Nawashtaki Grace Kiwhelu, Lucy Owenya, Mary Chitanda na Mwanasheria Mkuu

Mkuu sijaingiza siasa za vyuoni kama unavyodai. Nimejadili hoja yake kwa namna ambavyo mimi ninaona. Tatizo lenu kuna kundi fulani humu jamvini halitaki likosolewe. Na kwamba hoja ikitolewa na mmoja wa watu wa kundi hilo basi sisi wengine wote tuisifie na kuimwagia thanks. Tukiijadili kwa maono kinzani kinyume na vile mnavyotaka basi matatizo. Kama hivyo ndivyo basi waambieni mods wawaondoe wale wote wenye mtazamo tofauti na ninyi.
Mimi, Msando simfahamu wala hatuko pamoja kwenye hilo kundi unalosema lipo. Najua angesema anamshtaki Chatanda wa CCM na Mwanasheria Mkuu mngempa misenks ya kudondosha thread hii. Yeye kaona mbali zaidi. Kagundua tatizo hilo hata kwenye chama chake lipo. Na sio kwa majimbo hayo mawili tu Tanzania hii. Alifumbie macho kwa kuwa linaigusa CHADEMA au afanye kile ambacho TAALUMA na dhamira yake inamtaka kukifanya?
 
Mkuu nadhani imeelezwa mara kadhaa ndani ya thread hii kwa nini option ya maandamano ilionekana kushinda hiyo ya mahakamani. Ni kuwa hukumu ya kesi ingetolewa miaka kadhaa baadae na hivyo kupoteza ule uhai wa suala lenyewe. Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la ubungo ya Mh. Mnyika dhidi ya Keenja na. 1 ya mwaka 2006 hukumu yake ilitolewa lini? Huo ni mfano mdogo tu lakini zipo mamia kwa mamia ya kesi za namna hiyo. Nina uhakika unalifahamu hilo.

Tuwe tunafanya subira hasa kwenye kesi ambazo zitarekebisha mustakabali wa siasa za nchi yetu endapo hukumu sahihi itatolewa. Tusiangalie waliosababisha kesi ikafunguliwa tu. Nakumbuka hata ile ya Mgombea binafsi imechukua miaka kuiamua hivyo Majaji wetu walivyokuja kuiamua. Meya wa CHADEMA Arusha asingesababisha watu kufa. Yametokea. Tuyaache. Sio ya thread hii.
 
Kuna mbunge wa viti ,maalum namelok sokoine alichukua fomu monduli lakini kwa sasa yupo halmashauri ya arusha mjini naye aongezwe kwenye list
 
Kuna mbunge wa viti ,maalum namelok sokoine alichukua fomu monduli lakini kwa sasa yupo halmashauri ya arusha mjini naye aongezwe kwenye list

Unajua CDM walivuruga kura za BAWACHA kiasi kwamba hizo kura unazosema zikawa-nullified.
Walitengeneza vigezo vyao ambavyo yawezekana hizo fomu za CDM wilaya hazikuwa na kazi tena.

All we need to do here ni kumpa Msando a helping hand au changamoto zitakazo boresha kesi yake coz huyu mdudu anaitwa "viti maalum" upatikanaji wake umejaa kasoro si kwa CCM pekee bali vyama vya upinzani pia.

Baadhi ya dada zetu wanajikuta hawana uwezo wa kusema NO kwa walioshika funguo za kuwapeleka bungeni.
 
Go Msando, mimi ni Chadema nafurahishwa na hatua hii unayochukua, tukitafuta haki tutafute pasi kuangalia nani inamwathiri.
 
