Ndoa yangu inateketea

Cheguevara Jr

Senior Member
Feb 20, 2014
134
121
Habari wana JF wote kwa ujumla, bila ya kupoteza muda naomba kuja kwenye mada husika. Mimi ni kijana wa miaka 35,ndoa yanagu mpaka sasa inamiaka 5 tuu. Katika kipindi chote hichi tumeishi kwa furaha na upendo mkubwa tumebahatika kupata watoto 2.

Mke wangu ni mtumishi chuo kikuu(mwalimu)na mimi ni unga unga mwana pangu pakavu baada ya kampuni fulani ya mawasiliano niliyokua nafanya kazi kufungiwa na serikali kwa madai ya kukwepa kulipa na kuhujumu uchumi hivyo kesi bado iko mahakamani lakini sijawahi kukosa rizik japo kipato changu ni kidogo ila upendo na furaha viliendelea kushamiri.

KUANZA TATIZO
Mambo yalianza kua mabaya ktk ndoa yangu pale tuu mke wang alivyohamishwa kikazi na kuja hapa Dar ktk chuo kikuu fulani mwaka huu mwez 3 hivyo mimi niliendelea kubaki mkoni kwa lengo la kujipanga ili nihamie dar ili niwe karibu na familia yangu.

Ifahamike kua uhamisho wake haukua wa malipo kutokana na yy ndo aliomba kuhamishwa hivyo alipofika hapa Dar alifikia kwao maana yeye ni mzaliwa wa hapa dar.

Baada ya miezi 2 kupita mimi pia nikatoka mkoani na kuja hapa Dar,ila nilifikia nyumban kwetu kwa wazazi wangu (Mkuranga)
Harakaki za kutafuta nyumba zikaanza,kwa bahati mbaya wakati sijalipia nyumba nikafiwa na mzazi wangu(baba) chakushangaza mke wangu hakuweza kufika msibani kwa madai ya kukosa ruhusa kazini.

Sikua na neno maana bado nilikua kwenye majonzi,baada ya msiba kumalizika nilinza kujisikia homa kali na kulazwa hospitali,baada ya vipimo niligundulika ni Covid 19,

Mungu alisaidia nikaruhusiwa na kuendelea na matibabu nyumban. Wakati naendelea na matibabu mawasiliano na mke wangu yalikua ya tabu sana,simu za zilikua hazipaikan kwa madai mtoto wetu mdogo ameharibu simu yake hivyo ilinibidi niwe namtafuta mama mkwe kuongea na mke wangu

Hali ya kimawasiliano ilizidi kua mbaya zaid kadri siku zinavyozidi kusonga mbele,akawa hanitafuti,mpaka mimi nimtafute yeye, upendo wake kwangu ulikua umepungua sana kwangu. Maana hata kunijulia hali imekua vigumu kwake. Kibaya zaid alinza kufuta account namba yake ya wasapu na kuwa online kupitia Facebook nilivyomuuliza mbona nakuona online ushanunua simu nyingine?alinijibu kua ni ya ndugu yake wanaishi karibu pia namjua huyo mtu.

Nilimuomba namba ya simu anayoitumia ya huyo ndugu yake akanipa. Chaajabu sasa nikipiga ile namba anapokea muhusika wa ile simu na ananimbia yy yuko mbali kidogo na mke wangu.

Hii hali ilinishangaza sana kwan mda ambao nachat na mke wangu Facebook ndo mda huo nimepiga simu baada ya yy kunipa hiyo namba na kaniambia ndo anaitumia kwenye hiyo simu,

Niliendelea kuvumilia hii hali kwakua sikua na jinsi maana bado naendelea na matibabu. Hapa juzi kanitumia ujumbe kupitia Facebook anasema tuachane yy amechoka na maisha ya ndoa hivyo anahitaji kua single,haoni faida ya kua kwenye ndoa. Kwa kwel moyo wangu wote ulikua unawaka moto kwa maumivi makari sana

Kwakua bado naumwa halafu nakutana na changamoto kama hii. Ilinibidi nimtafute kwa kumpigia simu kupitia kwa mama ake akampa simu nikaongea nae.

Nilimuuliza kwan kipi kibaya ambacho nimekufanyia mpaka umefikia maamuz hayo ya kutaka tuachane?alinijibua kua yy amechoka na kudharauliwa hapo kwao maana inaonekama kama mimi nimemdamp tuu hapo kwao,

Nilimuuliza kwan hujui hali yangu ya kiafya kwasasa? Akanijibu kua anajua ila hayo ndo maamuzi aliyaamua kwan kichwa chake hakiko sawa,pia kazin kwake pia hajapandishwa mshahara hivyo hayuko sawa. Baada ya kuniambia hiyo alinikatia simu.

Ifahamike kua kipindi hiki chote ninachoumwa kaja kuniona mara moja tuu mpaka sasa ni mwez umekata hajaja kuniona.
Na mda huu yuko likizo haend kazin.

Naombeni ushauri wenu na mawazao nini nifanye kuinusuru ndoa yangu?hali yangu kiafya bado haija kaa sawa.ndoa inazidi kuniumiza msaada wenu tafadhali.
 
Si anataka kuachwa, muache mzee, usilazimishe kijani kuwa nyekundu, kwanini ubembeleze mapenzi, utakufa bure kwa kufosi mambo. Kwani bila ya yeye wewe hupumui, kifupi hana mpango na ww na ukilazimisha atakuja kukupiga tukio moja uione june-july

Katika makosa makubwa ni hili la mtu anataka kuachwa nawe umemganda, sasa ndio ukutee kicchwani empty set, hawezi kuwaza na kuwazua anajjichukulia kama yeye ndio oxygen gas yako.
 
