CHADEMA wanarudia makosa yale yale yaliyowahi kufanywa na NCCR-MAGEUZI na baadaye CUF.Migogoro ikishughulikiwa vizuri hukinufaisha Chama kwasababu mpaka mnaamua kupatana na kuyamaliza maanake ni kwamba mmeamua sasa kushughulikia matatizo ya msingi yaliyosababisha hadi mkaingia kwenye mgogoro na hatimaye kuamua kwenda na common ground.NCCR-MAGEUZI wakashindwa kushughulikia mgogoro wao katika namna inayofaa kwasababu waliuchukulia mgogoro kama tatizo kwao badala ya kuuchukulia mgogoro kama changamoto/maswali yaliyohitaji ufumbuzi/majibu sahihi,Matokeo yake Chama kikadhoofika.CHADEMA wakashindwa kujifunza kutokana na hayo makosa ya NCCR-MAGEUZI na wao wakajiingiza kwenye mtego huo huo sasa wanayaona matokeo yake japo hawataki kukiri hadharani,Nashukuru kwamba muasisi wa CHADEMA ameona matokeo ya mgogoro kwa Chama chake na kuamua kupiga stopu timua timua ndani ya Chama.
CUF wao walifanya kosa jubwa la kujaza Viongozi wengi wa ngazi ya Taifa kutoka imani moja ya kidini.CCM wakatumia mwanya huo kuwafungamanisha CUF na udini,Japo walijitetea lakini sura ya uongozi wa Taifa kwenye Chama chao uliwaangusha na kudhoofisha utetezi wao.CCM wakafanikiwa kutumiwa mbinu yao ya wagawe ili uendelee kuwatawala,CUF taratibu ikaanza kupotea huku Bara kutoka Chama kikuu cha Upinzani hadi hapa kilipo.CHADEMA nao wakaingia kwenye mtego huo huo wa maangamizi ya kisiasa.CHADEMA kama walivyokuwa CUF walishindwa kuweka uwiano mzuri wa Viongozi wa Kitaifa ambapo nyadhifa za juu zilishikwa na Wakristu na Wakaskazini huku watu wa imani nyingine na wa kutoka kanda nyingine wakipewa aidha unaibu/umakamu au nyadhifa zisizo na umuhimu sana ndani ya Chama.Kwa mfano nafasi nyeti kama za Mwenyekiti,Katibu mkuu,Mkurugenzi wa fedha,Mkurugenzi wa masuala ya Bunge,Hazina zimekwenda kwa Wakristu wa kaskazini.CCM waliuona huu mwanya na walikomaa nao miaka nenda miaka rudi japo kuna baadhi ya wanaCHADEMA waliamini kwamba propaganda machine ya CCM safari hii haitafanikiwa dhidi ya CHADEMA kama ilivyokuwa kwa CUF lakini baadhi yetu tulijua madhara ya propaganda za udini/ukanda dhidi ya CHADEMA yataanza kuonekana muda si mrefu kutokana na namna Viongozi wa CHADEMA walivyokuwa wakifanya makosa ya dhahiri kabisa ya kufanya mambo yale yale ambayo CCM wamekuwa wakijaribu kuwafungamanisha nayo.Hili ndilo kosa kubwa kabisa ambalo Viongozi wa CHADEMA wamelifanya la kurejea makosa ya kisiasa yaliyofanywa na Vyama vya NCC-MAGEUZI na CUF.