Newera
Senior Member
- Mar 8, 2017
- 132
- 202
Nilipooa ndipo nikagundua kipato changu hakitoshi.
Kuoa kunahitaji kujipanga sana, baada ya kuoa maisha yangu kiuchumi yalibadilika sana. Kuna mambo yalikuwa yanaenda poa kwa sababu nipo single, nikaoa mambo yakabadilika.
Kodi ya nyumba kutoka double hadi kwenye apartment, mdada wa kazi, bajeti ya chakula si mtu mmoja tena bali familia.
Niliumia kwa mwaka hadi kuanza kuhangaika nje ya kipato changu cha kawaida. Utanashati wangu uliisha kabisa, kununua nguo kila leo kukaisha, nikajifunza kuwekeza, kusave na kuishi kama mtu mzima.
Tuwaheshimu sana wanaume wanaomudu familia zao, tuwapongeze wazazi kwa kutulea. Usimlaumu aliyeshindwa mambo si mepesi, wanaume tupambane sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuoa kunahitaji kujipanga sana, baada ya kuoa maisha yangu kiuchumi yalibadilika sana. Kuna mambo yalikuwa yanaenda poa kwa sababu nipo single, nikaoa mambo yakabadilika.
Kodi ya nyumba kutoka double hadi kwenye apartment, mdada wa kazi, bajeti ya chakula si mtu mmoja tena bali familia.
Niliumia kwa mwaka hadi kuanza kuhangaika nje ya kipato changu cha kawaida. Utanashati wangu uliisha kabisa, kununua nguo kila leo kukaisha, nikajifunza kuwekeza, kusave na kuishi kama mtu mzima.
Tuwaheshimu sana wanaume wanaomudu familia zao, tuwapongeze wazazi kwa kutulea. Usimlaumu aliyeshindwa mambo si mepesi, wanaume tupambane sana.
Sent using Jamii Forums mobile app