Msonda, jitahidi usiwe Distracted from tha Main Issue, Ujue kwenye "Home of Great Thinkers" na Mataahira Wachache hawakosekani utawatambua kwa Kauli zao.
Back to Real Business, kuna Mambo machache naomba Unifafanulie, Kisheria na Kisiasa.
1. Baada Madiwani kula kiapo, Je, Kikao kilichokaa kumjadili Chatanda mpaka wajumbe wa CDM wakaamua Kutoka hakiwezi kuwa Termed kuwa ndio Kikao cha Kwanza?
2. Chatanda hakuwa NOMINATED na UWT Tanga, kwa Mujibu wa Katiba ya CCM, Jumuiya za Chama hicho hazina Mamlaka ya ku NOMINATE Wabunge wa Viti maalum, UWT, VIJANA, nafasi za Vyuo Vikuu na Walemavu, wanafanya Hatua ya Mwanzo ya Mchakato kwa kupiga Kura za Maoni, Maoni hayo yanapelekwa Kamati Kuu ya Taifa (CC), Kamati Kuu nayo pia HaiNOMINATE kama ifanyavyo Chadema kwa Mujibu wa Katiba yake, bali Hupeleka Mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu Taifa (NEC)kwa ajili ya hiyo NOMINATION. Kwa hiyo Chatanda na Viti Maalum wenzake wote Walikuwa NOMINATED na Halmashauri hiyo ambayo iliketi Mjini Dodoma, sasa Je, wote hao Wakaingie Halmashauri ya Dodoma?
3. Hivi kwa CDM kuandamana Barabarani hadi Watu Kufa kwa Kupinga uhalali wa Chatanda wakati Yenyewe Ina Chatanda wawili (Lucy Owenya na Grace Kiwelu) mungependa Tuwaelewe vipi?
 
Mkuu nadhani imeelezwa mara kadhaa ndani ya thread hii kwa nini option ya maandamano ilionekana kushinda hiyo ya mahakamani. Ni kuwa hukumu ya kesi ingetolewa miaka kadhaa baadae na hivyo kupoteza ule uhai wa suala lenyewe. Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la ubungo ya Mh. Mnyika dhidi ya Keenja na. 1 ya mwaka 2006 hukumu yake ilitolewa lini? Huo ni mfano mdogo tu lakini zipo mamia kwa mamia ya kesi za namna hiyo. Nina uhakika unalifahamu hilo.

Sasa maandamano yale yamemaliza vip mgogoro wa Umeya wa Arusha? Je unaweza kukiri sasa kuwa ku-opt kufanya maandamano badala ya kwenda makamani haukuwa uamuzi sahihi kwa mazingira ya suala husika?
 
Here are the court documents.

Well done Albert. I had an opportunity to meet you during the Tanganyika Law Society meeting in Arusha and had an inkling to ask whether you were suitable for CHADEMA (I have had this misgivings since you were elected a Councillor since i have known you for many years).

Despite my misgivings for particular reasons not related to the subject matter i fully support you in this endeavor since you are inclined to be reformist. I have always wished we could have people like you who are daring to go against peoples wish for the the sake of protecting/safeguarding a cause they believe in. I have read your court documents and will revert on how best you can modify them.
 
Sio wazo baya na pia mimi si mwanasheria lakini;

CCM walitumia udhaifu wa sheria kumpeleka Marry Arusha; Kwa tafsiri ya Mwanasheria Mkuu Chadema pia watumia udhaifu huo huo;

Ningekuwa mimi nadhani kwanza ninge mshitaki Mwanasheria Mkuu kwa Kesi ya Kikatiba kwa kutaka Marekebisho yatakayoekeleza kwa Kina Scope nzima ya wabunge wa viti maalumu;
Kuwashitaki Wabunge wenyewe ambao wao waliagizwa na vyama vyao kwa barua na sidhani kama walikuwa na option nadhani utanakosa uzito, labda ungewashitaki CCM na Chadema kwa kutumia sheria vibaya

Lingine kubwa: Sina hakika kama pia umepata kushauriana na viongozi wako wa CDM mkoa au Taifa pengine na maoni yao; Mara nyingine mtu anaweza hasifanikiwe sana kwa sababu tu ya methodogy unayotumia.

Zaidi ya hapo kila la kheri
 
Msando,
Usikasirike sana hadi ukaipoteza thread hii. Mimi nakuona jasiri sana. Umejisajili humu kwa jina lako halisi. Na hoja yako hii inagusa moja kwa moja maslahi ya watu. Watakuyumbisha kwa namna mbalimbali. Simamia kwenye hoja yako. Hizo siasa za vyuoni waachie wao waendelee nazo. Unalotaka kulifanya halijafanywa na wanasheria wengi nchi hii.
Watu hawajui kwamba kinachotutesa nchi hii ni utekelezaji, usimamizi na tafsiri mbovu za vifungu vya KATIBA na sheria zetu.

Nakushukuru WildCard kwa kunirudisha kwenye mstari.

Hii nchi ineliwa na kuvurugwa sana, ni wakati wa sisi kama vijana kuwa na mikakati thabiti ya kujikomboa. Kuikomboa hii nchi sio suala dogo ni lazima tujipange, tujijenge, tujuane na tujue tunasimamia nini. Sasa wengine wanakuwa waoga na wepesi kutafuta short cuts, tutajitofautisha vipi na CCM?

