Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Nchi yetu inaitwa Tanganyika

wazanzibar weng mdebwedo kuanzia kufikiri kwao midomo yao, ufahamu wao,ndio maana hoja zao si za msing wanashndwa kuvunja muungano wanakimbilia kuchoma makanisa nakufuatafuata wakristo walio tulia kimya wakingoja wakat
 
Wazenji bana mmmh, wamechoka eti kudhurumiwa na watanganyika!lol!
 
Mbona wazanzibar wanajielewa kwanini watanzania ni wepi? na watanganyika je?
 
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa Tanganyika,
maana ya neno Tanganyika, siijui,
Tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui

nilizaliwa Tanzania,
nilizaliwa Afrika
nilizaliwa duniani
nlizaliwa na mwanadamu

kwa hiyo;

mimi ni mtanzania
mimi ni mwafrika
mimi ni mdunia
mimi ni mwanadamu

maana ya Tanzania, najua
maana ya Afrika, najua
maana ya Dunia, najua
maana ya mwandamu, najua

nawauliza wazanzibari,
nini maana ya Zanzibari,
nani aliipa jina Zanzibari,
kwa nini wajivunie uzanzibari?
kwa nini wasijivunie utanzania?

HICHI KITU CHENYE UHARAMU NDANI YAKE YAANI TANZANIA , HAKUNA HAJA YA KUKIKUMBATIA,
MTU HULILIA CHAKE , TANZANIA ALIIANZISHA NYERERE BAADA YA KUIVAMIA ZANZIBAR NA KUWAKAMATA VIONGOZI WAKE NA KUWATUPA KATIKA MAJELA YA TANGANYIKA MWAKA 1964 KABLA YA HIYO UIITAYO TANZANIA HAJAIANZISHA.
KUMBUKA HAO VIONGOZI WA ZNZ NI WALIOCHAGULIWA KWA DEMOCRATICALLY PROCESS

JELA ZA NYERERE TANGANYIKA ZILIKUWA HIVI ,


MJUE NYERERE NA JELA ZAKE


Katika mwaka 1968 Hakimu Seaton, Hakimu wa Mahakama Kuu; alitembelea gereza la Mwanza.
Nilimuuliza kama kuna uhalali wowote juu ya kuwekwa kwetu kizuizini.

Mkuu wa gereza akamwambia Hakimu kuwa hakuna karatasi zozote zilizoletwa pamoja na mawaziri wa zamani wa Zanzibar.

Hakimu akaahidi kulifuatilia suala hili. Baada ya miaka minne tangu wakati huo, nikiwa katika gereza la Bukoba, Katibu wa Mkuu wa Mkoa alitoa shauri kuwa nimuombe Raisi anitoe kizuizini.

Nalimwambia kuwa kwa vile sijui nini kosa langu la kuwekewa kizuizini naona sina hoja za kimsingi juu ya ombi langu.


Alinijibu, “Hapana shaka ulipotiwa kizuizini ulisomewa amri ya kutiliwa kizuizini.”

Nilimwambia kuwa, vile ninavyo kumbuka mimi hapakuwepo amri ya mimi kutiwa kizuizini.
Suprintendent wa magereza akanambia kuwa ilikuwepo amri, hapo akanisomea hio amri ambayo ikionesha kuwa inatokana na Raisi na ambayo imeandikwa kwa lugha ya kisharia.

Amri hio inasema kuwa Raisi baada ya kutoshelezeka kuwa, fulani na fulani; akiwataja mawaziri wote wa Serikali ya Muhammad Shamte, kuwa walikhusika na vitendo vya uchochezi wa kukhatarisha salama ya nchi, alitoa amri tutiwe kizuizini.

Nalipomuuliza amri hio ilitiwa sahihi lini, ilidhihiri ilikuwa ni mwaka wa 1968, baada ya muda mchache tangu pale nionane na yule Jaji Mkuu, Seaton kwenye gereza la Mwanza!


Sisi tulivamiwa nchi yetu na kutiwa vizuizini katika mwaka wa 1964. Najuwa kulikuwa na mapinduzi (mavamizi) huko Zanzibar, na hicho kitendo cha kiharamia iwe kimetokea huko.

Lakini tangu kati ya mwaka wa 1964 pale tulipotiwa vizuizini mpaka hii 1968 ambapo hii amri ya kutiwa kizuizini kutolewa na kutiwa sahihi; wakati huo wote - miaka minne - kuwekwa kwetu kizuizini na yeye Raisi Nyerere ambae ndie aliekuwa na hukumu yote huko Tanzania bara basi hakukuwa kisharia hata katika hio sharia ya kidhalimu ya Tanzania.

