Mtazamo WANGU binafsi Arusha madiwani ambao kwakweli NI wawakilishi WA wananchi na bahati mzuri hakuna aliyepinga kuchaguliwa Kwai udiwani, wamekaa na kuamua KUMALIZA tofauti zao, Leo viongozi wao wanapokataa muafaka ule maana yake UZALENDO KWA CHAMA NI MKUBWA KULIKO KWA WANANCHI WA ARUSHA?
Kwa hili la ARUSHA NILIDHANI INGEKUWA WANANCHI KWANZA, CHAMA BAADAE
Mheshimiwa Nape kauli yako inatia mashaka kuhusu uadilifu wako. Uadilifu ni kitu consistent na unapoona mtu anakwenda back and forth hofu ya kutomwamini inazidi. Unapotoa kauli kuna wakati zinakurudi bila kudhamiria.
Nchi kwanza chama baadaye nikauli ya dhihaka. Suala la Arusha ni dogo sana kama tunataka kuitanguliza nchi kwanza.
CCM wangefuata tarataibu bila ubabe wakakubali kukaa meza ya majadiliano, vifo na majeruhi visingetokea. Kama mkurugenzi wa uchaguzi Arusha angetenda haki bila kushawishiwa na serikali ya chama chako ingekuwa nchi ikwanza.
Hata pale alipotokea Kada mwenzako Lowasaa na kusema utafutwe muafaka, chama chako kilimzogoa! nchi kwanza wewe unaipata kutoka wapi.
Nchi kwanza haianzii uchaguzi wa Arusha. Njia hii ya mkato wa kutaka umaarufu inadidimiza na kuwadhalilisha vijana waliotegemea kuwa ungekuwa na mchango tofauti na wenye mwelekeo wa nchi kwanza. Inaonekana tayari kilevi cha madaraka kimeashakuingia katika damu, ulevi ambao ni mbaya kuliko wa pombe kwani unaondoa heshima na utu wa mtu.
Mikataba ya madini, IPTL,Richmond, Dowans, Kagoda, meremeta, Tangold, Kiwira, Deep green, BAE,ujenzi BoT, pesa za kunusuru uchumi ni mambo yanayoliumiza taifa hili sana. Kashfa hzio peke yake zinaweza kutoa bajeti ya nchi.
Mwenyekiti wako, Waziri mkuu wako, Spika wako, Mwanasheria wa serikali yako, Katibu mkuu wa chama chako, wewe mwenyewe, Wabunge wa chama chako, Mkurugenzi wa PCCB wa seriklai yako wote mumeungana pamoja katika kuficha na kuwatetea waovu wanaolimaliza taifa kiuchumi na kimaadili bila haya wala soni. Mnakaa vikao vya kutafuta maeno ya kutughilibu kama vile, uchunguzi bado, kutoingilia madaraka, haki itendeke, tunafanyia kazi ili mradi tu muwakingie kifua wahalifu kudharau watu milioni 40.
Nape unafahamu fika pesa za kodi za masikini anayeishi kwa mlo mmoja ambaye mtoto wake haendi shule na asiye na mategemeo ya baadaye zinatafunwa na ninyi ndani ya serikali kwa kibali cha CC/NEC ambayo wewe ni mshiriki. Yote haya yanafanyika mchana na ukiyaona kwa macho yako mwenyewe, LEO UNAPATA WAPI USHUJAA WA KUSEMA NCHI KWANZA, endapo wewe na kundi lako mumeshindwa kuiweka nchi kwanza?
Nape unafahamu kuwa hujuma ndizo zinalipeleka taifa kwenye giza tororo! unajua dhuluma ya kupokea posho kwa kulala bungeni, unajua kuwa mashangingi yanaitafuna serikali bila huruma, leo unasema nchi kwanza! white elephant!
Wezi wa kuku wanafikishwa mahakamani na wengi tayari wapo keko, wezi waliokubuhu wa mali za umma mnawaita 'wanaochafua chama', badala ya kuwafikisha mhakamani mnaenda Dodoma katika mahakama ya kujivua gamba. Ghiliba hii umekuwa unapita nchi nzima ukiihubiri kana kwamba ukiiba na kuachia madaraka ndiyo nchi Kwanza!! Nape Nape, tafadhali usituchefue, tuna hasira ya kupigika kimaisha kutokana na uzembe uliokubuhu ndani ya chama na serikali amabayo wewe ni mshiriki muhimu, unapokuja na kauli za mzaha kama hizi unatudhalilisha na kututia hasira zaidi.
Kuliko kutafakari uchaguzi wa Arusha, nakuomba utafakari yafuatayo.
Hakuna aliyejua kaburu ataachia South Africa aliyoikalia miaka 500.
Hakuna aliyejua kuwa Idd Amin, Mobutu, Bokasa watafariki katika dhalili kubwa kiasi kile.
Hakuna aliyejua ukuta wa Berlin utavunjwa siku moja.
Hakuna aliyejua dola kubwa ya Urusi itaparaganyika na hakuna aliyejua kuwa Mubarak na Ben ALi wataondoka kwa dhalili.
Tuachie sisi tufikirie nchi kwanza, wewe enenda kwenye vikao vyenu mkapange mikakati ya kutetea wahalifu kwa njia ya gamba. Sisi tutatetea nchi yetu na hakika ni nchi yetu.