Ndoa nyingine wanaishi kama 'hostel'

Ndoa nyingine wanaishi kama 'hostel'

Na kipindi kile cha zamani mali zote zilikuwa chini ya baba, mashamba wakina mama wanaenda shamba kulima yakifikiwa kuvunwa mama hana chake ni ya baba kwa maana ingine uchumi ulikuwa ukimilikiwa kwa asilimia yote na wanaume na ukijumlisha na maadili ya enzi zile basi baba lazima awe kichwa cha familia tu...Sasa hivi hata sisi wanaume tunachangia kuporwa haki yetu ya kuwa kichwa cha nyumba..Mwanaume huna na hutaki kazi unalelewa tu na mwanamke uchumi wa familia anaushikilia mama wewe unabaki kumpeleka kazini then unazunguka tu na gari la wife mtaani hadi pesa ya nguo za ndani ni yeye anakupa...Hii tabia ya umarioo inatuaribia sifa zetu sana..Mwanaume umepaka rangi na umefuga kucha..Halafu uitwe kichwa cha familia...

tehe tehe tehe tehe..................................
 
wakati mwingine wanaume wenyewe mnasababisha mama aamue kuchukua jukumu la ubaba wenye nyumba kutoka na kushindwa kwenu kuyakabili majukumu yenu ya ubaba ya kila siku. Mama anakuwa ndie wa kutatua mahitaji ya familia kwa uharaka zaidi kuliko mwanaume.
 
Mwanamke anapata mimba mda wowote provided the right conditions ( maturity, egg, sperm, balanced hormones) utamlaumuje kwamba kaamua... Wewe si ungetumia condom au ufanye vasectomy basi kama unataka kujihakikishia hazai.
Mwili wa mwanamke huweza kupata mabadiliko ya vichocheo muda wowote kutokana na stress, mazingira na lishe hivyo unapolala na mwanamke hesabu mtoto maana anaweza kutokea hata nje ya hesabu ya siku za hatari zilizo-zoeleka.

Siyo kweli acha kupotosha.
 
huyu kabanga is my role model,for really....na hiyo avatar ya django unchained,ndo umemaliza kabisa...huwa hana mistari mirefu kwenye kuchangia hoja but maneno yake yanaishi aisee...Kabanga,SALUTE!
 
Kwa kijana anaefuta maadili ya kibantu kamwe hawezi kuwa hivyo. Hayo ni matokeo ya tamaduni za kitapeli.
Sifa za kichwa cha nyumba mmeipoteza wanaume wengi, unaishi kwenye nyumba hujui pango ni bei gani, unafungua fridge unatoa beer hujui mke wako ametoa wapi pesa. Hata wife akikwambia anakwenda seminar huna hata nguvu ya kuuliza utakaa muda gani.
 
Mwanamke Mmoja Nimemsikia Kwenye Tv Kwamba Kama Mwanamke Anajitosheleza Kiuchumi, Na Mwanaume Yuko Chini Yake, Wa Nini?
 
Umagharibi umechangia kwa kiasi kikubwa, na uko kwenye kitchen party ndo wanawake wanalishana sumu kabisa sasa akija kwa ndoa anaitapika kama ilivyo. Afu mambo ya mwanaume kutokuwajibika kwa familia nayo ni shiida katika hili.
 
Mwanamke Mmoja Nimemsikia Kwenye Tv Kwamba Kama Mwanamke Anajitosheleza Kiuchumi, Na Mwanaume Yuko Chini Yake, Wa Nini?

That is very wrong, huolewi kwasababu mwanaume mambo super, mwanamke ameumbwa kuwa msaidizi wa mwanaume lakini Mungu anaweza kuleta rizki kupitia mikono ya mwanamke.
 
ukiona unaogopa kuoa ujue una matatizo....sio wanawake wote wako hivyo
 
Hata kabla ya ndoa kero tupu....! Mdada anataka kutoa gundu tu!
Yaah!wenyewe wanaita kaangalie mkato wa chumba ndio kutoa gundu huko kisha waoaji wengine watafuatia.Kuna baadhi ya jamii ni sifa kubwa kwa mwanamke alie olewa mara nyingi.Huku kuna baadhi ya jamii mwanamke alie zaa anakuwa na nafasi kubwa ya kuolewa kuliko ambae bado mwali huku utetezi ukitoka kuwa huyo tayari ameshihirisha ana kizazi.
 
Mie nilikuwa nakampango ka kuoa ila baada ya kuona mwenza hajui hata majukumu yake kama mama nimepata wasiwasi.Eti anadai kuwa dunia ya sasa hamna kazi ya mwanamke wala ya mwanaume hvo asipofanya shughuli flani basi mie niifanye. Duuh... Ndoa za sasa ni kichefu chefu
 
Mie nilikuwa nakampango ka kuoa ila baada ya kuona mwenza hajui hata majukumu yake kama mama nimepata wasiwasi.Eti anadai kuwa dunia ya sasa hamna kazi ya mwanamke wala ya mwanaume hvo asipofanya shughuli flani basi mie niifanye. Duuh... Ndoa za sasa ni kichefu chefu

Kuna uzi niliuleta hapa, mtoto wa shost alikutana na boyfriend chuo kikuu, akawa mchumba hatimae mume. Wameanza maisha, baada ya kujifungua ndiyo kijana aliisoma number. Mke analoweka nappy za mtoto mpaka mume atoke kazini afue na kupika. Kijana alipopata upenyo wa kusepa hakugeuka nyuma.
 
Kuna uzi niliuleta hapa, mtoto wa shost alikutana na boyfriend chuo kikuu, akawa mchumba hatimae mume. Wameanza maisha, baada ya kujifungua ndiyo kijana aliisoma number. Mke analoweka nappy za mtoto mpaka mume atoke kazini afue na kupika. Kijana alipopata upenyo wa kusepa hakugeuka nyuma.
Vipi ulishapata mtoto na yule shemeji wetu wa age 31
 
Back
Top Bottom