Ndoa na iheshimiwe na watu wote

Ndoa na iheshimiwe na watu wote

Bradha

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2017
Posts
8,786
Reaction score
45,268
Habari wana JF

Nimekua nikitafakari namna ambavyo baadhi ya mambo yamekua yakifanywa na wanandoa au marafiki zao licha ya kuwa mambo hayo ni
kinyume na matakwa au ustaarabu wa ndoa.Baada ya tafakuri hiyo nimejikuta nikikumbuka maneno haya ambayo tumekua tukiyasikia
sana tuu,"Ndoa na iheshimiwe na watu wote".

Inawezekana leo wewe ni mme/mke wa mtu na bahati mbaya ulishawahi kuwa na mahusiano kabla.Tafadhali, usiendeleze mahusiano au mazungumzo ambayo ni kinyume na matakwa ya ndoa.Kuwa wa kwanza kuiheshimu ndoa yako.Sio sahihi kuendelea kuitana majina yale ya kimahaba, kuzungumza mahaba hata kama mnatumia codes ambazo mnaelewa ninyi wenyewe.Jumuika na jamii(marafiki, wafanya kazi wenzako, majirani n.k) ukiwa kama mme/mke wa mtu.

Inawezekana una rafiki yako ambaye sasa hivi ni mme/mke wa mtu.Pengine ulikua unamshirikisha katika mambo ambayo unajua sio sahihi kuendelea kumshirikisha kwasababu ameshafunga pingu za maisha na mwenzi wake.Naomba kukuomba kuwa usimshirikishe tena.Ndio, ni mtu mzima na ana uwezo wa kukataa mwenyewe pale utakapomshirikisha ila nnachokuomba ni umpunguzie majaribu, usimshirikishe katika mambo unayojua mke/mme wake akijua ataumia kwamba kakosewa heshima.Ndoa na iheshimiwe na watu wote.

Mkuu inawezekana mahusiano uliyonayo saivi ni mahusiano na mke/mme wa mtu.Pengine uliyaanzisha kwa kujua kua huyo ni mme/mke mtu au pengine hukujua na umekuja kujua hivyo baada ya kuwa naye kwenye mahusiano.Ninachokuomba leo ni ujitafakari na uchukue maamuzi sahihi.Usikubali kuwa chanzo cha huzuni kwa mke au mme wa mtu.Kama unampenda huyo mke/mme wa mtu basi iheshimu ndoa yake na ukae mbali.Ni ushauri tuu.

Inawezekana kwa bahati nzuri au mbaya umefanikiwa kujua siri za ndani za ndoa ya rafiki au ndugu yako.Pengine alikuamini akakuambia matatizo yake au mapito wanayopitia katika ndoa yao.Tafadhali, usiwe wa kwanza kwenda kuwasema pembeni na kuwakejeli na badala yake angalia kama kuna namna ya kuwasaidia.Ndio, inawezekana anaibiwa mme/mke wake lakini kwanini unashangilia na kumcheka.Nyumba kubwa akisikia mchepuko mtaani anasifiwa atajisikiaje?Inakufaa nini kuyaweka matatizo ya mwenzako hadharani?Iheshimu ndoa yake na ujitahidi kuwa sehemu ya ufumbuzi kwa kadiri utakavyoweza.

Wakuu tupendane.Tusiishi kwa kunyoosheana vidole, haitatufaa kitu.Tujitahidi kujali wanaotuzunguka na kutenda kwa wema kwa kadiri Mungu anavyotujalia.Ni kweli, duniani tupo watu wa namna mbalimbali ila mimi na wewe tunaweza kusaidia kwa kuwa wema.

Nawatakia wiki njema.

NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.
 
"Ndoa na iheshimiwe na watu wote,na malazi yawe safi;kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu" Mtume Paulo aliwaandikia maneno hayo Waebrani wakati huo,.lakini Neno la Mungu kwakuwa halifi,basi tuyaishi maneno haya,.

