Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
NDOA YANGU (01)
‘Chozi langu litalipwa’
By; KING T CONTROL
Nilipokuwa mdogo kipindi bado nasoma, nakumbuka maneno aliyokuwa anapenda kunambia marehemu baba. Maneno ambayo awali niliyachukulia mepesi sana kwa kuyanukuu pasipo kuujua uzito uliokuwa ndani yake. Endapo ningeyabeba na kumakinika nayo…. Huenda hadithi hii isingekuwepo kwenye maisha yangu.
Baba alisema....
"Utapokuwa mkubwa usije kuoa mwanamke eti kwa sababu unampenda naye anakupenda…! hapana. Bali oa mwanamke ambaye unamuhitaji na ukahakikisha naye anakuhitaji. Hapo mtaishi vizuri na kujenga familia bora. Kua ukikumbuka haya mwanangu ili usije kukosea kuoa kwani utakuwa umeyakosea kabisa maisha."
Maneno haya ya baba yaliishia kuwa ya baba akilini mwangu wala sijawahi kufikiria kama ipo siku yanaweza kuzitesa hisia zangu na kuuchoma moyo wangu kila nikumbukapo puuzio langu.
Hakika hii ni hadithi ya kweli katika maisha yangu. Hadithi ya NDOA YANGU...... Ingawa yanaweza kuwa ni makosa yangu lakini sikustahili malipo haya. Maumivu makali ya moyo yalizishawishi akili zangu zilipe kisasi lakini imani yangu ndiyo iliyonizua ikinikumbusha kuwa yupo mkuu baba mwenye kutoa hukumu siku ya malipo. Siku ambayo sote tutakuwa wadogo zaidi ya chembe ya punje ya haradali. Kama tunaamini kweli Mungu yupo na ndiye mwenye kuhukumu basi naamini kwa ubaya niliotendwa…….. chozi langu litalipwa.
Karibu kwenye mkasa wangu naamini nawe utajifunza mengi.
*******
Naitwa Onesmo, ni mtoto wa mwisho na pekee wa kiume kati ya watoto watano kwenye uzawa wetu. Nilipokuwa mkubwa baada ya kumaliza kidato cha nne baba alifariki kwa ajali ya gari na kutuachia ukiwa. Maisha yalibadilika siku baada ya siku na kuwa magumu. Dada yangu mmoja tu alibahatika kuolewa huku wengine wakizalishwa wakiwa nyumbani. Hali hii iliniumiza sana. Ndoto yangu ilikuwa kuona siku moja tunaishi maisha mazuri na ya fahari. Mama aliniusia mara nyingi sana kuwa nina mzigo mkubwa kwenye familia yetu, hivyo yanipasa niwe na upeo mkubwa kuweza kuwaongoza dada zangu nikiwa ndiye kaka yao wa pekee.
Hali hii ilinifanya niishi kwa kujituma sana kwenye kazi ingawa nilifeli kuendelea na masomo ya elimu ya juu. Siku zote niliamini kufeli shule sio kufeli maisha.
Nilijituma na kujichanganya kwenye kazi mbalimbali. Sikuchagua kazi ilimradi tu iwe ya halali isiyovunja maadili na utu. Na hapo ndipo nilipojijengea marafiki wengi wanaopenda kujishughulisha. Ni kweli kabisa ukiwa mvivu basi utatengeneza marafiki wengi wavivu. Ukiwa tapeli utawapata marafiki wengi matapeli. Halikadharika ukiwa mwizi vivyohivyo kama ukiwa mpenda kukaa vijiweni basi rafikizo watakuwa wa vijiweni tu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu kupenda kujituma na kufanya kazi ilinijengea kutengeneza marafiki wa tabia zangu. Na ndipo baada ya miaka kadhaa nilijiunga na kampuni moja ya umeme kama kibarua kipindi cha kujenga miradi ya umeme vijijini iliyosimamiwa na REA. Jitihada zangu kwenye kazi ngumu za umeme zilinifanikishia kuujua ujuzi wa kazi yenyewe mara baada ya kudumu kwenye miradi zaidi ya miwili mwishowe nikawa najua kila kitu kuhusu ufundi wa kujenga umeme mkubwa. Tabia yangu ya ucheshi na heshima ikawa kivutio cha kupendwa na kila mtu. Na ndipo viongozi wengi wa ‘site’ waliponizoea na kuniita kwenye miradi mbalimbali hadi pale nilipoajiriwa kwenye kampuni moja iliyoitwa Intercity Builders ltd. Sikuamini punde nilipoletewa barua ya kuajiliwa na kampuni hiyo kama fundi daraja la pili tulipomaliza mradi wa Dodoma.