Kwa muda wa miaka minne kabla ya kutiwa sahihi hii amri ya kuwekwa vizuizini sisi tulikuwa basi ni wafungwa wake yeye Nyerere.

Je, ndio inayumkinika katika muda huo iwe yeyote miongoni mwetu sisi tuweze kufanya vitendo vya uchochezi wa kukhatarisha salama ya taifa?

Tujaalie kuwa inakusudiwa ule muda kabla ya kukamatwa na kutiwa kizuizini.

Wakati huo sisi tulikuwa ni mawaziri wenye mas-ulia kwa vile tulichaguliwa kulingana na sharia ya kikatiba iliokuwepo nchini - Zanzibar - wakati huo.

Je, sisi wakati huo tutaweza kuwa tutende kama vile ilivyoelezwa katika hio amri iliotiwa sahihi na Julius Nyerere?

Kama itakavyokuwa, hilo taifa linalo elezwa kuwa ni Tanzania; halikuwepo kabla ya sisi kukamatwa na kutiwa vizuizini.

Huyo ndio mkuu wa nchi, anaejigamba kuwa yeye ni mwenye kuweka haqi, anafika kuzuwa na kupanga uwongo kama huo; ni jambo la kushangaza sana; lakini kwa watu kama yeye sio ajabu kulitenda.

Baada ya kupata hoja hizi ndipo nilipomwandikia Raisi, bila shaka maandishi yangu yalikuwa ni ya upole na kweli za hakika.

Sikupata majibu. Kwa hakika sikupata hata mara moja jawabu au hata kuarifiwa kuwa zimefika, baruwa zangu kadhaa wa kadhaa nilizompelekea Nyerere, tangu niko kizuizini na hata baada ya kutoka. Utaritibu wa hishima kama hio Tanzania inaonekana ni mpango wa kikoloni uliokwisha pitwa na wakati.


Dr. Kleru alikuwa ni Mkuu wa Mkoa aliepigwa risasi na mkulima, Abdulla Saidi Mwamindi; siku ya krismasi mwaka 1971. Mkulima huyu, Abdulla Saidi, alikuwa ni miongoni mwa watu kadhaa wa kadhaa walionyang’anywa mashamba yao kwa kuwanzishia vile vijiji vya ujamaa. Jeuri ya Mkuu wa Mkoa huyu ilifurutu ada.

Waliokuwa wakiteswa na kudhulumiwa na Mkuu wa Mkoa huyu walishitaki kwa wakuu wa chama.
Kila wakishitaki huambiwa wakashitaki polisi; na wakifanya hivyo.

Kamanda wa Polisi, Abubakar aliwaonya wakuu huko Dar es Salaam juu ya vitendo viovu na vya kuudhi vya Mkuu wa Mkoa huyu na juu ya ile tabia yake ya ulevi kufika kuanguka na kuingiliwa na wahuni.

Baada ya kupigwa marisasi na kuuliwa, wale jamaa wote waliokuwa wakipeleka mashtaka yao Polisi walikamatwa na kuwekwa kizuizini mpaka Abdulla Saidi Mwamindi ahukumiwe na kunyongwa. Hata kabla ya kesi kumalizika, magazeti na vyombo vyote vya khabari vya Serikali na vya Chama, vyote vilianza shutuma zao, sio tu dhidi ya Mwamindi, bali dhidi ya wakulima wote, huku wakisemwa, “mabepari", "wanyonyaji", "wakoloni" na makhaini".

Mudhahara uliopangwa na Sirikali ukaingia njiani kupita kuwashutumu na kuwalaani watu hawa. Kwa hali hii ikawa Mwamindi kesha hukumiwa na vibaraka vya Sirikali hata kabla ya kufikishwa mahakamani.

Mashahidi wote wale ambao wangeliweza kutowa ushahidi japo kuthibitisha juu ya vitendo vya uchokozi vya yule Mkuu wa Mkoa walizuiliwa mpaka pale kesi kumalizika.

Khatuwa hii ilikusudiwa kumtia khofu yeyote yule aliekuwa na fikra ya kutaka kutowa ushahidi upande wa mshitakiwa.

Hivi ndivyo sharia inavyo firigiswa katika nchi kama hivi Tanzania wakati ambapo sharia ya kumtia mtu kizuizini bila ya kupelekwa mahakama inatumika.

