Wataalamu wa kutafsiri ndoto msaada kidogo

Wataalamu wa kutafsiri ndoto msaada kidogo

Joined
Nov 30, 2022
Posts
27
Reaction score
18
Habari za kazi wakuu,

Aisee kuna ndoto zimekuwa zikinirudia rudia, ninataka pata tafsiri zake kama kuna mwenye atakua na ujuzi huo.

Nimekua nikiota sana matukio ya nyuma, yaani ndoto zangu nyingi zinahusu watu wote ambao nilkua nao kipindi niko shule ya msingi au mwanzoni wa sekondari hata kama walihamaga mda mrefu.

Naomba kuelewa maana yake sababu imekua vigumu kwa mimi kuota current issues kama watu wanaonizunguka sasa hivi n.k.

Wanasemaga ndoto ni vitu ulivyovifikiria sana mchana lakini unakuta mchana sijawaza kabisa hao watu lakini nikiota tu hao hapo.

Wengi wao ni familia yangu, majirani, tena mbaya zaidi wengine wamefariki au wameugua kias cha kwamba nina muda mrefu hatujawahi share nao experience pamoja.

Naomba kuwasilisha wakuu.
 
Kuna kurudi nyuma ki uchumi, either mzizi wa changamoto zako unazopitia upo kule
 
Kama ndoto zako zinahusu matukio ya nyuma ama mambo ya shule ilhali we ushamaliza kitambo ni ishara ya kua unarudi nyuma kumaisha ama unaenda kukutana na magumu punde.
 
Mafanikio yapo karibu hapo toa sadaka sana sali sana utaleta mrejesho hapa
 
Kwanini unataka kutafuta miujiza toka kwa watu wakati hata wewe waweza kufanya miujiza hiyo . Ndoto unazoota zinakuhusu wewe na wewe ndio utakayeweza ku solve hiyo riddle na si mtu mwingine... Hapa sanasana utapewa assumption za kila mmoja katika ndoto yako
 
Mie kuna ndoto nlikuwa naota mara kwa mara sana ila siku hizi sioti and naumia sana kwa nn siioti
Jambo nlilokuwa nalifanya haliwezekani kufanywa na binadamu.

Huwa naota nafukuzwa na viumbe sikumbuki kama huwa ni watu ama vitu gani ila huwa naota nafukuzwa.
Sasa huwa nafika sehem nakuwa kama.naendesha baiskeli isiyokuwepo yaan napedal hewani tu halafu nikipedal naanza kupaa hewani juu kufikia kama mita 30 hivi then naanza kuelekea mbele na mikono huwa naitandaza kama mabawa ya tai ndo huwa naitumia kujibalanze nisi overturn na hawa wanaonifukuza wanashindwa kunipata nakuwa ndo nimewaacha hivo.

Kuna kupindi huwa napita mazingira hatari kwwnye nguzo za umeme sasa kubalance nisigonge waya za umeme huwa napatashida sana na uoga mkubwa nahicho huwa najikuta naamka kutoka usingizini.

Nikiamka ile hali huwa inaendelea kuwepo kwamba naweza kupaa na huwa kuna furaha isiyo kifani. Huwa inadumu kama dakika 5 hadi 10 ndo narudi katika hali ya kawaida. Na huwa napata huzuni sana.
 
Mie kuna ndoto nlikuwa naota mara kwa mara sana ila siku hizi sioti and naumia sana kwa nn siioti
Jambo nlilokuwa nalifanya haliwezekani kufanywa na binadamu...
Hio sio ndoto mkuu, hizo hutokea ukiwa unakua kila mtu amepitia hio Hali na mpaka Sasa wanapitia ila ni kwa watoto tu
 
yaani ndoto zangu nyingi zinahusu watu wote ambao nilkua nao kipindi niko shule ya msingi au mwanzoni wa sekondari hata kama walihamaga mda mrefu....
Hauoti upo na ndugu zako na marafiki zako waliokufa miaka mingi?
 
Huwa naota nafukuzwa na viumbe sikumbuki kama huwa ni watu ama vitu gani ila huwa naota nafukuzwa.
Kuna kitu umeacha kufanya mkuu, ndio maana hauoti usiniulize ni kipi sababu unakijua

Ipo hivi unafuzwa aidha peke ako au na wenzako na watu au wadudu wasio na umbo maalum na unapambana kijiokoa aidha kwa kujificha au kupambana nao ana kwa ana

Sasa usiniulize nimejuaje
 
Sasa huwa nafika sehem nakuwa kama.naendesha baiskeli isiyokuwepo yaan napedal hewani tu halafu nikipedal naanza kupaa hewani juu kufikia kama mita 30 hivi then naanza kuelekea mbele na mikono huwa naitandaza kama mabawa ya tai ndo huwa naitumia kujibalanze nisi overturn na hawa wanaonifukuza wanashindwa kunipata nakuwa ndo nimewaacha hivo.
Hii ya watoto hizi ni ndoto za watoto hazina maana yoyote
 
Kuna kupindi huwa napita mazingira hatari kwwnye nguzo za umeme sasa kubalance nisigonge waya za umeme huwa napatashida sana na uoga mkubwa nahicho huwa najikuta naamka kutoka usingizini.
Hii sio ndoto ni mazingira ya kazi unayofanya
 
Nikiamka ile hali huwa inaendelea kuwepo kwamba naweza kupaa na huwa kuna furaha isiyo kifani. Huwa inadumu kama dakika 5 hadi 10 ndo narudi katika hali ya kawaida. Na huwa napata huzuni sana
Huo ni utoto, ukikua utakua huoti tena ndoto km hizo
 
Back
Top Bottom