Tukipendana katika roho na kweli bila unafiki lazima tuzione baraka za Mungu katikati ya maisha yetu,.ndoa ni baraka na ndio taasisi ya kwanza Mungu kuileta duniani hivyo hatuna budi kuiheshimu na kuitii kwa upendo na kwa uaminifu,kwa maana ndipo ilipo chemchem ya FURAHA ndani ya mioyo ya walioungana,.

Tusisahau kutembea katika imani na ukamilifu,pamoja na ukengeufu wa kibinadamu tunapokoseana tusiwe na mioyo migumu ya kushindwa kutubu na kuombana msamaha,.

Lindeni na mpende ndoa zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa lake.

Mungu akatubariki,sasa na milele.

Amen.
 
Ndoa nyingi hazina hadhi ya ndoa bali kichaka tu cha uhuni na umalaya wa siri siri,

Jamaaa umesema mambo muhimu sana na nguzo katika ndoa , kwa wale watao pitia post yako wakasoma mwanzo mwisho hakika na kama ndio atakuwa alijificha tu kwenye kichaka cha ndoa kwakufanya umalaya basi lazima atakata shauri nakuamua kuishi kama inavyo mpasa,

Tamaa haijawahi muacha mtu salama hata aweje, hivyo wana ndoa wabaki na ndoa zao.

Kama kuna ke anampango wakusimamia ndoa yake na yupo tayari kwa familia basi ani pm
 
"Ndoa na iheshimiwe na watu wote,na malazi yawe safi;kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu" Mtume Paulo aliwaandikia maneno hayo Waebrani wakati huo,.lakini Neno la Mungu kwakuwa halifi,basi tuyaishi maneno haya,.

Tukipendana katika roho na kweli bila unafiki lazima tuzione baraka za Mungu katikati ya maisha yetu,.ndoa ni baraka na ndio taasisi ya kwanza Mungu kuileta duniani hivyo hatuna budi kuiheshimu na kuitii kwa upendo na kwa uaminifu,kwa maana ndipo ilipo chemchem ya FURAHA ndani ya mioyo ya walioungana,.

Tusisahau kutembea katika imani na ukamilifu,pamoja na ukengeufu wa kibinadamu tunapokoseana tusiwe na mioyo migumu ya kushindwa kutubu na kuombana msamaha,.

Lindeni na mpende ndoa zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa lake.

Mungu akatubariki,sasa na milele.

Amen.
Ahsante sana mumu kwa hekima zako.

Umesema vizuri sana.
 
Ndoa nyingi hazina hadhi ya ndoa bali kichaka tu cha uhuni na umalaya wa siri siri,

Jamaaa umesema mambo muhimu sana na nguzo katika ndoa , kwa wale watao pitia post yako wakasoma mwanzo mwisho hakika na kama ndio atakuwa alijificha tu kwenye kichaka cha ndoa kwakufanya umalaya basi lazima atakata shauri nakuamua kuishi kama inavyo mpasa,

Tamaa haijawahi muacha mtu salama hata aweje, hivyo wana ndoa wabaki na ndoa zao.

Kama kuna ke anampango wakusimamia ndoa yake na yupo tayari kwa familia basi ani pm
Kweli mkuu.

Mungu akusaidie upate wa kufanana nawe.
 
Kwako! kwa kuwa umeandika kwa uchungu nikafikia my own conclusion
Sio mimi mkuu.Ukisoma kwa makini uzi unaweza kujua sababu.

Limeniuma sana swala la watu kushabikia "Mama mdogo wa taifa" na bahati mbaya hakuna mwenye uhakika wa taarifa hizi.Mnafikiri mama wa watu mwenye ndoa anajisikiaje?Yule ni kama mama yetu na tunamkosea sana heshima kwa kushabikia uvumi.

Na kama nikivyosema katika uzi, hata kama hizo taarifa ni za kweli, sio sahihi kukaa kuzizungumzia hadharani.
 
Back
Top Bottom