Ndoa ina changamoto zisizoisha

Ndoa ina changamoto zisizoisha

Yeye anatakiwa asimame kwa miguu yake yeye ndo anae umia moyo akiona hawezi aondoke ila akiona bado anayamudu aendelee tuu kuvumilia ila akumbuke kuna magonjwa
 
Ndoa nyingi zinakuwa na changamoto kwa kuwa zinafungwa kwa nguvu na sababu za kimaumbile na ki matamanio na sio ki mapenzi.........

Nguzo ya kwanza ya ndoa imara ni UPENDO.....

Kwenye upendo wa kweli kuna kuvumiliana

Kwenye upendo wa kweli kuna kujaliana

Kwenye upendo wa kweli kuna kutahaminiana

Kwenye upendo wa kweli kuna kuheshimiana.....

Mwanamume mwenye upendo wa kweli kwa mke wake Furaha ya mke wake ni jambo la msingi na la muhimu kwake.....hivyo basi huyatambua majukumu yake na kuyatekeleza bila shuruti......

Vivo hivyo kwa mwanamke mwenye mapenzi ya dhati kwa mumewe......

Nyumba yao hujala na furaha muda wote kwani kila mmoja anapenda kumuona mwenzake akifurahi.......

Ndoa zilizofungwa kwa matamanio Daima haziishi migogoro na maugomvi.....kwani uhalisia unawatoa unawatoa nje ya matamanio na kujua kuwa hukufanya maamuzi sahihi.......

Kabla hujafanya maamuzi yoyote yanayohusu Ndoa jaribu kusema na moyo wako ukiwa peke yako......Daima moyo haudanyanyi isipokuwa matamanio yanatuzidi nguvu na kuupuuza moyo......

Ni vigumu kuwatenganisha wapendanao kwani Daima mioyo yao huishi pamoja
Kweli kabisa ukioa mke wa mtu lazima utasalitiwa tuu. Nilioa mke wa watu si kusalitiwa huko.
 
Yeye anatakiwa asimame kwa miguu yake yeye ndo anae umia moyo akiona hawezi aondoke ila akiona bado anayamudu aendelee tuu kuvumilia ila akumbuke kuna magonjwa
Hili la magonjwa ndo balaa
 
Kweli kabisa ukioa mke wa mtu lazima utasalitiwa tuu. Nilioa mke wa watu si kusalitiwa huko.
Mhhh,kwamba akiachana na mume wake,akiolewa ataendeleza nae?
 
Pole sana Dada yangu kwa kuishi na MTU wa kuumiza moyo wako, binafsi nimeoa sipendi michepuko kwani najua maumivu yake na sijui nikigundua mke wangu anatabia hiyo, but mungu aturehemu
Mungu akusaidie uendelee na huo msimamo
 
Mhhh,kwamba akiachana na mume wake,akiolewa ataendeleza nae?
Hapana kuna mwanamke anamtongoza akiwa tayari kwenye mahusiano na mwanaume anayempenda kwa dhati. Lakini mwanaume huyo anaweza kuwa kashaoa tayari hivyo basi mwanamke anakubali kufunga ndoa hali anampenda zaidi yule mwanaume ambaye tayari yupo kwenye ndoa au kwasababu fulani hawezi kumwoa.
 
Hapana kuna mwanamke anamtongoza akiwa tayari kwenye mahusiano na mwanaume anayempenda kwa dhati. Lakini mwanaume huyo anaweza kuwa kashaoa tayari hivyo basi mwanamke anakubali kufunga ndoa hali anampenda zaidi yule mwanaume ambaye tayari yupo kwenye ndoa au kwasababu fulani hawezi kumwoa.
Nimekuelewa sanaaa
 
Unamuacha mke wa ndoa kwa kua alikusaliti ila unaenda kuoa mke alieachwa kwa kosa la kusaliti mapenzi bwana
 
Kusalitiwa kunaumiza kuliko kitu chochote. Achague kitu kimoja kati ya hivi
1.talaka
2.kumvumilia
3.kumrudia Mungu wake (awekeze muda wake katika ibada badala ya kumuwaza huyo pasua kichwa)
4.kumpuuza/kutomfatilia kabisa katika hilo
5.yeye pia achepuke
Akishindwa yote hayo,ajiandae kufa kwa presha maana wasiwasi wa mapenzi unaua.
Anaekupiga ngumi ya sikio na wewe mpige ya jicho....akikuuliza unaonaje na wewe mjibu unajisikije
 
Back
Top Bottom