Lakini pia zamani, ndugu zako wa kijijini ulikuwa unawatumia pesa kwa TMO inachukua mwezi mzima. Siku hizi, kwa M Pesa ni sekund kadhaa tu. Zamani, Dar - Mwanza ulitumia reli ya kati kwa siku 3, siku hizi ni masaa 12 tu kwa basi uko Mwanza. Zamani hakukuwa na Whatsaap, radia ilikuwa moja, gazeti la chama na serikali. Siku hizi taarifa zote unazipaata papo kwa papo kupitia Whatsapp na mitandao mingine ya kijamii. Tena haijalishi, aliye Kasulu, Tandahimba, Mererani, Dar, Tanga, Nairobi, New York, Tokyo au Madrid, as long as wote mko group moja la mnapata taarifa kwa pamoja.
Kifupi ninachotaka kusema ni kwamba, zama zimebadilika sana. Angalia maisha ya zamani, ukitaka kumtongoza mwanamke, inabidi umvizie anaenda kisimani, au dukani. Lakini siku hizi watu wanatongozana hata kama hawajawahi kuonana, ni kwa sababu ya mawasiliano kuwa rahisi. Wanandoa zamani ilikuwa vigumu ku cheat kwa kuwa ni ngumu kupata mawasiliano na mke au mume wa mtu. Na ukienda naye guest kila mtu atajua kwa kuwa watu walikuwa wachache. Siku hizi hayo yote yamerahishwa.