Ndivyo nilivyo .... Niko hivo....

Ndivyo nilivyo .... Niko hivo....

Thank you for being honest, you juc cementd trust kwa instings zangu...

Welcom a bottle of wine if u dont mind

Thanks, I have a glass of sweet red wine here we can tost. ....

Cheers... For being me...
 
Iko vizur sana nimekupenda japo skujiw,unafaaa kwa kila namna kuolewa nk, ktk maisha yng,ipo siku kama imepangwa.

Asanteee, nashukuru kwa pongezi. Ila maono yako umekosea Kasie ni bibi mtu mzima hayupo kwenye matarajio ya kuolewa. Nikutakie kheri wewe upate mke atayekufaa.
 
Hongera.

Kama uko hivyo haufati mkumbo kama vidada vya siku hizi unafaa.

Siku hizi wadada wanatisha sana siyo siri;

Ngozi bandia

Nywele bandia,

Kucha bandia,


Yani maisha ya siku hizi ni zaidi ya movie.

Hakuna watu wabaya kama wafanyabiashara. Mie nikienda kununua kitu huwa najiuliza mwenyewe na nikiridhika hakuna wa kunishawishi. Na akijiloga mwenye duka kujisogeza kunipamba na maneno matamu ya bidhaa yake kabla sijafanya maamuzi ya kuinunua bidhaa ile huwa naiacha na kwenda itafuta mahali pengine au kurudi siku ingine. Napenda nunua kitu kinachonifaa na nakitumia ipasavyo. Mfano hizi nywele za rangi ya gold nilisikia wataalam wa urembo wakisema hizi nywele zinawapendeza watu ambao weupe kidogo au maji ya kunde, sasa utafurahi na roho yako ukimkuta mdada katinga nywele hiyo halafu ni mweusi kama lupita nyong'o kisha kaweka rangi ya mdomo ya Pink iliyokoa mweeh siwasemi vibaya wadada laah, acha nibakie mshamba aiseeh.
 
Naweza nisiwe mrembo ila huwa napenda vitu visivokolea sana hata chumvi na mafuta kwenye chakula viwe kidogoo.

Si kuwa sipaki kabisa rangi za mwili na mdomo na wanja hapana, ila kama nimepaka basi huwezi kujua au nikaishia kupaka mafuta tuu mwili wote (nnayotumia siku zote) nikaongeza wanja wa chini ya macho na lipshine nimemaliza bila kusahau manukato ya upole.

Yeah I like that, upo vzr hongera
 
Kasinde, nenda hapo kwa Mangi kunywa tani yako nakuja kulipa. Yaani unakuta binti kajaliwa ngozi nyororo ya huu weusi unaong'ara halafu ameiharibu kwa mkorogo kisa naye awe kama wengine. Huwa nasikitika sana!
 
Hakuna watu wabaya kama wafanyabiashara. Mie nikienda kununua kitu huwa najiuliza mwenyewe na nikiridhika hakuna wa kunishawishi. Na akijiloga mwenye duka kujisogeza kunipamba na maneno matamu ya bidhaa yake kabla sijafanya maamuzi ya kuinunua bidhaa ile huwa naiacha na kwenda itafuta mahali pengine au kurudi siku ingine. Napenda nunua kitu kinachonifaa na nakitumia ipasavyo. Mfano hizi nywele za rangi ya gold nilisikia wataalam wa urembo wakisema hizi nywele zinawapendeza watu ambao weupe kidogo au maji ya kunde, sasa utafurahi na roho yako ukimkuta mdada katinga nywele hiyo halafu ni mweusi kama lupita nyong'o kisha kaweka rangi ya mdomo ya Pink iliyokoa mweeh siwasemi vibaya wadada laah, acha nibakie mshamba aiseeh.
Unakuta anakuwa kama kinyago[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Asante japo yaweza kuwa nna mapungufu vile vile ni kuwa niko hivyo sana mahei hei kuta tangu kuleee ugeuke kutizama yule anayekuja ni nani.

Definitely mkamilifu ni Muumba The almighty, so there has to some elements as u have said, though zinakuwa very minor as compared na mtu mwingine
 
Sipati picha speed na race ulotoka nayo hapo kanisani baada ya huyo mdada kukudistress [emoji593][emoji593]

Wala sikutoka speed ni kuwa nilimpa tabasamu la nyani lile wanaita monkey smile kisha nikamuaga nikaondoka sikutia neno zaidi maana sikutaka kupoteza upako nilioupata wa kutembea nao wiki nzima.
 
Kasinde katika ubora wakoo!!!
Embu niambiee ni nani huyo mama anayekuchezea akilii?
Mimi nimeridhika na wewe, yeye anakutakia nini??
I love u Kasie

hahahahah
kasie

Ibilisi acha uchokozi si kunichezea akili kiufupi wako wengi ambao wamekuwa wakiniona niko old fashion na nimekuwa nikiwaambia ndivyo nilivyo. Sasa huyu dada niliyekuja na nae leo kanisani najua yuko humu na huwa tunaonana kanisani sasa sikutaka aniondolee upako wangu ila kwa sasa nimepata wasaa wa kumfikishia ujumbe vizuri na najua atasoma hapa tuu ajue kuwa Kasie ndivyo alivyo.
 
Sasa Kasinde humu jf hatufahamian sasa huyo anayekucriticise anatoka wapi?
 
Ila wanawake mna vijimamboo?
si ungemalizana nae huko tu?
au umemwoneaa aibuu?/
Miss Natafuta njoo ujibu hizi tuhumaa, maana unaonekana ni wewe tu.

Sikuweza mwambia pale kwakuwa ni eneo la ibada na nalihesimu hata maongezi ya kanisani huwa siyaendekezi. Pia nilitaka kuwahi nyumbani kufanya mambo yangu na kiufupi nilimpuuzia muda ule kama yuko vizuri atagundua nilimlia kobisi zaidi ya kumpa monkey smile.

Ibilisi uache uchochezi sijataja jina la mtu hapa usinichonganoshe na watu zikiibuka ngumi upigane mwenyewe hehehee
 
Kabisaaa dada Kasie ..huwezi ukaishi kwa principle za watu wengine. Kufuata mkumbo ni dalili za kutojiamini.. Mwanamke mjanja anajiamini.
 
Back
Top Bottom