Sijui Experience ya ndoa kwa maana sijaoa ila kwa akili ya kawaida tu hapo hakuna mapenzi. Na yalishakufa toka yupo mkoa hapo Dar mmekuja kuyazika tu.
Last attempt ni kutafuta sehemu Dar ya kuishi na kwenda kumchukua akikataa muache aende zake. It's not easy kufanya maamuzi hayo ila ndio best thing for your well-being.
 
Pole sana Mkuu,
Kitendo cha mke wako kutafuta uhamisho wa kwenda Dar, nyumbani kwao ilipaswa kukupa ishara kuwa kuna jambo baya katika ndoa yenu kwa upande wake...

Mke wako ni mtu anapenda vitu (material wife) na kazi alonayo inampa kiburi.
Na pia familia yake inahusika katika kumshauri vibaya.

Kama kweli unampenda mke wako, bas tafuta mganga wa kienyeji afanye yafuatayo,
1.Amfukuzishe kazi na asipate kazi milele na
2.Amrudishe kwako.

Kila la kheri...
 
Pole sana Mkuu,
Kitendo cha mke wako kutafuta uhamisho wa kwenda Dar, nyumbani kwao ilipaswa kukupa ishara kuwa kuna jambo baya katika ndoa yenu kwa upande wake...

Mke wako ni mtu anapenda vitu (material wife) na kazi alonayo inampa kiburi.
Na pia familia yake inahusika katika kumshauri vibaya.

Kama kweli unampenda mke wako, bas tafuta mganga wa kienyeji afanye yafuatayo,
1.Amfukuzishe kazi na asipate kazi milele na
2.Amrudishe kwako.

Kila la kheri...
Fimbo ya dunia nzuri zaidi amuache tu kiroho safi asikunje roho . Mke ameolewa na unarudi kwenu unapokelewa na una watoto na mume ... Hivi unaanzaje kumwambia dingi issue za hivyo ....kuna shida mahala ...
 
Sijui Experience ya ndoa kwa maana sijaoa ila kwa akili ya kawaida tu hapo hakuna mapenzi. Na yalishakufa toka yupo mkoa hapo Dar mmekuja kuyazika tu.
Last attempt ni kutafuta sehemu Dar ya kuishi na kwenda kumchukua akikataa muache aende zake. It's not easy kufanya maamuzi hayo ila ndio best thing for your well-being.
Nashukuru kwa hilo
 
Ndio maana sina ndoto ya kuoa na kua na familia, ila ukweli ni kwamba uyo mkeo ashapata mwanaume mwingine mwenye ela na hasa ukizingatia ww kifedha umeyumba basi apo amna kitu, na mtoto wa mjini daslam tena! Achana na uyo mwanamke akutaki Fanya mpango wa kutafuta ela ila kamwe usimsamehe uyo mwanamke maana kesho atarudi tena kwa magoti kuomba msamaha, angalia namna ya kulea watoto wako kwa kadri uwezavyo.

Vivid example ni mm mwenyewe nilikua na mke na mtoto. Mwanamke akaanza tu from no where anataka kuondoka pasi na sababu za msingi kujaribu kufanya kila kitu kumzuia tena tukiwa na wazazi wangu na ndugu zangu akakataaa na maneno machafu kama yote. Nikamuacha akaondoka, ni suala la wiki tu akataka kurudi na kwakua ckumfukuza na amna hoja ya msingi iliomuondoa nyumbani kwangu, kaka nilikataa na ndoa iliishia apo mpaka Leo aamini.

Funzo, mwanamke akidai kuondoka kwako au kuachana bila sababu za msingi yani ujampiga, ujalala nje ya nyumba na ujamnyanyasa kwa lolote, muache aende na kamwe akitaka kurudi usimruhusu muache jumla.
Naomba kuwasilisha.
 
Ndio maana sina ndoto ya kuoa na kua na familia, ila ukweli ni kwamba uyo mkeo ashapata mwanaume mwingine mwenye ela na hasa ukizingatia ww kifedha umeyumba basi apo amna kitu, na mtoto wa mjini daslam tena! Achana na uyo mwanamke akutaki Fanya mpango wa kutafuta ela ila kamwe usimsamehe uyo mwanamke maana kesho atarudi tena kwa magoti kuomba msamaha, angalia namna ya kulea watoto wako kwa kadri uwezavyo.
Vivid example ni mm mwenyewe nilikua na mke na mtoto. Mwanamke akaanza tu from no where anataka kuondoka pasi na sababu za msingi kujaribu kufanya kila kitu kumzuia tena tukiwa na wazazi wangu na ndugu zangu akakataaa na maneno machafu kama yote. Nikamuacha akaondoka, ni suala la wiki tu akataka kurudi na kwakua ckumfukuza na amna hoja ya msingi iliomuondoa nyumbani kwangu, kaka nilikataa na ndoa iliishia apo mpaka Leo aamini.
Funzo, mwanamke akidai kuondoka kwako au kuachana bila sababu za msingi yani ujampiga, ujalala nje ya nyumba na ujamnyanyasa kwa lolote, muache aende na kamwe akitaka kurudi usimruhusu muache jumla.
Naomba kuwasilisha.
Nashukuru kwa kunifariji mkuu,yaan kumpoteza mtu uliyemthamin na kushea mambo mengi inaumasana
 
Back
Top Bottom