Top gun maverick
JF-Expert Member
- Dec 10, 2017
- 2,092
- 2,922
Habari wakuu ndo nimetoka ofisi za Tcu pale kivukoni mkabala na ikulu cha ajabu nimewakuta wanafunzi wengi wa multiple admission na ilipofika zamu yangu kuwaeleza nimechaguliwa vyuo viwili but sijatumiwa code number wakadai kwamba eti washatuma kwa watu wote hivyo sisi labda tutakuwa tumekuwa tumekosea namba ya simu. Aisee kajasho kembamba kalinitoka japo ilikuwa asubuhi mvua inanyesha.ikabidi sasa nitumie techniques za kuwatishia kwamba nitaandika barua kwa waziri wa elimu kuhusu kunyimwa haki ya msingi ya elimu ya juu .ndipo wakatoa form na tukapewa kujaza form six index number, na namba ya simu wakatuambia tuendelee kusubiri...