Ndesamburo aagwa kwa mara ya pili

Ndesamburo aagwa kwa mara ya pili

Gamba la Nyoka umeongea maneno ya maana sana. Una hekima.
 
Jamani chadema leo mlitakiwa muiachie familia na wasemaji wa familia.bado tu mnapora ya kwenu ya kisiasa na mabendera si mlifanya jana? Leo ilitakiwa kisiweko chochote cha kichama ili watu wasiopenda chadema na viongozi wa vyama mbali mbali na serikali wawe free kuhudhuria.

Sijapenda hili la SELASINI kuendelea kuwa msemaji.wapishe wazee wa ukoo au ndugu wa ndesamburo leo ndio washike usukani wa shughuli yao.

Jana mlisema chama kinaaga sasa na leo mumo tu mnakera.Familia ya ndesamburo mumeipora madaraka yote


utume akili ndugu yangu la sivyo taifa hili zitazidi kudidimia kama waeanzania wenyewe ndo wa akili kama za kwakop
 
Kwakweli apumzike pahala pema,nasisi tuliobaki tuwe na roho nzuri.tufate mazuri yake mzee wetu!
 
Pumzika kwa amani mwana mwema wa mama Tanganyika!
 
Jamani chadema leo mlitakiwa muiachie familia na wasemaji wa familia.bado tu mnapora ya kwenu ya kisiasa na mabendera si mlifanya jana? Leo ilitakiwa kisiweko chochote cha kichama ili watu wasiopenda chadema na viongozi wa vyama mbali mbali na serikali wawe free kuhudhuria.

Sijapenda hili la SELASINI kuendelea kuwa msemaji.wapishe wazee wa ukoo au ndugu wa ndesamburo leo ndio washike usukani wa shughuli yao.

Jana mlisema chama kinaaga sasa na leo mumo tu mnakera.Familia ya ndesamburo mumeipora madaraka yote
ndugu unapoona hali kama hiyo ujue kila kitu kimepangiliwa na sio matakwa ya chama. jaribu kuelewa pia sio kila kitu kitakwenda kama utakavyo wewe. ndio maana umeambiwa ni mwenyekiti wa kamati ya mazishi!
 
R.I.p muasisi na mfadhili wa chama mmbunge mstaafu ndesamburo
 
4f60dee83142819fd5324871e48a2e20.jpg

Wajukuu wa aliyekuwa mbunge wa Moshi Mjini Philimoni Ndesamburo,wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wake wakati wakilitoa nyumbani kwake Kiboroloni Kuelekea kanisani kwaajili ya Ibada ya Kumuaga.Picha na Diana Saria.

Kwa ufupi
Mwili wa Ndesamburo unaagwa kanisani leo kabla ya mazishi kufanyika nyumbani kwake baadaye mchana
Moshi. Mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo unaagwa kwa mara ya pili na wafuasi wa Chadema pamoja na wananchi ambao hawakupata nafasi ya kumuaga siku ya jana katika viwanja vya Majengo mjini Moshi.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mazishi, Joseph Selasini amewataka wananchi na watu wote waliohudhuria ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Usharika wa Kiborloni kuacha kupiga picha mwili wa marehemu ili kutunza heshima yake.

Viongozi mbalimbali wameendelea kuwasili katika kanisa hilo wakiwemo viongozi wa Chadema na Mbunge wa Singinda Kaskazini(CCM), Lazaro Nyalandu.

Awali wafuasi na wanachama wa Chadema walifurika nyumbani kwa Ndesamburo kwa ajili ya kuandamana kupelekwa mwili wake kanisani.

Mwili wa Ndesamburo umesaliwa nyumbani kwake kabla ya kupelekwa kanisani.
780050adcf9339d44680bd8a47aeba0a.jpg
099cb4019e599213529db0be7bb9509e.jpg

Chanzo: Mwananchi
Hapa ndo mahala ninapoukubali msimamo wa imani ya kiislam. Kuagaaga Mara mbilimbili ni kumsumbua marehem.
 
Back
Top Bottom