Watu kumi na mbili wa Iringa pamoja na yeye Mwamindi mwenyewe walikuwa pamoja na mimi gerezani Dodoma.
Kamanda wa Polisi Abubakar, na yeye vilevile aliwekwa na sisi siku mbili gerezani akiwa yumo katika pirika za kuhamishwa kutoka gereza hii na kupelekwa gereza jengine.


Ilani nyingi zilitolewa na kutangazwa ulimwenguni juu ya maafa na mateso katika magereza ya Zanzibar na Pemba.

Lakini hapana lililosemwa na kuelezwa walimwengu kukhusu mateso yanayowapata wazuiwa katika magereza ya Tanzania bara.

Sio kuwa uwovu na mateso wanayotendewa wazuiwa magerezani huko Tanzania bara hayajuulikani; mengi yake hayafiki ulimwenguni basi kwa sababu ya kukosekana demokrasia na heshima ya haki za binadamu juu ya haki ya kueleza na kujieleza.

Kutokana na hali hii, mateso na vitendo vya kikhabithi havielezwi nje kwa walimwengu kukhofia hao watakaoeleza kuadhibiwa na utawala wa kidikteta. Niliona kwa macho yangu nilipokuwa gereza la Mwanza, wakati ambapo Superintendent Odenyo ndie aliekuwa mkuu wa gereza wakati huo; niliona wafungwa walipozuiliwa chakula na maji kwa muda wa siku nne, kisha wakapelekwa hospitali (nusu maiti) na ripoti kuwa (ati) walikuwa wamegoma kula.

Nilipokuwa Dodoma nilikuwa nikisikia kadhia kama hizo.
Nikisikia, kwani baina yetu ilikuwa ni kuta, baina ya chumba niliokuwemo na vile vyumba vya mateso.

Katika gereza la Dodoma aliekuwa katili hivyo ni Ofisa Mkuu, aliepangwa jina “Iron Face” (Uso wa Chuma), kwa vile akijuulika kuwa hajapata kuwa na huruma.

Mkuu wa magereza hapa, alifika kuwa hajishughulishi tena na kazi yake; hivi ni kwa sababu kwa hichi cheo chake cha juu na daima kuwemo katika vikao na sherehe za kisiyasa, takribani alimuachilia uendeshaji wote wa gereza mikononi mwa msaidizi wake - huyu Ofisa Mkuu. Mabwana wawili hawa waliyafanya maisha ya gerezani hapa hayastahamiliki hata kidogo.


Ile mikutano ya kawaida ya kila Jumamosi ambapo ofisa mas-uli hutarajiwa asikilize malalamiko ya wafungwa ikawa haifanywi tena.

Ziara za kila mwezi gerezani za Mahakimu mbalimbali nazo pia zikasita. Wafungwa hutiwa gerezani na kufika kutolewa bila ya kujuwa kuwa wanahaki ya kuwasiliana na watu wao.

Inafaa ifahamike kuwa hivi kuharibika hali kiwango hichi, sio tu katika gereza la Dodoma. Niliiona hali kama hiyo katika gereza la Mwanza.

Gereza la Bukoba ilikuwa haijambo pale nilipoondoka.
Lakini, wakuu wa kisiasa; kama vile Mkuu wa Mkoa na Mawaziri dhahiri shaahir walikuwa wakijiepusha kuyazuru magereza na kujuwa hali za wafungwa na wazuiwa waliomo humo magerezani.

Ama Raisi na Makamu wa Raisi, si dhani kama iko siku wamewahi kuzuru gereza lolote lile katika Tanzania bara, licha kuzungumza na mabwana au mabibi waliowatia humo magerezani.

Hali katika gereza la Dodoma ilizidi kufanywa kuwa mbaya kwa ukhabithi wa huyu “Uso wa Chuma” na kulemaa kwa ulevi wa marungi Msaidizi wa Superintendent.


Mpango ulifanywa kumuuwa “Uso wa Chuma”. Mmoja wa wafungwa aliweza kupata kisu na akataka kumpiga nacho huyo “Uso wa Chuma”, kwa bahati akaanguka kifudifudi, kichwa chake mbali na yule mfungwa ambae alikuwa na pingu za chuma miguuni mwake na yeye vilevile akaanguka upande wake.

