Masalia Mpya
Member
- Mar 24, 2023
- 53
- 63
Habari zenu kwa ujumla
Nimekuwa nikiota ndoto zinazofanana fanana.
Iko hivi mimi naishi Dodoma, ila ni mwenyeji wa Lindi. Nimezaliwa huko na kusoma huko mpaka secondary. Chuo nikatoka kwenda mikoa mimgine. Kuanzia hapo nikawa narudi Lindi kama mgeni. Miaka 5 nyuma tulihamisha makazi na kuhamia Mtwara, yaani familia nzima walihama kwa hiyo Lindi tunakwenda kama wageni.
Sasa hivi nina familia yangu huku Dodoma naendelea na maisha yangu, hata nikienda kwetu Mtwara pia naenda kama mgeni siku chache naondoka.
Ndoto zinazonisumbua ni hizi, yaani kwa week mara 2 au 3 naota niko ambako tulishahama, maisha yanaendelea hapo Lindi. Kama ni misiba/ sherehe/ maisha ya familia yetu/ mtaani naota niko Lindi niko na majirani wa Lindi, ndugu walioko Lindi yaani kama vile hatujahama.
Sijawahi kuota niko Mtwara tuliko hamia, hata nikiota wazazi wangu au ndugu zangu naota tuko nyumbani Lindi.
Nashindwa kuelewa, mbona sioti nikiwa Dodoma au Mtwara? Mbona huku nina majirani na hata ndugu wengine Dodoma na Mtwara ila nawaota walioko Lindi? Kwa kweli zimenichosha.
Naombeni ushauri
Nimekuwa nikiota ndoto zinazofanana fanana.
Iko hivi mimi naishi Dodoma, ila ni mwenyeji wa Lindi. Nimezaliwa huko na kusoma huko mpaka secondary. Chuo nikatoka kwenda mikoa mimgine. Kuanzia hapo nikawa narudi Lindi kama mgeni. Miaka 5 nyuma tulihamisha makazi na kuhamia Mtwara, yaani familia nzima walihama kwa hiyo Lindi tunakwenda kama wageni.
Sasa hivi nina familia yangu huku Dodoma naendelea na maisha yangu, hata nikienda kwetu Mtwara pia naenda kama mgeni siku chache naondoka.
Ndoto zinazonisumbua ni hizi, yaani kwa week mara 2 au 3 naota niko ambako tulishahama, maisha yanaendelea hapo Lindi. Kama ni misiba/ sherehe/ maisha ya familia yetu/ mtaani naota niko Lindi niko na majirani wa Lindi, ndugu walioko Lindi yaani kama vile hatujahama.
Sijawahi kuota niko Mtwara tuliko hamia, hata nikiota wazazi wangu au ndugu zangu naota tuko nyumbani Lindi.
Nashindwa kuelewa, mbona sioti nikiwa Dodoma au Mtwara? Mbona huku nina majirani na hata ndugu wengine Dodoma na Mtwara ila nawaota walioko Lindi? Kwa kweli zimenichosha.
Naombeni ushauri