Ndoa inaelekea kunishinda

Ndoa inaelekea kunishinda

Na Mimi nawaza kitu Kama hicho niwe tu bize na maisha yangu na mwanangu aliye tumboni nafikiria kwanzia Leo nisishike simu yake Wala nisimfatilie akiamua kuchepuka achepuke maana nshaona nikijua naumia alafu ameshanikatisha tamaa coz ndokwanza tuna miezi 6 kwenye ndoa alafu namfuma na wanawake 3 Bora hata angekuwa mmoja ningesema labda kwakuwa na mimba ameona anitafutie msaidizi nafikiria hata siku akitaka nishiriki nae niwe tu Mimi natumia nae condom maisha yote kujiepusha na maradhi maana nimewasiliana na wadada wawili kati ya hao wanasema walikuwa hawatumii condom mmoja ndoanasubiri kazi ya upolisi hivyo alimforce wakapime ukimwi kuhofia asijepata maambukizi akakosa kazi, yani hata hajali afya yangu na mtoto wake mpaka Kuna wakati inanijia roho ya kishetani nawaza sijui nimchomee hata ndani jamani naumia Basi tu mpaka naona tena Kama huu ujauzito nlobeba ni mzigo kwangu maana mimba tu nayo inanitesa naumwa badala ya yeye kuwa faraja kwangu ndokawa Moto ananichoma
Ukishamchomea ndani.. umeshafikiria hatma yako baada ya hapo?...
Maisha lazima yaendelee..ndio viapo vya "Kwa raha na shida"...

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Bado naendelea kuona maajabu ya wanaume wa jf!

Utaskia piga chini!😂 (mtoa mada angekua wa kiume)

Dada kuwa busy na mimba yako usimfuatilie utajiumiza kitu ambacho si sawa kwa hali ulionayo.

Ndivyo walivyo.. inawezekana hakukuonesha kipindi chote cha hiyo 5 yrs ya mahusiano ila sasa ameona yupo free ameshakuoa na huna pa kwenda au cha kumfanya kwa kuwa unampenda.
 
Na Mimi nawaza kitu Kama hicho niwe tu bize na maisha yangu na mwanangu aliye tumboni nafikiria kwanzia Leo nisishike simu yake Wala nisimfatilie akiamua kuchepuka achepuke maana nshaona nikijua naumia alafu ameshanikatisha tamaa coz ndokwanza tuna miezi 6 kwenye ndoa alafu namfuma na wanawake 3 Bora hata angekuwa mmoja ningesema labda kwakuwa na mimba ameona anitafutie msaidizi nafikiria hata siku akitaka nishiriki nae niwe tu Mimi natumia nae condom maisha yote kujiepusha na maradhi maana nimewasiliana na wadada wawili kati ya hao wanasema walikuwa hawatumii condom mmoja ndoanasubiri kazi ya upolisi hivyo alimforce wakapime ukimwi kuhofia asijepata maambukizi akakosa kazi, yani hata hajali afya yangu na mtoto wake mpaka Kuna wakati inanijia roho ya kishetani nawaza sijui nimchomee hata ndani jamani naumia Basi tu mpaka naona tena Kama huu ujauzito nlobeba ni mzigo kwangu maana mimba tu nayo inanitesa naumwa badala ya yeye kuwa faraja kwangu ndokawa Moto ananichoma

Wazo la kumchoma moto litoe kabisa mawazoni mwako,huyo ni shetani mbaya anakuchochea ukishatimiza hiyo azma anakuacha kisha unabaki na majuto mengi.. Uko tayari kujifungua ukiwa jela? PLEASE NO..!
Ishu ya kutoshika simu yake ni the best option.. Matatizo acha yaje yenyewe usiyatafute
Ishu ya kutumia condom ni sahihi pia lakini nyie mkiwa kama wanandoa mnaongeza UFA mkubwa, na pia kumbuka kuna magonjwa mengine kama hepatitis B huo ni afadhali hata ukimwi.. Kuna ishu pia ya magonjwa ya kiroho kama nuksi, mapepo, kupungua kwa kinga za kiroho, kuibiwa nyota, kutekwa na jini mahaba nknk

