Mali za Lowassa hazisemwi kama alivyokuwa Mubarak madarakani penginehuelewi nafasi ya Lowassa ndani ya chama kulingana na mjadala huu, nimeyasema mengi sana. Kama EL ataondolewa madarakani kabisa, na hakubaliki na wananchi kama Mubarak mali zake zitakuja julikana wala sii zake tu na wenigine wote waliokuwa chini yake ama pamoja naye - Lowassa hajaondoka bado.Mkuu. Hakuna mahali mimi nimezungumzia ukali wa Lowassa au kufaa kwake bali hoja yangu imejikita kwenye ulinganisho wa uwiano. Kama Mubarak mali zake zimejulikana hatimaye kutaifishwa kwa nini kila siku tunaambiwa kwamba Lowassa ni tajiri wa kutupa wakati wanaosema hivyo hawajawahi kutuambia kwamba Lowassa ANAMILIKI nini. Mara zote mimi hupenda kujitenga na USHABIKI.
Kwenye siasa kufaa na kushinda UCHAGUZI ni vitu viwili tofauti. Wakati kushinda uchaguzi ni mikakati ya kikampeni na uzowefu wa kuratibisha minyukano ya kisiasa kuweza ni ubora miongoni mwa wanaoomba kuchaguliwa kuwa viongozi. Kama Ufisadi wa Lowassa umejikita kwenye kufikirishwa na wanasiasa wenzake ambao wengi wao ni maadui zake, mimi nitaendelea kuwa TOMASO ili niupate UKWELI.
Sikuwahi kumuunga mkono Lowassa na wala sina haja ya kufanya hivyo lakini najua athari za kuachia watu wengine washambuliwe bila ya wanaotoa mashambulizi kutakiwa kutoa ushahidi. Hata pale Mwembe Yanga Slaa alimtaja Lowassa kuwa fisadi kwa kufanya maamuzi yaliyoligharimu taifa lakini si kwa kukwapua mali za umma.
Kuna kisa hiki ambacho nimekibadili kifae kwa mazingira ya kwetu Tanzania. Kulikuwa na wamakonde, wachaga, wahaya, wanyakyusa na Wahadzabe wametekwa na majambazi. Wale majambazi wakaita "Wahaya tokeni mbele' Wahaya wakatoka na kuuawa mbele ya wenzao, waliendelea kuitwa hivyo mpaka ilipofika zamu ya kundi la Mwisho , jambazi mmoja akasema, "hao waue hapo hapo" wale mateka wakasema "sisi ni wamakonde msituue" na wao pia WAKAUAWA!!
Wanajamvi, bila shaka lolote kila binadamu hupenda madaraka, hupenda sifa na hupenda mali na kama yupo binadamu ambaye hapendi hivyo vitu, huyo hajaumbika nikiwa na maana ana mapungufu fulani. Kinachotutofautisha ni msukumo na kiwango cha tamaa kilicho nyuma ya jitihada zetu katika kuvitafuta. Tamaa ya wastani ni kitu kizuri kwani haitoi nafasi kwa tabia za ulafi, udanganyifu, wizi na hujuma. Lakini tamaa inapovuka mpaka, then hell breaks loose, na vyama kama CCM hugeuka na kuwa kama shamba la kuotesha na kukuza mafisadi kama Lowassa.
Edward Lowassa ni mfano tosha wa mavuno halisi kutoka shamba hilo la CCM lakini tofauti kati yake na makada wengine ni kwamba anawajibika. Aliwajibika kama Waziri Mkuu kwa kujiuzulu ili kuisetiri serikali ya CCM pamoja na Kiongozi wake mkuu, Raisi Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa hekima fisadi msaidizi ilibidi ajiuzulu ili fisadi mkuu abaki madarakani kumlinda yeye na mafisadi wengine ndani ya chama na serikalini. Hata hivyo yanayotokea sasa ni uthibitisho tosha kuwa ushirika katika maovu hauwezi kudumu milele na ni swala la muda tu kukuru kakara huanza.
Washiriki wote katika kuisetiri serikali pole pole wanaaza kuvuna walichopanda tukianza na Mwakyembe, Sitta, na Kikwete mwenyewe. Nyumba (CCM) inayowasetiri imeanza kuungua moto na taratibu moshi wake umewaathiri wote wanaoishi humo kiasi wanashindwa hata kuonana. Lengo langu hapa si kumtetea Fisadi Lowassa, la hasha, kwangu adui mkubwa wa taifa letu si mtu moja bali ni zimwi CCM. Ndani ya CCM naamini hakuna aliye safi hata moja lakini kama ni kumla nguruwe, hakuna aliyenona kama Edward Ngoyai Lowassa, mbunge wa Monduli.
