Ndio nimefika Musoma Mjini ila nimehuzunika sana

Kwanini mkoa wa Mara hauendelei bado upo nyuma kwenye swala la viwanda?

  • Kwa walio fika MSM ulivutiwa na nini?

  • Mpangilio wa mji

  • Style ya maisha na ukarimu wao


Results are only viewable after voting.

FOX21

JF-Expert Member
Oct 12, 2018
425
781
Ndugu zangu mnaoishi Musoma kwanza niwape pongezi kwa jinsi mnavyo pambana kupata mkate wenu wa kila siku.

Mkoa huu wa MARA japo una wakazi wengi wenye elimu ya sekondari na kuendelea ila nahuzunika kusema kundi kubwa la vijana wanahangaika mitaani kwa kukoswa ajira za kueleweka na kujikuta wanaishi kwenye mazingira magumu na hii inapelekea wengine kujihusisha na matukio ya kiuhalifu, kama kupora mali za watu na unyang'anyi.

Kwa hali kama hii ninapenda kuiomba serikali kulitizama kwa umakini sana ili kuiokoa jamii na matukio yasiofaa kama ubakaji na unyang'anyi. Maana tutaanza kusikia kuna makundi ya kihalifu kama miaka ya nyuma vijana walipokua na magenge ya uhalifu.

Ifikapo mida ya saa mbili za usiku, bado ni mapema sana ila huu muda usishangae kukutana na uporaji wa kutumia nguvu katika baadhi ya maeneo kama, Nyabange, Bweri, Majengo(songe), Baruti, Nyakato, Nyasho, nk. Inatakiwa jeshi la polisi liweke juhudi kutokomeza tabia za namna hii kwa Nguvu zote ili kuilinda heshima ya mkoa wa Mara. Naamini samaki hukujwa angali mbichi.

Nimefurahia ziara ya mkoani, japo maisha ya walio wengi ni changamoto.
 
Katika mji ambao sijawahi kuuelewa ni Musoma, mji umekata tamaa miaka yote kama uliwahi kwenda mwaka 2004 na ukatembea tembea ukirudi tena baada ya miaka 20 mwaka huu 2024 utakuta pako vile vile hakuna maendeleo ya maana mji haubadiliki
 
Katika mji ambao sijawahi kuuelewa ni Musoma, mji umekata tamaa miaka yote kama uliwahi kwenda mwaka 2004 na ukatembea tembea ukirudi tena baada ya miaka 20 mwaka huu 2024 utakuta pako vile vile hakuna maendeleo ya maana mji haubadiliki

Nenda sasa hivi kidogo lami pale mjini pamebadilika
 
Ndugu zangu mnaoishi Musoma kwanza niwape pongezi kwa jinsi mnavyo pambana kupata mkate wenu wa kila siku.

Mkoa huu wa MARA japo una wakazi wengi wenye elimu ya sekondari na kuendelea ila nahuzunika kusema kundi kubwa la vijana wanahangaika mitaani kwa kukoswa ajira za kueleweka na kujikuta wanaishi kwenye mazingira magumu na hii inapelekea wengine kujihusisha na matukio ya kiuhalifu, kama kupora mali za watu na unyang'anyi.

Kwa hali kama hii ninapenda kuiomba serikali kulitizama kwa umakini sana ili kuiokoa jamii na matukio yasiofaa kama ubakaji na unyang'anyi. Maana tutaanza kusikia kuna makundi ya kihalifu kama miaka ya nyuma vijana walipokua na magenge ya uhalifu.

Ifikapo mida ya saa mbili za usiku, bado ni mapema sana ila huu muda usishangae kukutana na uporaji wa kutumia nguvu katika baadhi ya maeneo kama, Nyabange, Bweri, Majengo(songe), Baruti, Nyakato, Nyasho, nk. Inatakiwa jeshi la polisi liweke juhudi kutokomeza tabia za namna hii kwa Nguvu zote ili kuilinda heshima ya mkoa wa Mara. Naamini samaki hukujwa angali mbichi.
Nimefurahia ziara ya mkoani, japo maisha ya walio wengi ni changamoto.
Hivi

Kama wenyeji hawataki ustaarabu na maendeleo…. Utailaumu serikali?
 
Nenda sasa hivi kidogo lami pale mjini pamebadilika
Nimeenda miaka miwili iliyopita ule mji haubadiliki mkuu, nikiwa mdogo niliwahi kwenda huko miaka ya 2006 lakini kupitia zilezile kumbukumbu zangu za utoto nilikua nakatiza mitaa na sioni jipya pako vile vile
 
Musoma inabadilika taratibu mnooooo hata wafanyabiashara ni wale wale hawaongezeki....namaanisha km ni mathayo, sjui kiondo, obeto ni walewale toka nimezaliwa
Kuna mfanyabiashara walikua wanamuita hussein sokoni naimani kabisa kama yuko hai bado ni yuleyule anawakimbiza
 
Ushawishi tu wa watu wa Bukoba. Kuanzia na wabunge, mawaziri nk.
Huoni Malinzi tu mkuu wa TFF alihakikisha Bukoba inapata uwanja wa kisasa wa mpira kaitaba siku hiz unasaport hadi mechi za usiku
Acha uongo, Bukoba ipo nyuma, unaongelea stendi ambayo hata stendi ipo tangu 2020.

Viwanja vya ndege kila mkoa vinajengwa kaangalie hapo Musoma uone ..
 
Back
Top Bottom