Kuna ishu nyingine hapa ambayo huwa wengi hawaijadili, sometimes mwanaume kuwa malaya wakati mkewe akiwa mjamzito ni side effect za mimba, kama zile hali zinazompata mwanamke za kutapika, kukosa hamu ama kutamani vyakula fulani fulani, nk kuna baadhi ya wanaume huamkwa na pepo baya la ngono na baada tu ya kujifungua pepo husepa
Kwa sasa shughulika na mtoto aliye tumboni ili asiathike afya ya akili tangu tumboni
 
Huyo mumeo hajaanza kukusaliti Jana wala Leo au baada ya ndoa ulikua unajua tabia yake since mwanzoni but ulijipa moyo atabadilika akikuoa au ulikomaa sana na ndoa ukitaka kuwakomesha wanawake wenzako mliokua ktk kinyang'anyiro cha kuvaa shela.
Tatizo wanawake wengi tunafia ndoa au tunang'ang'ania kuolewa hata km unaona mwanaume kimeo haswaa ndoa za kanisani wadada wanaamini wakiolewa hawaachiki wao ndo wao hapo ndo tunafeli...mwanaume anakuoa na mambo yake anafanya
Nakuja kukushauri:Angalia mema yake na mabaya yake then pima mzani mzani ulikoelekea!ila mwaka mmoja baado sana!
Halafu una kiumbe tumboni tulia usijemdhuru mtoto akaziliwa na shida
La mwisho usipende saaana kupekenyua pekenyua kipindi hiki utamuumiza mtoto na kama huwezi muacha mwanaume usimchunguze!!!
 
Usikate tamaa,vumilia tu,Usiondoke pambana na ndoa yako,hao michepuko wanapita tu

Hiyo ndiyo hulka ya mumeo kwahiyo ipotezee usimfuatilie ukimfuatilia utazidi kuumia kila kukicha,kikubwa asikuletee malazi tu.

Hakuna haja ya kushtaki kwa mchungaji

Wanasema ndoa kuvumilia,kwahiyo vumilia.


Wanaume na michepuko kama chura na maji.
Mbona wewe mwenyewe una jichanganya kumpa ushuri,sas akimuacha aendelee kuchepuka ataepukaje na kuletewa magonjwa?usiwe double standard.
 
Nami naomba kweli Mungu akutie nguvu, mimi kabla sijaoa ningekupa pole, lakini kwa sasa nakupa pongezi .
Kwanza mume wako ni mwanaume hasa! HASA.
Pili wewe unathamani kwake na ndio maana mpaka sasa yupo na wewe vinginevyo ingekua yupo na mmojawapo wa hao.
Tatu hata hayo maandiko tunayo ya rejea unakuta huko kuna vifungu vinavyoonyesha mwanaume fulani alikua na wake zaidi ya mmoja, rejea kwa yakobo, alikuwa na wake rasmi wawili na alizaa na wake wawili wasio rasmi na hao watoto waliotokana na wake hao wanne ndio taifa teule la Mungu huyo huyo unae enda kumshirikisha mchungaji.

Nguvu zilizo ndani yetu za ngono hazistahimiliki kwa mwanamke mmoja nyakati zote, yaani maisha yote ya mwanaume awe na mwanamke mmoja hio haipo hata huyo mchungaji anajua, nakwambia anajua ila uchungaji ndio umemsitiri

Kwenu wanawake sio tu kwamba mnaweza kuwa na mwanaume mmoja tu bali mnaweza kutokua na mwanaume na maisha yakaenda.

Badilisha fikra ,lea ndoa yako , lea ujauzito wako ,lea mume wako.

Pole lakini.
Asante
 
Simu Mimi ndonilimlazimisha ache nilimwambia kwakuwa ushamwambia una mke na umeomba msamaha tuanze upya simu niachie hakuna tena kumiliki simu ya Siri na nilifanya makusudi ili nijue Kama Kuna wengine Ila sahivi najutia nlichofanya coz naumia hata nikisema nishirikishe wazazi na wachungaji napata wakati mgumu maana najua ni watu wa dini hawatokubali tuachane watafanya juu chini aombe msamaha yaishe mwisho wa siku nitakuwa tu nimejitia aibu kwa kuwaelezea upumbavu wa mme wangu
Huna haja ya kuwashirikisha watu wa nje kwa sasa, nyie ndio watatuzi wa msingi kwenye hili tatizo na mengine ndani ya ndoa.. Mkishindwa kuyamaluza ndani nje itakuwa ngumu
All in all mpe muda kama kweli msamaha alioomba amemaanisha utajua tuu lakini kama ni tabia yake YATAJIRUDIA TENA NA TENA
 
Simu simu simu!

