- Thread starter
- #61
....... Siupendi kabisa usemi usemao ndoa ndoano... sipendi.... lakini mpwa wangu ana chini ya miezi 4 ndani ya ndoa yaani ni ndoa changa......... lakini jamaa kesha mtoa jino na ngeu na kumharibia reception yake.... jamani ndoa hii ni ya Kanisani.........hivi kwa hali kama hii kuivunja ndoa hii kuna makosa kweli?
............. Mashauriano juu ya kupatanisha ndoa za watu mara nyingi huwa hayafikii muafaka ya watu kurudiana na kuendelea na upendo kama ulivyokuwa awali.....ni ndoa chache sana ambazo zimetengamaa baada ya wazazi, wachungaji, mashekhe na watu wenye busara kuingilia kati....... lakini hoja yangu binafsi katika swala hili ni kujua kuivunja ndoa kama hii ambayo ni ya kanisani.....ni sawa ama la? maana wanaposema aliowaunganisha MUNGU mwanadamu asiwatenganishe..... ndo katika hali kama hii ya kupasuana?