Wakati huo mfungwa aliweza basi kuipata miguu ya “Uso wa Chuma” na kuanza kumpiga visu vya miguuni mpaka pale ilipowezekana kuzidiwa nguvu akanyang’anywa hicho kisu.

Hapo tena akaingiliwa mfungwa huyo kupigwa marungu mpaka akawahijiwezi ndipo alipotiwa pingu za mikono. Askari wa gereza akaamrishwa kumpiga marisasi ya miguu.

Hivyo ikawa kafungwa kila upande na marisasi miguuni mwake, hapo tena akasukumizwa katika chumba cha adhabu.
Baadae kidogo msaidizi wa superintendent akaja na yeye akaanza kumpiga vile alivyopenda.

Vilio vyake tukivisikia kutokea katika hicho chumba cha adhabu alimokuwemo na tukamuona askari aliekuwa zamu kwenye kidungu akigeuza uso na kupiga ukelele: “Wanamuuwa huyu mtu!” Binadamu huyu akavurumishwa tena humo chumbani kisha bomu la kutowa machozi likatupwa katika hicho chumba ambacho sehemu yake ya kupitia upepo ni ndogo kabisa. Usiku uleule akajifia.


Asubuhi yake wafungwa wote wakasimamishwa kwenye uwanja na maiti ikaletwa mbele yao uchi kama alivyozaliwa. Hapo tena msaidizi wa superintendent akawa anamchocha maiti kwa gongo huku akimwambia yule maiti: “Inuka uwaambie wenzio vipi ulivyokuwa hodari, na nini mwisho wa uhodari wako?”

Baada ya hivyo tena akawahutubia wafungwa kwa kuwaambia kuwa hivihivi ndivyo tutakavyomfanya yeyote yule miongoni mwenu asiposhika adabu yake.
Hapo tena wafungwa wote wakafungiwa vyumbani mwao kisha mabomu ya kutowa machozi yakatupwa humo vyumbani mwao.

Haya yalifanywa kwa makusudio ya kuwataka watajane wale waliokhusika na mpango huu. Haukupita muda isipokuwa wengi wakatajana na kukiri makosa yao.

Lakini adhabu na mateso yaliendelea kwa wiki kadhaa wa kadhaa. Chakula kikapunguzwa, hata kwetu sisi wazuiwa. Kila mtu alitaraji mauwaji haya yatafanyiwa uchunguzi na hukumu ya haki kupitishwa. Askari wa gereza ikawa wanasema hadharani kuwa ukifanywa uchunguzi watawaambia askari Polisi hakika ya mambo ilivyo. Lakini hapana lilokuwa.

Tulisikia katika redio, kama maneno ya kupita tu yaliosemwa Bungeni - kwa woga - na mmoja wa Wabunge kuwa kulikuwa na askari makhabithi walio waadhibisha wafungwa mpaka kufika kuwauwa.

Kubwa lililotokea ni uhamisho wa kawaida wa maofisa wa magereza wa vyeo vya juu kutoka magereza mbali mbali nchini. Khabari ikamalizikia hapo.

Katika nchi yenye sheria ya kutiwa watu vizuizini bila ya kupelekwa mahakamani, kelele zozote zile ni sawa na mbwa mwenye kubweka hazina athari yoyote ile, na sharia basi ni kwa kumtumikia bwana mtawala aendelee katika utawala wake na atende vile anavyopenda.
 
Swali zuri sana.

Tuendele kuitwa TANZANIA.

Nchi imeshabadilishwa majina mara nyingi mno. Kurudia jina la Tanganyika ni utumwa. Kama lazima kurudia majina ya kikoloni, basi ni bora turudie jina la kuanza kabisa alilotuachia muasisi wa kweli wa taifa, Karl Peters, yaani German East Africa.

Kwanza kuabudu mno mstakabali aliotuachia Muingereza ni dalili ya kutoelewa hii nchi imetokea wapi na inaenda wapi. Mjerumani alitawala hili taifa vizuri zaidi kuliko muingereza, Muingereza alipewa koloni na UN alisimamie tu mpaka litapoweza kujitawala, hivyo hakufanya chochote kuliendeleza hili koloni.

Iliitwa Deutsche Ost-Africa na wajerumani, waingereza ndo wakaiita Tanganyika.
 
Mtapewa hiyo Tanganyika na kuanza kutafuta mchawi mwingine, mtasema watu wa Pwani wavivu, tunataka wabara wajitenge.

