Ndoa ya mama PHD na baba standard seven

Ndoa ya mama PHD na baba standard seven

Nisah

Member
Joined
Jul 7, 2012
Posts
9
Reaction score
1
Habari zenu wakuu. Naombeni mawazo yenu nimsaidie dada yangu maana yuko katika wakati mgumu wa kuamua.

Ni dada mwenye miaka 32, mtoto mmoja, elimu ya PHD.

Amekutana na mwanaume, mfanya biashara wa kawaida tu, elimu std 7, anaemzidi kama miaka mitatu.

Wanapendana na mwanaume amepropose anataka wafunge ndoa haraka iwezekanavyo. kinachomtatiza ndugu yangu ni kwamba anawasiwasi kuwa understanding capacity yao inaweza kuja kuwaletea shida huko baadae as wanaume wakioa wanawake wa aina hii kunakuwaga na inferiority complex fulani na mara nyingi hawachukulii vitu vingi kwa namna sawa.

Kuna ambae ana uzoefu na jambo hili na wenye mawazo naomba tumsaidie ndugu yetu.

Natanguliza shukrani
 
Hapo zamani wanawake hawakuruhusiwa kusoma kabisaa,ilionekana kuwa wanamajivuno sana nandivo ilivo,hata mwanake kumiliki pesa haikufaa hawa watu ndio maana shetan hua anawatumia kufanikisha mambo yao.st 7 usisubutu hapo hakuna ndoa.uliona wapi mwanamke tajiri au msomi akaolewa?japo sio wote wengi wao huwa wanajivunia walicho nacho,hivi mme wa be kiroboto mnamjua? Lakini anawatoto utashaa sasa
 
ziko ndoa za ma dr kwa dr hazidumu!mimi kwa imani yangu na uzoefu,ktk mahusiano na hasa ndoa elimu haijalishi kabisa!kwani hujaona mtu wa la saba amestaarabika,anajali,anajiheshimu na anamapenzi ya dhati kuliko wa ma degree?mimi nakupa mfano hai,dada yangu ana mume hajasoma,yeye nshomile mpaka huko juu na anapost nono tuu,lakini huyo shemeji ukiambiwa hajasoma,huwezi kuamini maana ni full mapenzi!na wana amani kibao ktk ndoa.cha msingi dada yako awe na mapenzi ya dhati kwa mumewe na amheshimu,na hana haja ya kuonyesha jamii kuwa mumewe hajasoma,ampige sopsop,maisha yasonge mbele!
 
Mimi sioni tatizo,kikubwa ni kupendana na kuheshimiana!Elimu ni muhimu lakini haiwezi kuzuia wapendanao washindwe kuishi pamoja!mwanamke atakuwa anatoa theories alizosoma darasani ili mwanaume ajifunze kutoka kwake.On the other hand mwanaume atakuwa anampa mke wake real life context principles,mwisho wa siku kila mtu atakuwa ana cha kujifunza kutoka kwa mwezake na ndoa inaweza kudumu!
 
Mimi sioni tatizo,kikubwa ni kupendana na kuheshimiana!Elimu ni muhimu lakini haiwezi kuzuia wapendanao washindwe kuishi pamoja!mwanamke atakuwa anatoa theories alizosoma darasani ili mwanaume ajifunze kutoka kwake.On the other hand mwanaume atakuwa anampa mke wake real life context principles,mwisho wa siku kila mtu atakuwa ana cha kujifunza kutoka kwa mwezake na ndoa inaweza kudumu!

I don't think it's that easy.

I just happen to believe that there has to be some sort of a balance.
 
Mmmh PHD..STD 7!!!
Siku mapenzi yakipungua mwanaume atajutaa huko ndani, labda aombe apendwe daima na milele na mwanamke awe na busara za kutosha!!!!
 
Hiyo ndoa ni ngumu..... Hapo kutakuwa na ''infirioriti'' and ''superioriti'' complex ya maana
 
I don't think it's that easy.

I just happen to believe that there has to be some sort of a balance.
Upo sahihi mkuu,lakini sote tumekuwa mashahidi wa matatizo makubwa yanayotokea kwa wanandoa hata kama kuna uwiano mkubwa wa kiwango cha elimu.Sidhani kama tofauti kubwa ya kielimu inaweza kuwa chanzo cha matatizo katika ndoa!Labda unieleze kidogo elimu ina umuhimu gani katika ndoa!
 
Ha ha ha PHD and STD 7!!! Labda kama huyo mwanaume ana hela ya nguvu!!! Ili mapenzi yatulizwe na pochi!!! Kwa kweli ni pagumu sana!!!! Japo pia wapo wanawake wachache ambao elimu yao haiwasumbui sana hata na hela pia!! Wengi wao akisoma tu na kamshahara kazuri ni hatari!! Kuna mmoja namfahamu mumuwe alimpa mimba akiwa kati ya form 4 or six na alipojifungua aliendelea na shule na mume pia akasoma japo kwa elimu ya kawaida. Imagine baada ya ile mimba mume yule aliamua kumsomesha mkewe first degree, second degree ili akimaliza na yeye aweze kujiendeleza kielimu maana wasingeweza kusoma wote kwa mshahara na familia (wana watoto wawili sasa). You know what!!!! Mke sasa ameajiriwa na post nzuri, safari za nje kwa sana na sasa anamalizia masters!!!! Ameamua kumwacha mume na kumwachia pia wale watoto!!!! Ameenda kupanga chumba!!!! Hao ndio wanawake!!! Jamani siku hizi bora upende, mguu moja nje mwingine ndani!!! You invest a lot but you reap pain!!!!
 
