirelate na wizard
Bahati mbaya au nzuri kwa anaeamini na hata asieamini masuala ya kiroho, bado atapitia tu michakato ya kiroho pale mambo yake yanapokwama.

Watu tumepoteza attachment ya mawasiliano baina ya Mwili, Nafsi na Roho ndiomaana tunashindwa kutatua masuala ya kimaisha ijapokuwa UTU wetu wa ndani unatupa ujumbe mapema.

Watu wasichokijua ni kuwa nafsi na roho Pia zina hisia na hisia zake huwa kweli hazihusu mambo ya kubashiri wala kukisia bali uhalisia wa jambo, UTU wa mtu unapoona changamoto ktk mwili wako hukupa alert ya kipi kitatokea, kilitokea ama kinachotokea na suluhisho la maamuzi hubaki ktk fikra zako za kimwili.

Machale/re yanayowapata watu kuhusu jambo fulani na likatokea kweli hizo ni hisia za Nafsi the same thing kwa ndoto wanazoota watu na zinatimia kweli, bahati mbaya ni kuwa hisia za Nafsi na Roho haziji kwa mfanano wa matukio/taswira za mambo ya mwilini bali kupitia mifano ambayo kwa wataalamu wa sayansi ya kiroho wanajua kusoma na kutambua maana ya alama hizi za ndoto.

Mtu anaota yuko shule na baadhi ya watu aliosoma nao kimaana ya kimwili haihusu shule na nafsi/roho kamwe haiwezi kukupa mfano/alama ya jambo ambalo hujawai kuliona/kulisikia bali mfanano wa jambo hilo na vitu ambavyo fikra/akili zako za mwili zinaweza kulitumia kupata maana.

Shule, marafiki, masomo, mitihani, walimu, kalamu, makaratasi, wanafunzi, adhabu, hisia za uoga, mbio, ugomvi, mapambano, majengo, makazi, au hata taswira za watu/vitu ktk ndoto zako hazina maana yake direct na vitu hivyo ktk fikra za mwili bali mfanano navyo.

Mtu anaota yuko ktk shule ya zamani (jambo la kale/chanzo cha tatizo), katika shule ya msingi(chanzo cha tatizo), akapata taarifa za ujio wa mtihani(jambo analohangaika nalo sasa) kuwa mtihani huo utafanyika ijapokuwa hajajiandaa(hauna suluhu/hujawekeza nguvu za kutatua jambo lako ktk msingi wake, iwe ndoa, masuala ya kifamilia, uchumi n.k.

Au kuna wale wanaota wapo ktk makazi yao ya zamani/nyumba ya zamani walioishi utotoni ghafla hupatwa na giza/hisia za uoga na upinzani mkali tafsiri yake ya mfanano na maisha yako ya sasa asili yake ilianza ktk....

Naishia hapa maana hata Mimi bado naendelea kuyasoma mambo ya kiroho maana ni mapana na hakuna gwiji wa mambo haya.

Nalog off.
 
Ukiwa na awareness unaweza kuikata ndoto au hata kui pause, ukaamka kwenda chooni na ukirudi ukaendelea ulipokua umeishia, inategemea na ukubwa wa ufahamu wako.

Kurudi darasani sio kupata maarifa mapya bali unarudia kujifunza jambo ambalo unatakiwa uwe umeshajifunza ila hutaki kujifunza na kulivuka.

Maisha ya kila siku ya mwanadamu ni kujifunza kila siku na kutengeneza experience mpya kila siku.

ukiona umerudi darasani jitathmini, ukiendelea kupuuzia ulimwengu utaongea kwa vitendo mfano kupata madhara au changamoto yoyote katika maisha au shughuli za kila siku.
Hili la kupause ndoto nadhani sometimes huwa tunalifanya bila ya kujitambua this week nimepitia situation kama hii
 
Ukiwa na awareness unaweza kuikata ndoto au hata kui pause, ukaamka kwenda chooni na ukirudi ukaendelea ulipokua umeishia, inategemea na ukubwa wa ufahamu wako.

Kurudi darasani sio kupata maarifa mapya bali unarudia kujifunza jambo ambalo unatakiwa uwe umeshajifunza ila hutaki kujifunza na kulivuka.

Maisha ya kila siku ya mwanadamu ni kujifunza kila siku na kutengeneza experience mpya kila siku.

ukiona umerudi darasani jitathmini, ukiendelea kupuuzia ulimwengu utaongea kwa vitendo mfano kupata madhara au changamoto yoyote katika maisha au shughuli za kila siku.
sawa lakini fikiria, wewe ni std seven au form four leaver ila unaota uko darasani/lecture room university, unaonaje hapo
 
Back
Top Bottom