Ndesamburo aagwa kwa mara ya pili

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,720
55,859
4f60dee83142819fd5324871e48a2e20.jpg

Wajukuu wa aliyekuwa mbunge wa Moshi Mjini Philimoni Ndesamburo,wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wake wakati wakilitoa nyumbani kwake Kiboroloni Kuelekea kanisani kwaajili ya Ibada ya Kumuaga.Picha na Diana Saria.

Kwa ufupi
Mwili wa Ndesamburo unaagwa kanisani leo kabla ya mazishi kufanyika nyumbani kwake baadaye mchana
Moshi. Mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo unaagwa kwa mara ya pili na wafuasi wa Chadema pamoja na wananchi ambao hawakupata nafasi ya kumuaga siku ya jana katika viwanja vya Majengo mjini Moshi.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mazishi, Joseph Selasini amewataka wananchi na watu wote waliohudhuria ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Usharika wa Kiborloni kuacha kupiga picha mwili wa marehemu ili kutunza heshima yake.

Viongozi mbalimbali wameendelea kuwasili katika kanisa hilo wakiwemo viongozi wa Chadema na Mbunge wa Singinda Kaskazini(CCM), Lazaro Nyalandu.

Awali wafuasi na wanachama wa Chadema walifurika nyumbani kwa Ndesamburo kwa ajili ya kuandamana kupelekwa mwili wake kanisani.

Mwili wa Ndesamburo umesaliwa nyumbani kwake kabla ya kupelekwa kanisani.
780050adcf9339d44680bd8a47aeba0a.jpg
099cb4019e599213529db0be7bb9509e.jpg

Yanayojiri Moshi Kwenye Mazishi ya Mzee Ndesamburo
JUNE 6, 2017.
ndesamburo-1.png


MOSHI, KILIMANJARO: Viongozi wa CHADEMA pamoja na wananchi wakiwasili katika Usharika wa Kiboriloni kwa ajili ya ibada ya kumuombea aliyekuwa Mbunge wa Muda Mrefu wa Moshi Mjini na Muasisi wa chama marehemu Mzee Philemon Ndesamburo.

ndesamburo-2.png


Maandalizi kanisani hapo.

ndesamburo-3.png


Viongozi wa Chadema wakiwa wamejiandaa kuupokea mwili wa marehemu.

ndesamburo-4.png


Kaburi ambamo atazikwa mzee Ndesamburo.

ndesamburo-1-1.jpg

18921827_627192624140006_4009560877510862677_n.jpg

ndesamburo-2-1.jpg


ndesamburo-3.jpg


ndesamburo-4.jpg


ndesamburo-5.jpg


ndesamburo-6.jpg


ndesamburo-7.jpg


ndesamburo-8.jpg
19030485_627128254146443_3364723213717273336_n.jpg

Mbunge wa zamani na mfanyabiashara maarufu kutoka Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo amezikwa leo June 6, 2017 nyumbani kwake KDC Moshi huku mazishi yake yakihudhuriwa na mamia ya watu wakiwemo viongozi mbalimbali.
 
R. I. P mzee, nilikuwa mbokomu kule mwisho wa njia unapita shule ya secondary ,sikujua kama kamanda soon utatutoka
 
Umati huu unadhihirisha namna ulivyowatendea watu wa moshi uungwana na utu bila kujali dini kabila wala itikadi zao. nenda gwiji wa demokrasia Moshi nenda baba wa mageuzi nenda mtu wa watu. Kalale peponi NDESAPESA
 
Back
Top Bottom