Mimi, tofauti na wengi, naamini EL pamoja na madhambi yake yote, katika kujiuzulu Uwaziri Mkuu alitumia busara. Nampongeza kwa tendo lake hilo, likifuatiwa na la juzi la kukataa kujiuzulu CCM na kumhusisha Raisi katika sakata la Richmond, jambo ambalo limezidi kuiumbua CCM na kuiacha uchi. Wakati wa Richmond kuna watu kama Hosea tulitegemea wangejiuzulu lakini hawakufanya hivyo na leo kuna watu kama Luhanjo tulitegemea watajiuzulu mara moja lakini bado wapo tu ! Tusidanganyane, Kikwete hakuwa na ujasiri wa kumfukuza Lowassa.
Karibuni mtakaodai na mimi Mag3 niko kwenye payroll ya Lowassa, hilo halinipi taabu hata kidogo, siwezi kumzuia yeyote kufikiria hivyo. Ukweli ni kuwa kama Raisi 2015 atatoka CCM (na hilo Mungu atupishilie mbali !), basi ndani ya hiki Chama cha Mafisadi, kwa sasa hakuna kama Lowassa kama taifa linataka kujinasua kwenye dimbwi la utawala legelege uliojaa usanii. Uwajibikaji, uvumilivu na ujasiri aliouonyesha ni dalili nzuri katika Uongozi kama hraisiazitasukumwa na ulafi na tamaa, vitu ambavyo hata hivyo vimemganda kama kupe na kumwandama kama kivu
Huna jipya, ufisadi ndiyo wimbo wa taifa siku hizi. Watu hawana kazi ya kufanya kutwa kumwandama Lowassa. Sasa subiri awe Rais ndiyo utajua hicho unachoongea uko nje ya mstari.
Kigarama una akili sana! Karibu kwenye kambi yetu ya Lowassa!
Mfano wa Sigara hauhusiani kabisa na Ufisadi hata kidogo. Ufisadi unaweza fanywa na baba watoto wasiwe mafisadi, unaweza fanywa na ndugu mmoja wengine wakawa wazuri hii ni hulka ya mtu - period.Mkuu Pasco, wengi tu wameshindwa kuelewa lengo la mada lakini taratibu tutajaribu kuwaelewesha. Wavuta sigara huathirika afya zao kwa kiwango fulani lakini wanaoshinda nao wakiuvuta huo moshi imegundulika huathirika zaidi... dawa ni kukaa mbali na huyo mvuta sigara. Fisadi aliyekubuhu hatufai lakini huyo anayeshinda na fisadi, anaishi nyumba moja na fisadi, anakaa meza moja na fisadi, anakula na fisadi, anacheza na fisadi, anashirikiana na fisadi ...yaani hakai mbali na fisadii lakini analalamikia ufisadi...huyu ni mnafiki na hatari kuliko hata huyo fisadi. Dr. Shein kaishi nao miaka yoote hiyo akifaidi matunda ya ufisadi bila kulalama, leo eti anatufaa, ya Rabi !
Ndani ya CCM hakuna mwenye heri, period.
......... Tatizo lenu mnafikiri kwamba hata fisadi anaweza kuacha Ufisadi akilishwa zaidi..Hapo ndipo mnapokosea toka lini ikawa hivyo na hamna hata mfano mmoja wa fisadi aliyewahi kuwa fisadi akaacha Ufisadi kwa sababu kapewa nafasi ya kuongoza..Magereza yasizinge jengwa!.
Haiwezi kwisha mkuu wangu kwa sababu matatizo ni sisi wananchi kama alivyosema Mag3. Na matatizo haya tunayaona kwa mifano hapa hapa JF, watu wanazungumzia biashara za kimachinga kwa maana tunashindwa kufikiria nje ya hapo.. ndio maana hadi leo hatuwezi hata kutengeneza sindano ya kushonea wakati nasikia Ethiopia leo wanatengeneza magari na umeme wa kumwaga.Well said, Mkandara. Sina cha kuongeza hapo.
Labda tu niulize recycling Tz itakwisha kweli kama mambo yenyewe ndo hivi?
Mkuu "medula oblangata" zaidi ya EL ziko nyingi tu, sema haziko kwenye hizo cycles za kisiasa...Zing said:Utadhani bongo zetu zimekuwa cloned kwamba Bila medula oblangata ya Eddo magogni basi UFASADI hautaisha
@fairpayer Nguvu za lowasa na heshima ni za kisanii.
Sio sababu Lowasa anapata covarage kubwa kwenye Vyomb vya habari basi udhani ndiyo heshima au ni PM bora Kuliko hata Pinda Baba hata kama anaheshimikaa vipi watoto wakijua baba yao ni mwizi ni tatizo no matter hata awe mkali vipi.............
Nakupa mfano katika zira moja akiwa PM kama kawa Lowasa kutaka misifa alimuaibisha DC mmoja mbele ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara. Yule Dc alikaa kimya lakini nyuma ya pazia alimwambia Kwa mwendo huu hutafika mbali.( Na kweli baadae yaatokea )
Na kitu alichokuwa anamuabishia DC kilikuwa kwenye madesk Ofisi za waziri Mkuu Lakini sababu ya kupenda ubabe na kutaka sifa DC akatolewa kafara.
Hivi Kiongzi bora mchapakazi, anayetaka heshima ndio mpaka amfokee DC au RC mbele ya wannchi . Ndio style ya Lowasa ya kuwadangaya watu. Then cha ajabu mtu amemuabisha lakini anarudi magogoni anashindwa hata kumuamisha au kufukuza kazi Bado huyo unamuita mchapakazi. Hizo ndio danganya toto za Eddo........
So elewa uchapakazi na misifa ya Lowasa yanataokana na yeye kupenda au hata kuteka atention ya media. Uchapakazi wa lowasa hauna uhusiao na uchpakazi wa kweli wa kiongozi. Sumaye ni bora kuliko Lowasa tofauti mmoja hapigi kelele na hana magazeti na mwingine ni mipiga kelele na ana magazeti
Mkuu I hope na naomba sana isiwe kwamba mnamfagilia huyu jamaa kwa malengo fulani maana katika cycles za viongozi hakuwepo aliingia kwa nguvu na Ufisadi mkubwa dhidi ya wale aliowakuta. Kajipandisha cheo kama Hitler au Idd Amin na mtu kama huyu lazima tumwogope sana halafu wala msifikirie kwamba JK leo anaongoza nchi bila Lowassa..Mkuu "medula oblangata" zaidi ya EL ziko nyingi tu, sema haziko kwenye hizo cycles za kisiasa...
Cha kwanza kwenye cycles hizo ni majina yenye influence kwenye siasa, pamoja na watu wao wa karibu ndugu jamaa na marafiki etc, then pesa...
Simply as that, hata ukielezea kwa namna gani, this is the bottom line...Kwamba tutawapata viongozi kutokana na cycles za kisiasa...
Na hivyo si kweli kwamba EL ndo ameonekana kuwa anafaa kati ya wenye "medula oblangata"
Bali tunamzungumzia yeye kwa kuwa yuko kwenye hizo cycles zinazo determine ama kutoa viongozi wakuu wa nchi...
Kwa kifupi yuko kwenye tabaka la watawala...
True, on the other hand, kama ukiwa upande wa EL ninaamini ni sawa na kuwa upande wa JK na ukiwa upande wa JK ni sawa na kuwa upande wa EL, hilo wengi hawalioni.Mkuu I hope na naomba sana isiwe kwamba mnamfagilia huyu jamaa kwa malengo fulani maana katika cycles za viongozi hakuwepo aliingia kwa nguvu na Ufisadi mkubwa dhidi ya wale aliowakuta. Kajipandisha cheo kama Hitler au Idd Amin na mtu kama huyu lazima tumwogope sana halafu wala msifikirie kwamba JK leo anaongoza nchi bila Lowassa..
Lowassa yupo na amejaa tele kama pishi la mchele...hivyo, matokeo yote mnayoyaona leo yanatokana na kuwepo kwake kwa sababu wapo viongozi wengi wanashindwa kuifanya kazi yao kwa sababu yake. Mwinri, Mama Ana Tibaijuka, Magufuli ni miongozi mwa wachache wanajaribu kutoa ushawishi wa maana lakini wamefikia mahala wanakwenda na upepo tu.
Huko Ikulu na Usalama ndio usiseme aidha uko na Lowassa au kinyume ndio utanafsirika umesimama wapi na hakuna upande wa JK..Ni siasa ambazo zipo bungeni hadi NEC CCM wenyewe makundi ndani ya chama ni ya Lowassa na wapinzani wake..JK haonekani ni hakimu aliyepigwa Kipapai.
Mkuu Mkandara, Sitta hafai kabisa kuwa rais wetu!, kosa lake ni moja tuu, anapenda ukuu na kupenda makuu!, Sitta sio humble, anapenda utukufu, hata akilivaa lile joho, unamuona kabisa ni mtu anayejisikia!. Ili kuukwaa tuu uspika, akabadili gari, S Class 500 ili aifanane na ya rais, akaomba nyumba yenye hadhi, serikali ikampangishia kwa kodi ya US $ 8,000 per month!. Ametumia sikumbuki kiasi gani kuikarabati ile ofisi yake ya ubunge pale urambo ili ifananie na hadhi yake!.
Achilia ufisadi wake mdogo mdogo kama kununua ointment ya ngozi toka duka la dawa la aliyemuoa binti yake, for more than 2m bila prescription, na maitainance ya nyumba ndogo kwa magari na feha za umma!.
Udhaifu mkubwa wa Sitta ni pale alipo bow to pressure, ya kukubali kumtoa EL kafara ya richmond, wakati yeye kama speaker, anaujua ukweli halisi, alitakiwa kuitumia hiyo opportunity kumu impeach jamaa na yeye ndiye angekuwa shujaa wa kweli!.
Hatuwataki kabisa viongozi waoga kama kunguru, Sitta na kenge lake wanaojiita makamanda wa vita dhidi ya ufisadi, baada ya kupata fununu wanaweza kutemwa, waka devise safe heaven ya CCJ wakijiaminisha itasajiliwa as if hawaijui system ya nchi hii ilioachwa na nyerere, mpaka mkeo anaweza kuwa ndiye informer dhidi yako kule kwenye ile ofisi yao!. Masikini Mpendazoe akajitoa mhanga akijiita shujaa na humu JF wanachama wenzetu mashuhuri waka join the team ya CCJ!. Dekio Tendwa akaambiwa usiisajili CCJ! Sitta akapiga magoti CCM!.
Ni Sitta huyu huyu aliopata uspika kwa fedha za RA baada ya kumuadhibu EL, RA alijiapisha kumuadabisha, baada ya jitihada za kumny'angany'a kadi ya CCM kuzuiliwa na JK kama fadhila ya kumuokoa na impeachment, RA akamfix kwenye uspika. Hata huo uwaziri amepewa tuu kwenye ile formular ya keep closer to your friends but closer to your enemies!. Kwenye CCM Sitta hana chake!.
Ila pia mkuu Mkandara, kwenye mukhtadha wa kumtetea Lowassa kama mgombea` ajaye wa CCM, Sitta hatufai kama pacemaker, anaweza kugeuza kibao na kuwa contender, hivyo tunsumfagilie kabisa!. Subiri uchaguzi mkuu wa ndani ya CCM mwakani, hadi Nape atapigwa paranja, EL atasafishwa, atarejeshwa CC na 2015 ndiye mgombea!.
Lakini mbona mnamsema Sitta kwa ushahidi ambao hamuukubali kwa Lowassa?.. Siita hafai lakini kwa uchache wake ni bora kuliko Lowassa yaani Lowassa hana mfano CCM hata mdogo na tunaendelea kuishi ktk zama zake. Hivi jamani mmewahi kujiuliza kwa nini wazungu wanatengeneza vicatoon vya kina Batman, The Incredible Hulk, The Magnificent seven na kadhalika kama sii kusisitiza kizazi chao kiwe na Ujasiri wa kupambana na Ufisadi wakati hawa ni mabepari..Sasa leo sisi badala ya kujifunza na catoon ama sinema hizi kumbe tunaenda kutazama kama intertainment na kurudi nyumbani tukisimuliana jinsi Jambazi lilivyowasumbua..ongezea na
1. scandal zake za ustawishaji makao makuu
2. scandal zake za Kituo cha uwekezaji cha Taifa
Sitta hafai kabisaaa.......
.............Siwezi kumlinganisha Lowassa na Kigoda, Sumaye, .......... Mramba na wengine wengi tu ambao wanaweza kabisa kushika nafasi ya mgombea wa CCM mbele ya Lowassa tukiachukulia mwenye nafuu..Huyu Lowassa hafai yaani hata kwa kufikiria isipokuwa anapigiwa debe sana kwa sababu...na sitaki sana kurudia hili neno jamani mbona mnataka kuniweka maneno mdomoni ambayo mtakuja nichukia mimi badala yake..
Hata hivyo binafsi leo nasema Dr. Shein, .........Mwanri, Membe, Mwinyi, na kuna wanawake wengi sana CCM wakitumikia wizara ya Sheria, Fedha na hazina wanaweza kabisa kuchukua nafasi ya mgombea wa chama CCM na hawa wote ni bora kuliko Lowassa, .. .............
Mkandara kaka yangu. Mbona ya Richmond umeshaambiwa kwenye NEC ya CCM? Yaani ukweli unaujua lakini umeamua kuupindisha?
Richmond Lowassa alikua bangusilo!
Mkuu Nyunyu, usiwe na wasiwasi na Lowassa, wala usitafute uhakika wowote kuhusu uwezo wake.
Naomba nikupe kisa kidogo tuu cha kweli,
Hivi unajua kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar, walioishi mji Mkongwe ni Waarabu tupu?. Hivi unataarifa wengi wa machotara wa kiarabu kabla ya mapinduzi matukufu, walizaliwa na wajakazi wa kike waliokuwa wakifanya kazi za ndani kwa waarabu?. Wajakazi hao au waliridhia, au walibakwa ndipo mixed blood ilivyoanza?.
Ni baada ya mapinduzi yale, ndipo wanaume wa kiarabu wa mji mkongwe waliuwawa na wamatumbi kujitwalia wake zao na binti zao!. Sasa ili wazawa wajiridhishe Zanzibar ni yao, Abedi Karume aliongoza na kusimamia ujenzi wa yale maghorofa ya Michenzani na waswahili wenzangu na mimi ndio nao kwa mara ya kwanza, wakakaa ghorofani!.
Sasa unajua baada ya kifo cha Karume, nini kilifuatia yale ambayo hayakukamilika?!. Huwezi kuamini, serikali ya ASP na serikali ya CCM ziliabandon kila kitu!. Walitelekeza kila jema la Karume!.
Hiki ndicho serikali ya CCM ilichokifanya kwa kuabandon mazuri yote ya Lowassa. Hili la shule za kata, kujenga na kuongeza idadi ya walimu ndio ilikuwa hatua ya kwanza. Hatua ya pili ilikuwa ni kuongeza vifaa, vitabu vya ziada na kiada, vifaa vya maabara, na kuhakikisha kila mtoto wa shule anakaa kwenye kiti.
Hatua nyingine ilikuwa mni kila shule kutoa chakula bure, alianzia kwa kutoa agizo, shule zote zinazozunguka ranchi za taifa, zipewe maziwa bure!.
Mpango wa Lowassa ni kuwa kila mwanafunzi anayemaliza primary lazima aende sekondari na hatimaye chuo kikuu na elimu yote ingekuwa bure toka shule za vidudu mpaka chuo kikuu!. Baada ya kutemwa serikali ya CCM ilitelekeza mipango yote hii!.
Nakuhakikishia, kama Lowassa angekuwepo, hali ya nchi yetu isingekuwa kama hivi tulivyo sasa!.
Nawashauri wapenda mabadiliko ya kweli wote, tupiganie mgombea wa CCM awe ni Edward Lowassa!.
Unajua watu wasauhaulifu sana na nadhani hili ni tatizo la Wadanganyika.. Inabidi tukapimwe vichwa vyetu maana ni huyu huyu Lowassa akiwa madarakani tuliona Karamagi akichukua bandari TICKS, Mzee Kigunge akichukua vituo vya Mabus na Parking, mashirika ya simu na TV yalokuwa na bei nafuu kwa wananchi yakipigwa vita hadi yakafilisiwa na kuzaliwa kwa Voda ambayo contract zake zote ni za serikali ya Lowassa, EPA, Buzwagi, Banki kuu Mama Meghji akitoa mabillioni na kutetea bungeni mwisho wake mabangusilo Balali, Msabah, Diallo na Karamagi aliyeweka mkataba akiwa London wakajiuzulu.. hivi kweli hawa wote ni heroes kwa kujizulu mbona hawasemwi ila Lowassa!... Likaundwa baraza jipya la mawaziri yote kutokana na kushindwa kwa waziri mkuu kuongoza njia inayotakiwa, leo bado watu wanamfikiria Lowassa...Ama kweli kama hutastaajabu ya Mussa ya Firaun kiboko..a Big NO.....Lowassa hakuwa bangusilo Richmond (hiyo ni picha anayojitahidi kui-paint).............JK hakumuambia Lowassa apindishe ushauri wa Tanesco FYI.....huo ulikuwa ni ushauri wa EL kwa JK..........
Hii mada imekuwa ngumu kwa wengi na kweli inaonyesha dhahiri mindset ya typical Mtanganyika, yaani inanikumbusha viongozi wetu wa leo wanavyokurupuka na kusign mikataba bila ya ku"read between the lines" na mwisho wake mavuno ni mikataba mibovu. Ng'wanangwa kabla sijaendelea hebu chukua time umsome JokaKuu kama ninavyomnukuu hapa chini;
Ng'wanangwa, naamini kuna wachache ambao wameweza kunielewa na inaonekana wewe definitely si moja kati ya watu hao. Upende usipende the most influential but controversial figure ndani ya CCM kwa hivi sasa ni Edward Ngoyai Lowassa. Ni Lowassa tu ameweza kuwa na jeuri ya kumnyooshea kidole Raisi wa nchi katika kikao rasmi cha chama anachokiongoza na asichukuliwe hatua yoyote.
Ndani ya CCM kuna makundi mawili makubwa kundi moja likimuunga mkono Lowassa na kundi lingine likimpinga Lowassa lakini ukweli ni kuwa Mwenyekiti wa Chama hana ujasiri wa kuonyesha yuko upande gani. Mimi sijawahi kuwa mwanachama wala shabiki wa hiki chama cha mafisadi na kama kuna kitu nakiombea kila siku nikiamka ni hiki chama cha wezi kusambaratika.
Swali linaloumiza vichwa vya wengi kama mimi ni namna chama hiki cha CCM, adui mkubwa wa taifa, kinavyoweza kusambaratishwa na kufa bila umwagaji damu. Hapo ndipo wazo likanijia kuwa labda njia nzuri zaidi ya kufikia lengo hilo ni kuutumia huo udhaifu uliokiandama CCM kama turufu ya kukisambaratisha. Wapenzi wa Lowassa wamejipanga kikweli kweli na, asikudanganye mtu, nguvu anayo, pesa anayo na mtandao anao.
Hapo ndipo linakuja jibu kutoka kwa JokaKuu kwamba asiyemtaka Lowassa ndani ya CCM ahame chama ! na mimi nachojaribu ni kuwaua ndege wawili kwa jiwe moja. Wakati CCM wakikwaruzana kuhusu Lowassa, kwenye hiyo njia kuelekea miaka hamsini zaidi CCM wanazodai wataendelea kuitawala Tanzania, sisi (macatalyst !) tunazidi kuiwekea miiba.
Hakuna, na narudia kusema hakuna mtu ndani ya CCM ambaye ni afadhali kuwa Raisi wa Tanzania ( ingawa wengi wananisoma visivyo) kwani woote ama wameoza au wanaunga mkono uozo. Ninachosema na ambacho siombei msamaha ni kuwa kwenye huo uozo kama itakuwa lazima Raisi atoke humo, basi afadhali Edward Ngoyai Lowassa.
Kwa nini nasema hivyo ? Ni yeye aliweza kuvunja ile miiko ya kijinga ya nidhamu ndani ya chama ambayo imekuwa ikitumiwa kulindana kwa kumsifia mfalme alivyoweka madudu kumbe yuko uchi ! Lowassa alionyesha njia kwa kumkumbusha mfalme kuwa ajisetiri hata kwa kipande cha kanga kwani
wakati mwingine, kwa wanafiki, ushangiliaji unaweza njia ya kuficha dhihaka.
Nje ya CCM mbona watu wako wengi tu ambao wanaweza kuliongoza hili taifa ! Kwa nini kiongozi wa nchi hii atoke CCM, chama ovu ambacho kimepoteza dira na kupiga kambi kwenye dimbwi la rushwa, ufisadi, ulafi, uhuni n.k. Go Edward go, usipunguze mwendo, the country needs you ! Sasa Ng'wanangwa, there, uwanja wako, niite majina yoote unayofikiria.