Mmmh PHD..STD 7!!!
Siku mapenzi yakipungua mwanaume atajutaa huko ndani, labda aombe apendwe daima na milele na mwanamke awe na busara za kutosha!!!!
Nakubaliana na wewe mkuu,kwa hiyo kitu cha msingi katika ndoa ni busara,na busara haipatikani darasani!!
 
Upo sahihi mkuu,lakini sote tumekuwa mashahidi wa matatizo makubwa yanayotokea kwa wanandoa hata kama kuna uwiano mkubwa wa kiwango cha elimu.Sidhani kama tofauti kubwa ya kielimu inaweza kuwa chanzo cha matatizo katika ndoa!Labda unieleze kidogo elimu ina umuhimu gani katika ndoa!

Kwanza niseme kuwa ni wazi haya mambo hayafuati kanuni.

Ila pia kuna kitu kinaitwa 'male ego'.

Uwezekano wa mwanaume huyo kujiona duni mbele ya mkewe ni mkubwa sana.

Sasa mwanaume akiwa na hisia za kujiona kwamba yeye ni duni mbele ya mwanamke wake kwa sababu hawalingani kielimu, hiyo si dalili njema ya kuwa na ndoa ama mahusiano yenye mafanikio.

Kitu ambacho labda kinaweza ku-offset hiyo disparity ni mkwanja mrefu.

Sasa wanaume wangapi wenye elimu ya darasa la saba ambao wanaweza kuwa na mkwanja mrefu kushinda mwanamke mwenye PhD.?

Labda Bakhresa tu:becky:
 
Habari zenu wakuu. Naombeni mawazo yenu nimsaidie dada yangu maana yuko katika wakati mgumu wa kuamua.

Ni dada mwenye miaka 32, mtoto mmoja, elimu ya PHD. Amekutana na mwanaume, mfanya biashara wa kawaida tu, elimu std 7, anaemzidi kama miaka mitatu. Wanapendana na mwanaume amepropose anataka wafunge ndoa haraka iwezekanavyo. kinachomtatiza ndugu yangu ni kwamba anawasiwasi kuwa understanding capacity yao inaweza kuja kuwaletea shida huko baadae as wanaume wakioa wanawake wa aina hii kunakuwaga na inferiority complex fulani na mara nyingi hawachukulii vitu vingi kwa namna sawa. Kuna ambae ana uzoefu na jambo hili na wenye mawazo naomba tumsaidie ndugu yetu. natanguliza shukran

KAmfunika hadi Nchimbi....
 
Kuna mmoja namfahamu mumuwe alimpa mimba akiwa kati ya form 4 or six na alipojifungua aliendelea na shule na mume pia akasoma japo kwa elimu ya kawaida. Imagine baada ya ile mimba mume yule aliamua kumsomesha mkewe first degree, second degree ili akimaliza na yeye aweze kujiendeleza kielimu maana wasingeweza kusoma wote kwa mshahara na familia (wana watoto wawili sasa). You know what!!!! Mke sasa ameajiriwa na post nzuri, safari za nje kwa sana na sasa anamalizia masters!!!! Ameamua kumwacha mume na kumwachia pia wale watoto!!!! Ameenda kupanga chumba!!!! Hao ndio wanawake!!! Jamani siku hizi bora upende, mguu moja nje mwingine ndani!!! You invest a lot but you reap pain!!!!
Mkuu elimu ni nyenzo ambayo mwanadamu akiipata,inatakiwa imsaidie kukabiliana na maisha.Elimu yoyote ambayo humpelekea mtu kufanya mambo ambayo hayakutarajiwa na jamii kufanywa na mtu mwenye elimu kama yake,basi hapo tunaweza kusema mtu husika hajaelimika,elimu aliyonayo ni kama mapambo tuu!!
 
Ha ha ha PHD and STD 7!!! Labda kama huyo mwanaume ana hela ya nguvu!!! Ili mapenzi yatulizwe na pochi!!! Kwa kweli ni pagumu sana!!!! Japo pia wapo wanawake wachache ambao elimu yao haiwasumbui sana hata na hela pia!! Wengi wao akisoma tu na kamshahara kazuri ni hatari!! Kuna mmoja namfahamu mumuwe alimpa mimba akiwa kati ya form 4 or six na alipojifungua aliendelea na shule na mume pia akasoma japo kwa elimu ya kawaida. Imagine baada ya ile mimba mume yule aliamua kumsomesha mkewe first degree, second degree ili akimaliza na yeye aweze kujiendeleza kielimu maana wasingeweza kusoma wote kwa mshahara na familia (wana watoto wawili sasa). You know what!!!! Mke sasa ameajiriwa na post nzuri, safari za nje kwa sana na sasa anamalizia masters!!!! Ameamua kumwacha mume na kumwachia pia wale watoto!!!! Ameenda kupanga chumba!!!! Hao ndio wanawake!!! Jamani siku hizi bora upende, mguu moja nje mwingine ndani!!! You invest a lot but you reap pain!!!!