I am not knocking the idea that people should be able to decide.I just want to lower people's expectations.Kama mnafikiri kujitoa kwenye muungano ndio mnatatua matatizo yenu jueni hilo.
 
pole sana kwamwewe!!

njoo na hoja zinazoelerweka, sio kila kitu useme "nyerere" mwalimu sasa ni marehemu, njoo na hoja hai na tutazijadili. tuambie ni kwa nini tuikatae tanzania tuliyozaliwa na kwa nini tuirudie tanganyika ya wakoloni na "wauza watumwa'!

tuambie kwa nini tuililie nchi ambayo mipaka yake ni ya kikoloni na ya kitumwa, kwa nini tuikane nchi amabyo mipaka yttake ni ywa kizalendo na kizawa iliyochorwa na mwalimu nyrere na sheikkh abedi amani karume!

tuambie mpendwa,

tuambie kama unapinga mambo mema ya kwetu kwa sababu ya hasira za kuwekwa gerezani au ni kwa sababu ya uzalendo?

ubarikiwe sana mpendwa,

Glory to God!
 
pole sana kwamwewe!!

Njoo na hoja zinazoelerweka, sio kila kitu useme "nyerere" mwalimu sasa ni marehemu, njoo na hoja hai na tutazijadili. Tuambie ni kwa nini tuikatae tanzania tuliyozaliwa na kwa nini tuirudie tanganyika ya wakoloni na "wauza watumwa'!

Tuambie kwa nini tuililie nchi ambayo mipaka yake ni ya kikoloni na ya kitumwa, kwa nini tuikane nchi amabyo mipaka yttake ni ywa kizalendo na kizawa iliyochorwa na mwalimu nyrere na sheikkh abedi amani karume!

Tuambie mpendwa,

tuambie kama unapinga mambo mema ya kwetu kwa sababu ya hasira za kuwekwa gerezani au ni kwa sababu ya uzalendo?

Ubarikiwe sana mpendwa,

glory to god!

tanzania ni mtoto wa mavamizi baada ya nyerere kuvamia zanzibar ndio akazaliwa jee kuna uhalali gani kuwepo au imani yako inaruhusu kuvamia na kupora kitu cha mtu???
 
Vp mzee ban yako imetokana na kauli hii?
Jamani watanganyika wenzangu ila hamna haja ya kuwaachia hao midebwedo kale ka-nchi kao kwani nasikia kana mafuta na gas so ni vyema tukachimba ss weeee, alafu tukimaliza ndo tuwape wauwane pia tutakuwa tumefidia gaharama za makanisa na bar zilizochomwa kule kwao.
 
Mtapewa hiyo Tanganyika na kuanza kutafuta mchawi mwingine, mtasema watu wa Pwani wavivu, tunataka wabara wajitenge.

I am not knocking the idea that people should be able to decide.I just want to lower people's expectations.Kama mnafikiri kujitoa kwenye muungano ndio mnatatua matatizo yenu jueni hilo.

red ya kwanza : Tupewe na nani? maneno mengine mjifikirie kwanza......
red ya pili : tatizo sugu ni huu muungano wa kimagumashi, litatatulika haka kamuungano kakikoma
 
Nimefuatilia sana maelezo ya watu wa Zanzibar na nikaja kugundua kuwa wana haki ya kudai nchi yao. Maana kama serikali na ya muungano basi Nchi mbili huru zimeungana. Kwa hiyo ni vyema wadai nchi yao. Hivi niwaulize Watanganyika;......uko na mtu unayewatangazia Ulimwengu kuwa ni nduguyo lakini mtu huyohuyo anautangazia ulimwengu kuwa wewe unalazimisha undugu na wewe ni mwizi wa raslimali zake.....wewe unamnyonya.....kwa nini uendeleee kumkumbatia.

Kwa hali hii inabidi tusiulazimishe undugu.....ni muda wa sisi Watanganyika kupinga kudhalilishwa na ndugu huyu asiyetaka huo undugu.

Ushauri ni kuwa......Njia waitumiayo wazenj si nzuri sana. Jengeni hoja mwisho mtafanikiwa. Lakini kwa upande mwingine nawapongeza maana kwa serikali yetu ya sasa unaweza kusema mpaka siku 100 mfululizo na hakuna wa kukusikiliza.

Wito wangu kwa Watanzania ni kuwa inabidi tujipime.......maana madai yao yameandikwa hadi kwa makala ya Kiingereza watu wa nje wanasoma na matokeo yake tunaonana na kuonekana wabaya. Nimeona comment za nchi jirani zetu hususan Malawi...wakisema Uroho wa Tanzania sio wa leo maana hata wenzetu wa Zanzibar tunawanyanyasa. Wanandai tunawadhulumu fedha zitokanazo na npato la taifa.

