Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,991
- 831,561
Kwanza ieleweke wazi kuwa NDELE si kwa wanawake bali ni kwa wanaume hasa wale madomo zege
na wale ambao fani yao kubwa na hobby ni CHUBWI CHUBWI, wazee wa chupi, wazee wa kutokwa na denda wakiona gauni, wale ndugu zangu ambao ukimpa milioni inafika lakini sio jinsia pinzani Hiki kitu si cha leo jana wala karne iliyopita, kina historia ya vizazi na vizazi! Mfalme Suleiman alikuwa na wake 300 na masuria(michepuko)600! Acha kabisa hiki kifaa Mswati anadipu
Tamaa ya ngono kaumbiwa mwanaume ni jambo la kiasili mno mpaka kwa wanyama, ni katika harakati hizi za kutaka kupendwa na wanawake wengi ama mwanamke yeyote utakayemtaka ndio wataalam wa sayansi mbadala wakaja na ufumbuzi wa ndele kule Tanga (kumbuka mapenzi yalizaliwa Tanga
)lakini hii ilikuwa nyakati hizo enzi hizo, ambapo hesabu ya wanawake na wanaume ilikaribiana kufanana kabisa!Leo hii tuko kwenye ulimwengu mwingine kabisa, pengo kati ya hizi jinsia mbili ni kubwa mno, wanawake ni wengi kuliko wanaume! Ndele haina nafasi tena, siku hizi silaha SHEKELI
siku hizi huangaliwi wewe ni nani bali una bei gani kibindoni NDELE ina madhara mengi, Kwanza wapigaji ni wengi unaweza kupigwa pesa na usiipate ndele lakini ukibahatika kumpata mkweli na akakutengeneza tegemea haya yafuatayo
-wake za watu watakuwa wako

-wafanyakazi wa ndani
-kina mwajuma ndalandefu n the like
-wafupi wanene wembamba weusi wembamba
wote wall-wenye gundu wenye Mali wenye kimavi wenye bahati NDELE haibagui

Utachoka wewe...utawakimbia...itakuwa kero LAKINI mwisho wa siku NDELE ikiisha nguvu nyota yako ya NGEKEWA! nyota yako ya KUPAPATIKIWA na kila gauni, nyota yako ya kupendwa ikafa utajuza kuzaliwa....utakataliwa mpaka na CHANGUDOA
kama bado unataka ndele chukua muda kufikiri mara nyingi kabla hujachukua maamuzi
NB: faida ya ndele ni sifa ya kuwa kiwembe kuliko TOPAZ