Wanawakw wa Aina hii ndiyo wanatuharibia wanawake wooooootw tunaonekana si waaminifu, Lakini la hasha kaka yangu mm nimesomeshwa na mume wangu na ninaishi naye vizuri tu na ninamheshimu na kumpenda.
 
Kwanza niseme kuwa ni wazi haya mambo hayafuati kanuni.

Ila pia kuna kitu kinaitwa 'male ego'.

Uwezekano wa mwanaume huyo kujiona duni mbele ya mkewe ni mkubwa sana.

Sasa mwanaume akiwa na hisia za kujiona kwamba yeye ni duni mbele ya mwanamke wake kwa sababu hawalingani kielimu, hiyo si dalili njema ya kuwa na ndoa ama mahusiano yenye mafanikio.

Kitu ambacho labda kinaweza ku-offset hiyo disparity ni mkwanja mrefu.

Sasa wanaume wangapi wenye elimu ya darasa la saba ambao wanaweza kuwa na mkwanja mrefu kushinda mwanamke mwenye PhD.?

Labda Bakhresa tu:becky:
Nimekuelewa vizuri sana mkuu,kwa kiasi kikubwa tofauti ya kielimu inaweza kusababisha matatizo katika ndoa kama ulivyoelezea.Lakini,lazima pia tukubaliane kuwa kuna uwezekana (Ingawa ni mdogo) ndoa hiyo ikaishi kwa furaha na upendo,haya yote yatategemea sana busara zao!!
 
Wanawakw wa Aina hii ndiyo wanatuharibia wanawake wooooootw tunaonekana si waaminifu, Lakini la hasha kaka yangu mm nimesomeshwa na mume wangu na ninaishi naye vizuri tu na ninamheshimu na kumpenda.

Hongera sana LISA!! Mumeo anakupenda na anapenda uwe na maisha mazuri. Wanaume wengi sana wanapenda wake zao wasome ila ni kwa wachache wanawake wanapenda hata kuchangia ada ya mume asome!! Ni mmoja tu namfahamu mume alikuwa na certificate ya mambo ya materials management na mke masters. Binti alimkazania mume wake akasoma na akamaliza masters ya Materials pale Mzumbe na sasa anafanya zile za kimataifa nje!!!! Mke sasa anasoma PhD na mume amebaki na watoto japo ni sandwich programme!! haya ni mapenzi ya kwali. Kwa hiyo wachache wa ukweli wapo ila wengi ni waongo (wake kwa waume).
 
Nimekuelewa vizuri sana mkuu,kwa kiasi kikubwa tofauti ya kielimu inaweza kusababisha matatizo katika ndoa kama ulivyoelezea.Lakini,lazima pia tukubaliane kuwa kuna uwezekana (Ingawa ni mdogo) ndoa hiyo ikaishi kwa furaha na upendo,haya yote yatategemea sana busara zao!!

Since opposites attract,yes, it is very possible.

But likely?

Not so much.
 
NI RAHISI KWA MISINGI IFUATAYO
-mwanamke na mwanaume wote wakitambua na kuishi katika orole and postion zao kama mume na mke
-mwanamke asipoangalia kigezo cha elimu yake kama fimboa ya kuchapia huyo mume na mume asipotumia kigezo cha elimua yake kama unyonge wake kwa mkewe
-mwanamke hasa akikubali kujishusha na kukubali kuwa ameolewa na mume na sio PHD
-mwanaume ajiamini akijivunia uanaume wake na akatimiza majukumu yake kama mume
-mwanamke akikubali kuwa taken care of as while a husband is providing
-mwanamke na mwanaume wakiiacha mioyo yao iseme na iongoze ndoa yao
-mwanamke akiiiacha PHD yake getini na kuingia ndani kama mke

AND THE VICE VERSA IS TRUE!
 
NI RAHISI KWA MISINGI IFUATAYO
-mwanamke na mwanaume wote wakitambua na kuishi katika orole and postion zao kama mume na mke
-mwanamke asipoangalia kigezo cha elimu yake kama fimboa ya kuchapia huyo mume na mume asipotumia kigezo cha elimua yake kama unyonge wake kwa mkewe
-mwanamke hasa akikubali kujishusha na kukubali kuwa ameolewa na mume na sio PHD
-mwanaume ajiamini akijivunia uanaume wake na akatimiza majukumu yake kama mume
-mwanamke akikubali kuwa taken care of as while a husband is providing
-mwanamke na mwanaume wakiiacha mioyo yao iseme na iongoze ndoa yao
-mwanamke akiiiacha PHD yake getini na kuingia ndani kama mke

AND THE VICE VERSA IS TRUE!

That's easier said than done.
 
Back
Top Bottom