Wewe huna simu ya siri? Mumeo ana rukhsa ya kushika simu yako?

Siku hizi kwanza mnafunga ndoa za nini?

Unakuta wanandoa eti ni marufuku kila mmoja kushika simu ya mwenzake.

A dead giveaway.

Vumilianeni tu sasa. Ndoa mliitaka wenyewe…

Mkishindwa kuvumiliana, achaneni.

Kuachana siyo mwisho wa dunia.

Na hata ingekuwa mwisho wa dunia, ni bora tu kuachana kuliko kuendelea kudanganyana kama mko mataahira.
Umemaliza kila kitu
 
Huyo mumeo hajaanza kukusaliti Jana wala Leo au baada ya ndoa ulikua unajua tabia yake since mwanzoni but ulijipa moyo atabadilika akikuoa au ulikomaa sana na ndoa ukitaka kuwakomesha wanawake wenzako mliokua ktk kinyang'anyiro cha kuvaa shela.
Tatizo wanawake wengi tunafia ndoa au tunang'ang'ania kuolewa hata km unaona mwanaume kimeo haswaa ndoa za kanisani wadada wanaamini wakiolewa hawaachiki wao ndo wao hapo ndo tunafeli...mwanaume anakuoa na mambo yake anafanya
Nakuja kukushauri:Angalia mema yake na mabaya yake then pima mzani mzani ulikoelekea!ila mwaka mmoja baado sana!
Halafu una kiumbe tumboni tulia usijemdhuru mtoto akaziliwa na shida
La mwisho usipende saaana kupekenyua pekenyua kipindi hiki utamuumiza mtoto na kama huwezi muacha mwanaume usimchunguze!!!
✅✅✅✅✅
 
Na Mimi nawaza kitu Kama hicho niwe tu bize na maisha yangu na mwanangu aliye tumboni nafikiria kwanzia Leo nisishike simu yake Wala nisimfatilie akiamua kuchepuka achepuke maana nshaona nikijua naumia alafu ameshanikatisha tamaa coz ndokwanza tuna miezi 6 kwenye ndoa alafu namfuma na wanawake 3 Bora hata angekuwa mmoja ningesema labda kwakuwa na mimba ameona anitafutie msaidizi nafikiria hata siku akitaka nishiriki nae niwe tu Mimi natumia nae condom maisha yote kujiepusha na maradhi maana nimewasiliana na wadada wawili kati ya hao wanasema walikuwa hawatumii condom mmoja ndoanasubiri kazi ya upolisi hivyo alimforce wakapime ukimwi kuhofia asijepata maambukizi akakosa kazi, yani hata hajali afya yangu na mtoto wake mpaka Kuna wakati inanijia roho ya kishetani nawaza sijui nimchomee hata ndani jamani naumia Basi tu mpaka naona tena Kama huu ujauzito nlobeba ni mzigo kwangu maana mimba tu nayo inanitesa naumwa badala ya yeye kuwa faraja kwangu ndokawa Moto ananichoma
Pole sana best usifikie hukoo!vumilia Lea mwanao atabadilika huyoo!ondoa mawazo hasi au kumfanyia mambo mabaya utafungwa na kusababisha matatizo
Acha kumfatilia na hao wanawake zake unajitia presha buree!
 
