Huyo mwanamke hana hata makosa, makosa unayo wewe.
Hell is for devil na weak gents.
Ulitakiwa uanze kujiuliza kama aliyezaa nae alishindwa kumuoa, je, wewe ni nani mpaka ujitwike msalaba?
(Tufanye mapenzi upofu. Kufanya kosa si kosa bali kurudia kosa)
Unakula makofi bado upo tu.
(Tufanye kofi la mpenzi haliumi)
Unatukaniwa mpaka wazazi wako na mnaitwa idiot.
(Tufanye tusi la kiingereza haliumi)
Kimsingi hukuwa tayari kuoa na hujawa tayari.
Huyo mwanamke hana hata makosa, makosa unayo wewe.
Hell is for devil na weak gents.
Ulitakiwa uanze kujiuliza kama aliyezaa nae alishindwa kumuoa, je, wewe ni nani mpaka ujitwike msalaba?
(Tufanye mapenzi upofu. Kufanya kosa si kosa bali kurudia kosa)
Unakula makofi bado upo tu.
(Tufanye kofi la mpenzi haliumi)
Unatukaniwa mpaka wazazi wako na mnaitwa idiot.
(Tufanye tusi la kiingereza haliumi)
Kimsingi hukuwa tayari kuoa na hujawa tayari.
Uzoefu tu, nipo kwenye ndoa kwa muda mrefu, watoto wa ndoa idadi inaridhisha na huko nje pia nimezaa na wanawake tofauti tofauti idadi ya watoto inayoridhisha. Nakupa ushauri wa kiume, huyo mkeo hana makosa, mwenye makosa ni yule aliyekutangulia, alimuacha huyo demu huku akiwa bado anampenda, akitegemea labda ateseke ili waweze kurudiana au laa. Ulipoingia wewe kwenye hayo mahusiano, wewe ukawa umempa huyo mwanamke kiburi, ambacho ndio kilichomuumiza aliyekutangulia na kuja kukuambia maneno ya ajabu. Yale maneno aliyafanyia vitendo kwa mambo ya kiswahili na kupelekea hizo mimba zako kutokamatika, na huyo mwanamke kuvishwa sura nyingine ya kukuchukia wewe. Kama bado unampenda sana huyo mkeo, kutana na watu wa kiroho; na kama hiyo vita uiwezi, achana na huyo mwanamke endelea na maisha yako.
Hapo hamna ndoa ndugu
Uneshaambiwa hauwezi kuzaa naye ina maana jamaa kashamuendea kwa wataalamu
Mwanamke kashakwambia hawezi kuacha kuongea na mzazi mwenzake inamaanisha kwamba jamaa anamla unayemuita mke wako
Mshaanza kupigana chupa na kumwagana damu utakuja upigwe bisu la tumbo au uwekewe sumu ufe
Nenda kaishi na mwanamke uliyezaa naye huyo hakufai
Wanawake wasio na watoto wako wengi sana dunia hii,ikawaje ukaoa Single Maza?
1). Kuna kumpenda na Kumtegemea huyu mdada(mke) sio kama anampenda mumewe ila anahitaji huduma zake.
Huyo alie mzalisha hatoi huduma kama huyu alie nae, Mwanamke anae mpenda mume wake hawezi kuongea na mwanaume alie mzalisha na kumtekeleza.
Mume ndio msemaji na msimamizi wa familia baba mtoto akitaka kuongea au kumuona mtoto amtafute msemaji wa familia(mume) sio ex wake. Hii inaonesha Mwanamke bado ana hisia na mzazi mwenziwe.
2). Mwanaume usikubali kufanyiwa dharau na mke au Mwanamke kwasababu hii ni ishara ya usaliti. Anakufanya uanze kujishuku mwenyewe ili anapo kusaliti awe na sababu ya kusema si nilikwambia wewe dhaifu sasa niwachie anae weza afanye nitakavyo.
Je, bora niondoke?Ndugu zangu ambao mpo kwenye ndoa naombeni ushauri kabla sijafanya maamuzi yangu mwenyewe.
Nipo kwenye hii ndoa kwa miaka 11 ila mwanamke ambaye nilikutana nae alikuwa na mtoto tayari ila naomba niseme alikuwa mwenyewe na mtoto wa miaka 2 mwanaume wake alimkimbia, sasa baada ya hapo mwanaume wake wa zamani kufahamu huyu mwanamke ana mwanaume mwingine siku moja akaniambia kwamba huyu mwanamke huwezi kuja kumzalisha maisha yako yote hata iweje.
Ndugu zangu mpaka leo huyu mwanamke amepata mimba mara 3 ila zote zimetoka. Sasa baada ya hapo mwanamke akaanza kunidharau na kuniambia kwamba sina mbegu za kumzalisha. Me kama mwanaume nikapoteza confidence nikaenda kupiga nje na nimepata mtoto vizuri bila shida kabisa
Sasa amekuja kugundua kwamba me nimezaa nje ila nilivumilia mateso yote na maneno yote ya mateso na alikuwa muda wote ananidharau sana na kusema hata iweje umenikuta na mtoto na taka usitake siwezi kuacha kuongea na baba wa mtoto.
Akinikuta nakunywa anamwaga drinks zote kwenye sink.
Sasa jana usiku nimepigwa vyupa vibaya sana damu nyingi zimetoka sababu anataka tuwe tunatumia password moja, ameingia kwenye simu amekuta yule mwanamke mwingine mwenye mtoto amenitumia picha za mtoto.
Baada ya hapo akanitukania wazazi wote na kuwaita Idiots familia nzima pamoja na mimi...
Nilikuwa tu naomba ushauri nini cha kufanya ila tumeenda hospitali tumegundua zile mimba 3 alipata moja imeziba mirija yake ya uzazi so hawezi pata mimba kwa njia ya kawaida.
Naombeni ushauri wenu tafadhali kwa hili suala.
Je, bora niondoke?
Tuko pamoja kiongozi,usikate tamaa kwani kisichokuua basi kinakujenga. Bado una nafasi ya kufanya maamuzi sahihi.Najuta sana maisha yangu yote nimefanya makosa na kuwa mpole imenifanya nionekane mjinga kila mahala kwa ajiki ya upole wangu....
Daaa nashukuru sana tena sanaa nadhani umesema vitu vingi sana na kwa hilo kwa kweli nashukuru sana na nimekuelewa vizuri kabisaa....Nadhani umenishauri kutoka kwenye experience yako na kwa hilo asante sana ndugu yangu tena sanaa umeniambia kitu au ushauri ambao inabidi niufanyie kazi...Again asante sana...
Kusikia Kwa Kenge Mpaka Atoke Damu Puani Na MasikioniVumilia tu mkuu. Tulishasema humu hakuna kuoa mwanamke ambaye sio bikra, wewe ulikuwa wapi