Ndoa imenizawadia kiharusi

Ndoa imenizawadia kiharusi

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,946
Reaction score
38,656
Great Thinkers,

Kama heading inavyojieleza; mimi Msanii nimeoa na pia tumejaliwa watoto 2. Ninawapenda sana hawa watoto. Naamini ni zao la ndoa yetu.

Wengi wanaonifahamu, wanajua mapito ninayoyapitia kwenye hii ndoa. I tried so hard to humble myself na kuwa kiongozi wa familia kwa kutotumia misuli ya mwili dhidi ya matumizi ya akili kwenye hii ndoa.

Kwanza kabisa, naomba ku-declare my position kwamba, matendo au matukio ya mwanamke mmoja au mwanaume mmoja siyo justification ya tabia za jumla kwa wanawake ama wanaume wote.

Kikubwa ni kwamba nawaasa vijana wanaotaka kuingia kwenye mahusiano ya ndoa, wajitahidi kutafuta wenza wanaoendana nao. Usisite kuachana na toxic relationship. Ni bora usieleweke na jamii lakini ukaelewa kile unachokifanya kwa manufaa ya nafsi yako. Bahati mbaya sana tumezitosa mila na tamaduni zetu tumezipiga chini kwa ujumla wake. Badala ya kuchagua desturi nzuri na kuachana nazo zile mbovu.

Ndoa yangu haipo katika good shape. Mitikisiko ninayokumbana nayo imenipatia stress na sasa ninaishi kwa Neema za Mungu baada ya kupigwa stroke (kiharusi). Bado ni mwanaume kamili lakini nimejirudi ktk abstaining lane kwa sababu kwa sasa nailinda sana nafsi yangu over tamaa za mwili. Mwaka wa nne sasa nimemuweka mbali shemeji na wifi yenu. Sijaachana naye lakini nina amani yupo mbali kwa sasa.

Niliamua kuwa mkimya kwa muda mrefu sana, Namshukuru binafsi rafiki yangu Dr. Mariposa kunichomoa mafichoni.

For the sake of humility and a long, healthy life, ni busara ndoa zikaangaliwa kwa pande mbili. Moja as perfect intimacy na mbili as disaster against humanity. Ukipata mwenza sahihi, heaven itahamia chini ya dari lenu. Ukikosea kupata mwenza sahihi hakika kuzimu itawafurahia sana na itajidhihirisha kwenu.

Msanii wa JF
 
Wanawake wana changamoto sana. sio walioko kwenye ndoa wala michepuko ama GF's

kwangu huyu mshangaz ananipa stress sana.

anakuja kutaka sex pale anapojickia, hata mara moja kwa miezi mitatu kmmke😅😅😅

Screenshot_20250817-110450.jpg
👇👇👇
 
Pole sana mkuu.
Changamoto za ndoa huwa kubwa zaidi pale unapokuwa na watoto.
Ni vipi utawaacha watoto wawe na mzazi mmoja baba au mama , hii kidogo ina leta shida.

Kama wanaume tunapaswa kujua wenzetu ni dhaufu kwa baadhi ya mambo hivyo tunapo lalamika matokeo ya udhaifu wao sisi nasintuna hesabiwa dhaifu pamoja nao.

Kumkimbia mwanamke kisa ana changamoto hizi na zile ni udhaifu, kuathirika kwa sababu ya changamoto za mwanamke ni udhaifu.
 
Mkuu pole sana! Haya mambo wanasema yasikie kwa mwingine! Mimi binafsi namshukuru Mungu mambo yanaenda,mimi Mnyakyusa huyu wangu Muhaya,mwanzoni mwanzoni alileta za nshomile,nikampiga matukio mawili matakatifu akatulia...saiz adabu ipo tunasonga yuko very submissive
 
Back
Top Bottom