Wazo la kumchoma moto litoe kabisa mawazoni mwako,huyo ni shetani mbaya anakuchochea ukishatimiza hiyo azma anakuacha kisha unabaki na majuto mengi.. Uko tayari kujifungua ukiwa jela? PLEASE NO..!
Ishu ya kutoshika simu yake ni the best option.. Matatizo acha yaje yenyewe usiyatafute
Ishu ya kutumia condom ni sahihi pia lakini nyie mkiwa kama wanandoa mnaongeza UFA mkubwa, na pia kumbuka kuna magonjwa mengine kama hepatitis B huo ni afadhali hata ukimwi.. Kuna ishu pia ya magonjwa ya kiroho kama nuksi, mapepo, kupungua kwa kinga za kiroho, kuibiwa nyota, kutekwa na jini mahaba nknk

Kuna ishu nyingine hapa ambayo huwa wengi hawaijadili, sometimes mwanaume kuwa malaya wakati mkewe akiwa mjamzito ni side effect za mimba, kama zile hali zinazompata mwanamke za kutapika, kukosa hamu ama kutamani vyakula fulani fulani, nk kuna baadhi ya wanaume huamkwa na pepo baya la ngono na baada tu ya kujifungua pepo husepa
Kwa sasa shughulika na mtoto aliye tumboni ili asiathike afya ya akili tangu tumboni
Mimi mwenyewe swala la condom tena wanandoa linanipa wakati mgumu Ila sasa nafanyaje mtu mwenyewe ana miaka 30 Ila hasikii dah! Inaumiza sana yani hata haogopi magonjwa Ila itabidi tu tutumie Sina namna Mimi ni muoga sana wa magonjwa yani nisipotumia nae Kinga nitawashwa kumfatilia Ila nikitumia kidogo naweza nikajicontrol kumfatilia
 
Kama ni movie ndio kwanza ipo kwenye ....
”Starring”....“Executive Producers”...”Title”... usijaribu kuvunja ambacho mungu amekiunganisha mkuu!

Nachokiona wewe umeolewa ila ni mgeni kwenye michezo ya mapenzi. Nikutoe hofu tu kuwa wanaume 80% huwa wana cheat ila kwa adabu sana! 20% ndio ambao hawana adabu kwenye cheating wao hawana aibu kuonesha kuwa wana cheat na hawa ndio wabaya sana.

Ukivunja ndoa sababu mume ameku cheat jua uendako pia utachitiwa tu na utakuwa dissapoonted mara mbili! Jifunze kuishi na hio hali kuwa mumeo sio muaminifu na maumivu yakizidi na wewe tafta mtu akugongege kwa siri ili akufariji. Hio ndio namna ya kupunguza machungu ila usiache kumuheshimu mumeo hata ukishaanza kuliwa maana ukiteleza hapo tu utapewa talaka kwa aibu na fedhea. Liwa nje ila usianze dharau na kejeli utakamatwa.
Ushauri wako una nguvu za Giza aseeehh!achepukee!two wrong can't make it right man!
 
Ushauri wenu jamani mimi nimeolewa nipo kwenye ndoa hatujamaliza hata mwaka Ila kinachoniumiza mme Wangu ananisaliti, nimemkuta anamiliki simu ya Siri pamoja na line alikuwa kaficha kabatini baada ya kugombana naye akakubali kuwa ana mchepuko akampigia akaweka loud nikawa nawasikia akamuomba samahani kwa kumchezea akamwambia Mimi nimeoa, nina mke nmeona siyo vizuri kumsaliti mke wangu dada akalalamika we badae akakubali kumblock kidogo nikapata amani.

Baada ya hapo hiyo simu ya Siri akaweka mezani akatoka zake Ila kilichoniumiza zaidi baada ya lisaa zilikuwa zinaingia text kutoka no. tofauti tofauti 2 baada ya kuchart nao kumbe nao ni michepuko yake tena jumla nimemfuma na wanawake 3 kwa wakati mmoja.

Msamaha kaniomba Ila nashindwa kumsamehe, naumia sana Bora ningemkamata hata na mmoja nisingeumia sana Ila wa 3 ukitegemea ndoa haina hata mwaka nawaza sijui kalogwa, natamani nimshirikishe hata mchungaji wetu Ila napata wakati mgumu naona ni vitu vya aibu hata kushirikisha watu wetu wa karibu. Natamani niondoke Ila kinachonipa wakati mgumu tayari Mimi ni mjamzito yaani nawaza ingekuwa siyo hii mimba ningeachana nae ananifanya Hadi nakata tamaa na mimba niliyonayo kitu ambacho ni dhambi, Naombeni mnishauri nifanyaje nahisi kuchanganyikiwa nakosa maamuzi presha imeshuka naona Kama dunia imeniangukia kweli ndoa ni ngumu sana duh! Mungu anitie tu nguvu.
Shirikisha watu wazima katika hilo tatizo usikae nalo peke yako. Nenda kwa shangazi au mama mkwe wako umweleze watakusaidia.