Tafakari............. chukua hatua.
 
Nimefuatilia sana maelezo ya watu wa Zanzibar na nikaja kugundua kuwa wana haki ya kudai nchi yao. Maana kama serikali na ya muungano basi Nchi mbili huru zimeungana. Kwa hiyo ni vyema wadai nchi yao. Hivi niwaulize Watanganyika;......uko na mtu unayewatangazia Ulimwengu kuwa ni nduguyo lakini mtu huyohuyo anautangazia ulimwengu kuwa wewe unalazimisha undugu na wewe ni mwizi wa raslimali zake.....wewe unamnyonya.....kwa nini uendeleee kumkumbatia.

Kwa hali hii inabidi tusiulazimishe undugu.....ni muda wa sisi Watanganyika kupinga kudhalilishwa na ndugu huyu asiyetaka huo undugu.

Ushauri ni kuwa......Njia waitumiayo wazenj si nzuri sana. Jengeni hoja mwisho mtafanikiwa. Lakini kwa upande mwingine nawapongeza maana kwa serikali yetu ya sasa unaweza kusema mpaka siku 100 mfululizo na hakuna wa kukusikiliza.

Wito wangu kwa Watanzania ni kuwa inabidi tujipime.......maana madai yao yameandikwa hadi kwa makala ya Kiingereza watu wa nje wanasoma na matokeo yake tunaonana na kuonekana wabaya. Nimeona comment za nchi jirani zetu hususan Malawi...wakisema Uroho wa Tanzania sio wa leo maana hata wenzetu

Ulitaka tufanyaje. Mbona ni simple calculation, wakishapata nchi yao na sisi tunapata ya kwetu
 
Ulitaka tufanyaje. Mbona ni simple calculation, wakishapata nchi yao na sisi tunapata ya
kwetu

Sawa issue ni sisi kukaaa kimya as if tunawanyanyasa kweli. Na sisi tuwaambie viongozi wetu kuwa waachieni wakae peke yako. Wala hatuatakuwa wa kwanza kuvunja muungano. Kama ni matusi yametosha. Maana wakipata nchi yao kimya kimya watadhani sisi inatuuma.
 
  • Thanks
Reactions: PPM
naomba nisipate upofu, niweze kushuhudia MAKUU YA MUNGU KWA TAIFA LA TANZANIA!
 
Huu Muungano waanze kuuvunja wao ili maandiko yatimie..
 
kazi kwelikweli MUUNGANO hauna maisha marefu sisi wenyewe watanganyika tumeuchoka.....hakuna shida hizo jamuhuri za PEMBA MJI MKUU WETE NA JAMUHURI YA unguja mji mkuu Zanzibar zitapatikana tu
 
Yan nnavyokereka na hzo kelele za hawa wanaojiite et n wazanzibar na cc bara tunajipendekeza tuwaache then itatusaidia hata cc tunaodai tanganyika yetu bila kelele bnafs nmechoka sana they better go their way!
 
Ila mie nakwambia wananyea kambi. Huyu Seif mwenyewe ni tunda la UDSM sasa sijui kule kwao angesoma chuo gani...tena ukute hata boom alilamba. Kutakuwa na mtu kawadanganya. They have been duped!!
 
Fursa ya Watanzania kuandika Katiba ya nchi upya ituwezeshe kuamua ama tuendelee na Muungano au tuachane nao.

Kwa maoni yangu, hakuna sababu za Watanganyika kung'ang'ania Muungano. Kama kweli Wazenj, wakiongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wao, Seif Sharif Hamad, bila kificho au aibu, wanataka kuwa na Zanzibar independent state, basi iwe hivyo.

Katika historia itakayoandikwa karne zijazo tutaonekana kwamba maamuzi ya kuvunja Muungano ni ya kijinga, kwa vile nchi nyingi jarani sasa zinaungana ili ziweze kupiga hatua kubwa na za haraka kuendelea kiuchumi. Hata hapa Afrika Mashariki, Rwanda na Burundi zimeomba kujiunga na Jumuiya ya EAC kwa mtindo huo huo.

Labda baada ya uongozi wa Maalim Seif, Zenj ijirudi na ifikirie kuingia katika Federation of East African States itakayojumuisha Tanganyika, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom