Ndege ya Air Tanzania kukaa muda mrefu kwenye Matengenezo huko Malaysia

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
501
947
Nchi ya Tanzania ilinunua ndege mpya aina ya dreamliner natumaini ni mwaka 2021 lakin ndege hii haina zaidi ya miaka mitatu tayari iko gereji. Ndege mpya aingii akilini mwangu. Wakati ndege hiyo inapelekwa kwenye matengenezo wananchi hatukutaarifiwa na baadaye raia mwema ndo katoa taarifa hii.

Hasara inayopatikana kwa ndege hiyo kutofanya kazi kwa muda huo ni hasara kubwa na hii inaonyesha jinsi hatuko maakini na mali za umma. Ndege ina muda mrefu kwenye matengenezo na wananchi wanakosa huduma na huku tukielezwa na MD wa Air Tanzania kuwa iko kwenye foleni na muda wake wa matengenezo bado kwa sababu kuna ndege zingine mbele yake.

Huu mradi wa kununua ndege binafsi naona kama tunapoteza fedha za umma bure na ni afadhali fedha za kununua ndege mpya zingeelekezwa kwenye miradi mingine kama afya, barabara, maji n.k. Mwaka ujao utaona ripoti ya CAG kuhusu hasara ya ATCL.

Nimesoma leo kuwa Ethiopian Airlines imetengeza faida ya $6.1 billion kwa mwaka mmoja na Kampuni inasimamiwa na Serikali ya Ethiopia. Sisi tunakwama wapi. Tuwe maakini na fedha za umma. Wananchi wanakamuliwa kwa jili ya kodi.
 
Dar - Mwanza siku hizi imekuwa kawaida flight ya saa saba mchana ikiruka nyingine mpaka saa tano usiku, hapo katikati kuna gap kubwa sana hakuna ndege yeyote na bado delay zakutosha.

Usafiri wa ndege hapo katikati ulianza kuwa wa kawaida sana Tanzania enzi za fast jet na watu wengi sana walianza kuwa wanapanda ndege, Toka Air Tanzania wamebaki wenyewe kwenye game usafiri wa ndege sasahivi umeanza kuwa anasa na kuwa kana kwamba wanasaidia tu na sio biashara.

Kuna Hatari hili shirika kurudi lilikotoka kwa kufa au kutumia hela za Watanzania kila siku kufidia gharama za uendeshaji.

Back to the topic: unanunuaje ndege ambayo within 3yrs inakwenda kwenye major repair au hata scheduled repair ambayo itacost huge amount of money na time? ROI hapo inawork vipi? maana tayari hiyo ndege ni unreliable just baada tu yakutoka Kwa mtengenezaji.
Warrant policy imekaaje kwa ndege iliyorun 3yrs halafu inahitaji matengenezo ambayo NI fault ya manufacturer? ( Au kuna vitu tunafichwa)
 
Toka fast jest itimuliwe na baadaye haya madude yaanze kuletwa sikuwahi kutaka kujua au kuangalia sherehe zake wanapo yapokea, maana nilijua hapa tumepigwa tayari.

Serikali yetu na nyingine nyingi za kiafrika pamoja na yote wanayofanya, hazipo kwa lengo la kusaidia jamii bali kudidimiza.

Sasa hilo dubwasha ndani ya miaka 3 limekufa na majamaa yanapiga pesa mbele kwa mbele no rescue dog hata mmoja mwenye huruma hapo.
 
Nchi ya Tanzania ilinunua ndege mpya aina ya dreamliner natumaini ni mwaka 2021 lakin ndege hii haina zaidi ya miaka mitatu tayari iko gereji. Ndege mpya aingii akilini mwangu.

Mkuu kwa ufahamu wako, je ndege ikiwa mpya ni baada ya muda gani inapaswa ifanyiwe "major maintenance na inspection"?

Maana naona swali na wasiwasi wako umeuelekeza kwenye umri wa ndege lakini haujenga msingi wa hii hoja kwa kuweka bayana umri wa ndege vs matengenezo ya lazima
 
Back
Top Bottom