Vijana wengi wanapooa uwa wanakuwa wagumu kuachana na tabia za ujana mpk upite muda kidogo.
Usifikirie kuondoka kabla ya kusolve hiyo kesi ukiona habadiliki ndio unaweza kuchukua hatua nyingine.
 
Simu Mimi ndonilimlazimisha ache nilimwambia kwakuwa ushamwambia una mke na umeomba msamaha tuanze upya simu niachie hakuna tena kumiliki simu ya Siri na nilifanya makusudi ili nijue Kama Kuna wengine Ila sahivi najutia nlichofanya coz naumia hata nikisema nishirikishe wazazi na wachungaji napata wakati mgumu maana najua ni watu wa dini hawatokubali tuachane watafanya juu chini aombe msamaha yaishe mwisho wa siku nitakuwa tu nimejitia aibu kwa kuwaelezea upumbavu wa mme wangu
Kwa sasa usifanye nae mapenzi, atakuletea magonjwa utaumia zaidi, na usimuulize kitu chochote kuanzia sasa ingawa najua ndo atapata nafasi ya kufanya ujinga wake.

Kama kweli hataki kukupoteza, ukamnyamazia kila kitu, utaona akiumia mwenyewe, usimjibu tusi lolote kaa kimya akilala nje usimuulize kalala wapi. Kama anakujitaji atabadilika, kama hakuhitaji utaona akifurahia hiyo hali .

Jitahidi umalize miaka miwili tuone, ikishindikana baada ya miaka miwili omba taraka, usijitafutie kifo mwenyewe.

Kuna dada mmoja yamempata kama yako baada ya miezi 7 ya ndoa, mwanzoni mwanaume alikuwa akiomba msamaha, siku wamegombana kwa hasira mme akafunguka.

" kwanza wewe ndo ulikuwa ukilazimisha ndoa kisa umri umeenda mimi nilitaka tuendelee kusomana kwa muda zaidi, miaka miwili ilikuwa haitoshi mimi kufanya maamuzi . ndio na mimi ni mtu mzima ila na fulani nampenda nashindwa kumuacha"

Hapo ndo dada wa watu amejua kuwa hakuna mapenzi, dada ana 34 mwanaume ana 38.

Wiki iliyopita ilikuwa wiki ya sheria , dada alikuja kuomba ushauri afanye nini. Nimesituka nikajua ni wewe ila mwisho nimejua sio wewe naana yeye bado hana mimba.

Kweli ndoa ni ngumu.
 
Pole sana dada lakn nachoweza kukushauri ni kuwa mvumilivu ili mradi anakuomba samahani atapunguza ama kuacha kabisa bahati mbaya hao michepuko nao hawawezi kudondoka wote ghafla mpe muda awatoe taratibu kabla hujafanya maamuzi yako, usikute ameanza nao kabla yako na kaamua ww ndo akuweke ndani maana ake ww ndo mwenye mme tulia sana. Ila kama ameanza nao wakati mko kwenye ndoa hiyo itakuwa tabia yake. Fanya kile moyo unataka ili usiumize mtoto wa tumboni.
 
Na miaka 28 nina miaka naye mi 5 kabla ya ndoa na alikuwa hayupo hivi mpaka nawaza au kalogwa mbona ghafla wanawake wote hao alafu Bora ingekuwa hata ana muda nao nilivyongea nao wawili kawatongoza mwezi wa 12 mmoja ndo toka mwezi wa 11 yani kinachonishangaza kwanini wote iwe ghafla ndani ya mwezi mmoja
Either uhuni ni hulka yake au kuna nguvu za giza. Shetani hapendagi kuona watu wana furaha. Wewe cha kwanza kama una wifi yako mnaelewana mwambie. Mimi naamini dada wa mumeo hawez yaanika mapungufu ya mdogo ake. Akiendelea na hiyo tabia basi hakufai.

Sio kila ndoa ni lazima mzeeke pamoja. Kuliko kua na mawazo ya kuua bora urudi kwenu aibu utaipata kwa muda mchache lakini utakua na amani ya moyo kwa muda mrefu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom