Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Wanajamvi, bila shaka lolote kila binadamu hupenda madaraka, hupenda sifa na hupenda mali na kama yupo binadamu ambaye hapendi hivyo vitu, huyo hajaumbika nikiwa na maana ana mapungufu fulani. Kinachotutofautisha ni msukumo na kiwango cha tamaa kilicho nyuma ya jitihada zetu katika kuvitafuta. Tamaa ya wastani ni kitu kizuri kwani haitoi nafasi kwa tabia za ulafi, udanganyifu, wizi na hujuma. Lakini tamaa inapovuka mpaka, then hell breaks loose, na vyama kama CCM hugeuka na kuwa kama shamba la kuotesha na kukuza mafisadi kama Lowassa.
Edward Lowassa ni mfano tosha wa mavuno halisi kutoka shamba hilo la CCM lakini tofauti kati yake na makada wengine ni kwamba anawajibika. Aliwajibika kama Waziri Mkuu kwa kujiuzulu ili kuisetiri serikali ya CCM pamoja na Kiongozi wake mkuu, Raisi Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa hekima fisadi msaidizi ilibidi ajiuzulu ili fisadi mkuu abaki madarakani kumlinda yeye na mafisadi wengine ndani ya chama na serikalini. Hata hivyo yanayotokea sasa ni uthibitisho tosha kuwa ushirika katika maovu hauwezi kudumu milele na ni swala la muda tu kukuru kakara huanza.
Washiriki wote katika kuisetiri serikali pole pole wanaaza kuvuna walichopanda tukianza na Mwakyembe, Sitta, na Kikwete mwenyewe. Nyumba (CCM) inayowasetiri imeanza kuungua moto na taratibu moshi wake umewaathiri wote wanaoishi humo kiasi wanashindwa hata kuonana. Lengo langu hapa si kumtetea Fisadi Lowassa, la hasha, kwangu adui mkubwa wa taifa letu si mtu moja bali ni zimwi CCM. Ndani ya CCM naamini hakuna aliye safi hata moja lakini kama ni kumla nguruwe, hakuna aliyenona kama Edward Ngoyai Lowassa, mbunge wa Monduli.
Mimi, tofauti na wengi, naamini EL pamoja na madhambi yake yote, katika kujiuzulu Uwaziri Mkuu alitumia busara. Nampongeza kwa tendo lake hilo, likifuatiwa na la juzi la kukataa kujiuzulu CCM na kumhusisha Raisi katika sakata la Richmond, jambo ambalo limezidi kuiumbua CCM na kuiacha uchi. Wakati wa Richmond kuna watu kama Hosea tulitegemea wangejiuzulu lakini hawakufanya hivyo na leo kuna watu kama Luhanjo tulitegemea watajiuzulu mara moja lakini bado wapo tu ! Tusidanganyane, Kikwete hakuwa na ujasiri wa kumfukuza Lowassa.
Karibuni mtakaodai na mimi Mag3 niko kwenye payroll ya Lowassa, hilo halinipi taabu hata kidogo, siwezi kumzuia yeyote kufikiria hivyo. Ukweli ni kuwa kama Raisi 2015 atatoka CCM (na hilo Mungu atupishilie mbali !), basi ndani ya hiki Chama cha Mafisadi, kwa sasa hakuna kama Lowassa kama taifa linataka kujinasua kwenye dimbwi la utawala legelege uliojaa usanii. Uwajibikaji, uvumilivu na ujasiri aliouonyesha ni dalili nzuri katika Uongozi kama hazitasukumwa na ulafi na tamaa, vitu ambavyo hata hivyo vimemganda kama kupe na kumwandama kama kivuli chake !
Edward Lowassa ni mfano tosha wa mavuno halisi kutoka shamba hilo la CCM lakini tofauti kati yake na makada wengine ni kwamba anawajibika. Aliwajibika kama Waziri Mkuu kwa kujiuzulu ili kuisetiri serikali ya CCM pamoja na Kiongozi wake mkuu, Raisi Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa hekima fisadi msaidizi ilibidi ajiuzulu ili fisadi mkuu abaki madarakani kumlinda yeye na mafisadi wengine ndani ya chama na serikalini. Hata hivyo yanayotokea sasa ni uthibitisho tosha kuwa ushirika katika maovu hauwezi kudumu milele na ni swala la muda tu kukuru kakara huanza.
Washiriki wote katika kuisetiri serikali pole pole wanaaza kuvuna walichopanda tukianza na Mwakyembe, Sitta, na Kikwete mwenyewe. Nyumba (CCM) inayowasetiri imeanza kuungua moto na taratibu moshi wake umewaathiri wote wanaoishi humo kiasi wanashindwa hata kuonana. Lengo langu hapa si kumtetea Fisadi Lowassa, la hasha, kwangu adui mkubwa wa taifa letu si mtu moja bali ni zimwi CCM. Ndani ya CCM naamini hakuna aliye safi hata moja lakini kama ni kumla nguruwe, hakuna aliyenona kama Edward Ngoyai Lowassa, mbunge wa Monduli.
Mimi, tofauti na wengi, naamini EL pamoja na madhambi yake yote, katika kujiuzulu Uwaziri Mkuu alitumia busara. Nampongeza kwa tendo lake hilo, likifuatiwa na la juzi la kukataa kujiuzulu CCM na kumhusisha Raisi katika sakata la Richmond, jambo ambalo limezidi kuiumbua CCM na kuiacha uchi. Wakati wa Richmond kuna watu kama Hosea tulitegemea wangejiuzulu lakini hawakufanya hivyo na leo kuna watu kama Luhanjo tulitegemea watajiuzulu mara moja lakini bado wapo tu ! Tusidanganyane, Kikwete hakuwa na ujasiri wa kumfukuza Lowassa.
Karibuni mtakaodai na mimi Mag3 niko kwenye payroll ya Lowassa, hilo halinipi taabu hata kidogo, siwezi kumzuia yeyote kufikiria hivyo. Ukweli ni kuwa kama Raisi 2015 atatoka CCM (na hilo Mungu atupishilie mbali !), basi ndani ya hiki Chama cha Mafisadi, kwa sasa hakuna kama Lowassa kama taifa linataka kujinasua kwenye dimbwi la utawala legelege uliojaa usanii. Uwajibikaji, uvumilivu na ujasiri aliouonyesha ni dalili nzuri katika Uongozi kama hazitasukumwa na ulafi na tamaa, vitu ambavyo hata hivyo vimemganda kama kupe na kumwandama kama kivuli chake !