Ndoa ina changamoto zisizoisha

Ndoa ina changamoto zisizoisha

Ishoo

Senior Member
Joined
May 18, 2017
Posts
110
Reaction score
73
Story ya ndugu yangu

Nimeolewa na huyu mwanaume miaka 5 iliyopita,wakati wote huo sikugundua kama ananisaliti.

Nakumbuka ilikuwa mwezi wa pili 2017, mume wangu aliposafiri kuelekea kijijini kwao, alikaa huko kwa muda wa wiki tatu, baada ya kurejea nilibaini kama huko alipata mchepuko, nilimuuliza kwa wema, akakubali na akaomba msamaha, yakaisha.

Lakini baadae nikagundua tena ana mchepuko mwingine kazini kwake, nikamuuliza alibisha sana, nikasema Mungu yupo na atamuumbua. Baada ya muda tena ndo nikayabaini mawasiliano yake na Huyo mwanamke anayefanya nae kazi, (pia huyo dada ni mke wa mtu) baada ya kumuuliza akakiri kosa.

Kinachoniumiza ni leo tena nimegundua bado anawasiliana na Huyo mwanamke, baada ya kumuuliza kanijia juu eti bora ndoa ivunjike.

Please great thinkers nisaidieni ushauri kwa huyu ndugu yangu. Kumbuka ana watoto 3 na ni mjamzito. Pia huyu mwanamke ni mfanyakazi wa serikali, mume pia ni mfanyakazi.

Wakiachana watoto itakuwaje?
Na wanafanya kazi sehemu moja, kisaikolojia athari zake ni zipi? Kwa watoto na wenyewe wahusika
 
Yani ndg yako hajui kama watoto wanaweza kulelewa hata kama baba na mama wametengana?!
Nadhani ,hicho ndo kinachofanya aendelee kumng'ang'ania huyo mume
 
Pole dada yangu siku nyingine jifunze kutofatilia mawasiliano ya mwanaume. Wewe ndio bora kuliko mchepuko na kama anajali familia wewe tulia tu.Hakuna mwanaume asiye na mchepuko
Asante,kinachomuuma yeye anadai hajawahi chepuka,ila Mr daily yupo na mchepuko,tena wake za watu
 
Amuulize kitu anachokosa kwa mkewe (maana yawezekana ananyimwa au hapati share kwa 100% maana baadhi ya wanawake ni wachoyo na wazembe kitandani utadhani umelala na maiti) ili mkewe ampatie ipasavyo.
 
Mwanaume wa aina hiyo huwa ni tabia na huwa hawabadiliki, muhimu ndugu yako atafute njia sahihi ya kuendesha maisha yake na watoto wake kuepusha kutengeneza yatima kwa kuletewa maradhi ndani ya nyumba.
 
Back
Top Bottom