Ndoa inaelekea kunishinda

Kwani wewe kabla hajakuoa hukuwa na michepuko? Mwanaume ukimchunguza sana ndoa itakushinda amekuoa maana yake amekuona unamfaa akaacha wote akaamua kukuweka ndani Ili mpate familia usikate tamaa focus kwenye ndoa achana na mambo ya kumfuatilia
 
Hahaha nilikuwa nimenuna Ila umenifanya nimecheka ushauri wako nitaufanyia kazi
Huu ushauri ndo umeuona wa kukufurahisha?
Na umeahidi kuufanyia kazi basi sawa. Utanitambua vizuri, kwanza nshaongeza mwingine wa nne na nimenunua simu nyingine naicha ktk chaji kibandani siji nayo nyumbani.
 
Ushauri wangu kwako!

Kwasasa muweke pembeni kimawazo na kihisia usije ukakosa vyote, hudumia mimba yako ujifungue salama .. Kumbuka huyo ndio atakuwa faraja yako
Wanawake wengi kwenye ndoa, watoto ndio hua faraja zao na si mme tena, sijui hua kunatokeaga nini
 
hapo chacha kwamba unamuacha mtu kisa kucheat??? aaah utani huo....labda hiyo cheating iambatane na mambo mengine kama vipigo, na matabia mengine mabaya ila cheating plain??? ooohhh tutazikana siachi mtoto wa mtu
 
shauri kama hizi zimepitwa na wakati, yaani aendelee kukaa kisa mimba kwani baba wa mtoto akifa Leo hiyo mimba hawezi kulea peke yake? afya yako ni muhimu Sana kuliko kitu kingine mama afu muache uoga wa maisha wanawake pambaneni
 
shauri kama hizi zimepitwa na wakati, yaani aendelee kukaa kisa mimba kwani baba wa mtoto akifa Leo hiyo mimba hawezi kulea peke yake? afya yako ni muhimu Sana kuliko kitu kingine mama afu muache uoga wa maisha wanawake pambaneni
Unaanzaje kumshauri mtu avunje ndoa yake??
 


Ukewenza ndio asili ya mwanadamu kivipi?

Mbona ndio ya kwanza Mungu aliumba mume mmoja na mke mmoja tu ? Yaani Adam na Hawa tu?

Ingekuwa ni serious kiasi hicho si Adam angeumbiwa mke zaidi ya mmoja kuonesha msisitizo?
 
Wanawake wengi kwenye ndoa, watoto ndio hua faraja zao na si mme tena, sijui hua kunatokeaga nini
Na Mme siku akichokwa na michepuko na kurudi nyumbani anakuta mama/mke tayari anahimaya yake na watoto wake, anabaki kulia lia mke wangu amewalisha sumu watoto, kumbe sumu aliiacha mwenyewe mlangoni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi huu ushauri wako umezaa matunda? Au bado hajaleta feedback?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…