Taratibu hadithi ya maisha yangu ikaanza kuwa nzuri mara baada ya kufika ofisini na kupewa maelekezo yote. Niliiona nyota njema ya ndoto yangu ikiangaza mbele yangu. Mkataba wangu ulikuwa wa miaka miwili sambamba na mshahara wa laki saba. Haikuwa pesa nyingi kwa wenye nazo, lakini kwa mwenzangu na mimi ilikuwa ni zaidi ya tunu ya ndoto. Kiwango cha mshahara ambao sijategemea kama nitakipata nikiwa na umri ule. Miaka ishirini na nne tu! Hakika ilikuwa furaha si kwangu tu bali kwa familia nzima.
“Mwanangu nakupa baraka zote, kafanye kazi utukumbuke baba kuwa makini sana na matumizi ya pesa unaona hali yetu baba. Nakuombea kila la heri baba uende salama.”
Hayo yalikuwa maneno ya mama siku moja kabla ya safari. Usiku ambao tulikesha kuzungumza mambo mengi sana ya kimaisha. Ilikuwa ndio ajira yangu rasmi ya kwanza na kazi ilikuwa jijini Mbeya.
“Usijali mama, nawaahidi sasa ugumu wa maisha tuliyopitia unaenda kuwa kikomo.”
Nilizingatia moyoni na kumuahidi mama huku nikimtoa hofu.
Alfajiri saa kumi na moja mama na dadaangu walinisindikiza hadi Ubungo nilipokutana na mafundi wenzangu wawili tayari kuelekea kazini mkoani Mbeya. Tuliagana na kujumuika na wenzangu huku moyoni nikiwa mwingi wa matumaini. Nilijua fika sitoweza ufanyia mchezo mshahara wa laki saba kwa mwezi. Kila nilipofumba macho niliziona picha za utajiri wangu baada ya miaka miwili ya mkataba. Daaah! Laiti ningelijua juu ya safari ile ndio itakuwa chanzo cha matukio ya kuumiza maisha yangu? Basi nisingelithubutu kukubali kwenda huko wala kusaini mkataba na kampuni ile. Hakika wao ndio walionifanya nipajua Mbeya kwa mara ya kwanza na kunikutanisha na hasidi wa maisha yangu…………
Oooooh! ! NDOA YANGU
Hakika Chozi langu Litalipwa
‘Chozi langu litalipwa’
By; KING T CONTROL
Nilipokuwa mdogo kipindi bado nasoma, nakumbuka maneno aliyokuwa anapenda kunambia marehemu baba. Maneno ambayo awali niliyachukulia mepesi sana kwa kuyanukuu pasipo kuujua uzito uliokuwa ndani yake. Endapo ningeyabeba na kumakinika nayo…. Huenda hadithi hii isingekuwepo kwenye maisha yangu.
Baba alisema....
"Utapokuwa mkubwa usije kuoa mwanamke eti kwa sababu unampenda naye anakupenda…! hapana. Bali oa mwanamke ambaye unamuhitaji na ukahakikisha naye anakuhitaji. Hapo mtaishi vizuri na kujenga familia bora. Kua ukikumbuka haya mwanangu ili usije kukosea kuoa kwani utakuwa umeyakosea kabisa maisha."
Maneno haya ya baba yaliishia kuwa ya baba akilini mwangu wala sijawahi kufikiria kama ipo siku yanaweza kuzitesa hisia zangu na kuuchoma moyo wangu kila nikumbukapo puuzio langu.
Hakika hii ni hadithi ya kweli katika maisha yangu. Hadithi ya NDOA YANGU...... Ingawa yanaweza kuwa ni makosa yangu lakini sikustahili malipo haya. Maumivu makali ya moyo yalizishawishi akili zangu zilipe kisasi lakini imani yangu ndiyo iliyonizua ikinikumbusha kuwa yupo mkuu baba mwenye kutoa hukumu siku ya malipo. Siku ambayo sote tutakuwa wadogo zaidi ya chembe ya punje ya haradali. Kama tunaamini kweli Mungu yupo na ndiye mwenye kuhukumu basi naamini kwa ubaya niliotendwa…….. chozi langu litalipwa.
Karibu kwenye mkasa wangu naamini nawe utajifunza mengi.
*******
Naitwa Onesmo, ni mtoto wa mwisho na pekee wa kiume kati ya watoto watano kwenye uzawa wetu. Nilipokuwa mkubwa baada ya kumaliza kidato cha nne baba alifariki kwa ajali ya gari na kutuachia ukiwa. Maisha yalibadilika siku baada ya siku na kuwa magumu. Dada yangu mmoja tu alibahatika kuolewa huku wengine wakizalishwa wakiwa nyumbani. Hali hii iliniumiza sana. Ndoto yangu ilikuwa kuona siku moja tunaishi maisha mazuri na ya fahari. Mama aliniusia mara nyingi sana kuwa nina mzigo mkubwa kwenye familia yetu, hivyo yanipasa niwe na upeo mkubwa kuweza kuwaongoza dada zangu nikiwa ndiye kaka yao wa pekee.
Hali hii ilinifanya niishi kwa kujituma sana kwenye kazi ingawa nilifeli kuendelea na masomo ya elimu ya juu. Siku zote niliamini kufeli shule sio kufeli maisha.
Nilijituma na kujichanganya kwenye kazi mbalimbali. Sikuchagua kazi ilimradi tu iwe ya halali isiyovunja maadili na utu. Na hapo ndipo nilipojijengea marafiki wengi wanaopenda kujishughulisha. Ni kweli kabisa ukiwa mvivu basi utatengeneza marafiki wengi wavivu. Ukiwa tapeli utawapata marafiki wengi matapeli. Halikadharika ukiwa mwizi vivyohivyo kama ukiwa mpenda kukaa vijiweni basi rafikizo watakuwa wa vijiweni tu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwangu kupenda kujituma na kufanya kazi ilinijengea kutengeneza marafiki wa tabia zangu. Na ndipo baada ya miaka kadhaa nilijiunga na kampuni moja ya umeme kama kibarua kipindi cha kujenga miradi ya umeme vijijini iliyosimamiwa na REA. Jitihada zangu kwenye kazi ngumu za umeme zilinifanikishia kuujua ujuzi wa kazi yenyewe mara baada ya kudumu kwenye miradi zaidi ya miwili mwishowe nikawa najua kila kitu kuhusu ufundi wa kujenga umeme mkubwa. Tabia yangu ya ucheshi na heshima ikawa kivutio cha kupendwa na kila mtu. Na ndipo viongozi wengi wa ‘site’ waliponizoea na kuniita kwenye miradi mbalimbali hadi pale nilipoajiriwa kwenye kampuni moja iliyoitwa Intercity Builders ltd. Sikuamini punde nilipoletewa barua ya kuajiliwa na kampuni hiyo kama fundi daraja la pili tulipomaliza mradi wa Dodoma.
Taratibu hadithi ya maisha yangu ikaanza kuwa nzuri mara baada ya kufika ofisini na kupewa maelekezo yote. Niliiona nyota njema ya ndoto yangu ikiangaza mbele yangu. Mkataba wangu ulikuwa wa miaka miwili sambamba na mshahara wa laki saba. Haikuwa pesa nyingi kwa wenye nazo, lakini kwa mwenzangu na mimi ilikuwa ni zaidi ya tunu ya ndoto. Kiwango cha mshahara ambao sijategemea kama nitakipata nikiwa na umri ule. Miaka ishirini na nne tu! Hakika ilikuwa furaha si kwangu tu bali kwa familia nzima.
“Mwanangu nakupa baraka zote, kafanye kazi utukumbuke baba kuwa makini sana na matumizi ya pesa unaona hali yetu baba. Nakuombea kila la heri baba uende salama.”
Hayo yalikuwa maneno ya mama siku moja kabla ya safari. Usiku ambao tulikesha kuzungumza mambo mengi sana ya kimaisha. Ilikuwa ndio ajira yangu rasmi ya kwanza na kazi ilikuwa jijini Mbeya.
“Usijali mama, nawaahidi sasa ugumu wa maisha tuliyopitia unaenda kuwa kikomo.”
Nilizingatia moyoni na kumuahidi mama huku nikimtoa hofu.
Alfajiri saa kumi na moja mama na dadaangu walinisindikiza hadi Ubungo nilipokutana na mafundi wenzangu wawili tayari kuelekea kazini mkoani Mbeya. Tuliagana na kujumuika na wenzangu huku moyoni nikiwa mwingi wa matumaini. Nilijua fika sitoweza ufanyia mchezo mshahara wa laki saba kwa mwezi. Kila nilipofumba macho niliziona picha za utajiri wangu baada ya miaka miwili ya mkataba. Daaah! Laiti ningelijua juu ya safari ile ndio itakuwa chanzo cha matukio ya kuumiza maisha yangu? Basi nisingelithubutu kukubali kwenda huko wala kusaini mkataba na kampuni ile. Hakika wao ndio walionifanya nipajua Mbeya kwa mara ya kwanza na kunikutanisha na hasidi wa maisha yangu…………
Oooooh! ! NDOA YANGU
Hakika Chozi langu Litalipwa