Kwa nini tuogope jamabo ambalo kwanza linatujenga mbele ya jamii na ni haki? Unajengaje chama kwa kufungua matawi peke yake? Tunaweza kuwa na matawi kila mahali lakini tukawa na viongozi waongo, wezi, wababaishaji, wavunjaji sheria na kadhalika. Tutakuwa tumejenga chama au tumekibomoa?

naamini kwamba kwa kushauriana na kujadili hoja zetu tutakuwa na a movement ambayo hakuna wa kuizuia. Tutafanikiwa tu.
 
Nani kakutukana?

Kama baba yako kakukosea wewe mwanawe, unachotakiwa ni kumaliza tofauti zako na yeye na sio kwenda kumshitaki. Hujafanya jitihada zozote za kuhakikisha suala hilo linamalizika au walau linapatiwa ufumbuzi katika majukwaa ya ndani ya chama.
Je ulifanya hivyo ikashindikana? Ninachokiona hapa ni kama vile unataka kutuaminisha kuwa ulifanya jitihada hizo zikagonga mwamba, kitu ambacho sijajiridhisha (baada ya kusoma hii thread) kuwa umekifanya.
Ashakum si matusi: Mkeo akikunyima unyumba utakwenda kumshitaki mahakamani?

Unachofanya ni kujidai huelewi. Naamini kabisa kwamba unaelewa.

Au kama ni kweli ni kwa sababu husomi vitu ukaelewa. Hili ni tatizo la wengi. wengi sana. Hata Mwanasheria Mkuu wa Serikali limemkuta.

Umesoma sentensi hii kwenye hiyo barua;


Sisi ni washauri wa kisheria wa Madiwani ambao majina na anuani zao yameorodheshwa hapa chini na kwa mantiki hiyo tumeagizwa kukuandikia kama ifuatavyo;
Sasa, huoni tofauti ya AlbertMsando Legal Consultants kuwa wawakilishi wa Madiwani wa Chadema dhidi ya Mkurugenzi wa halmashauri na Albert Msando dhidi ya Mary Chitanda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali?

Tatizo lako ulikurupuka mwanzoni bila kujiuliza maswali yafuatayo;

1. Why Albert?

2. What is the objective?

3. What will be the outcome?

4. What is the strategy?

5. What are the risks?

Then

6. How can I contribute in making all those better, first class?

Badala yake ukaanza kushambulia bila hoja yoyote ya msingi. Haukuwa au hauko peke yako.

Ulichonisaidia kikubwa ni kunipa indication kwamba ni kwa jinsi gani mnaweza wote mkaamini kwamba ni chama kimoja lakini mkawa na fikra za vyama viwili tofauti.

Hilo nimeliona na nitalifanyia kazi kuanzia ngazi ya kijiji, kata, wilaya, mkoa, jimbo na taifa. Chama kitaendelea kukua.

Hakikisha kama unaipenda nchi yako na Chadema basi unakuwa mstari wa mbele kukijenga chama kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Mimi sio CCM hata siku moja na sitakuwa. Nitabaki kuwa mwanachama mtiifu wa Chadema.

Mwisho, Chadema ndio imenifundisha siasa. SIO Zitto. Chadema ndio walionichukua mara baada ya kufukuzwa chuo na kuniteua kwenye nafasi ya Ukurugenzi wa Sheria na Katiba in 2003 na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa kwa tiketi ya Vijana. Jiulize hao unawaona wamebobea ndani ya Chadema walikuwa wapi. By then nilikuwa mwaka wa tatu Mlimani.

My brother, tujenge chama. tuachane na siasa zisizojenga. Kama kuna ambacho hujaelewa uliza. Wengi nimekuwa na very constructive discussions humu ndani na walikuwa au wana mawazo kinzani.
 
Well done Albert. I had an opportunity to meet you during the Tanganyika Law Society meeting in Arusha and had an inkling to ask whether you were suitable for CHADEMA (I have had this misgivings since you were elected a Councillor since i have known you for many years).

Despite my misgivings for particular reasons not related to the subject matter i fully support you in this endeavor since you are inclined to be reformist. I have always wished we could have people like you who are daring to go against peoples wish for the the sake of protecting/safeguarding a cause they believe in. I have read your court documents and will revert on how best you can modify them.

Thank you Caren. That is a plus on my part. This task isnt Albert's task, it is for all those who wish good fro the law and the country.

Reach me at albert@albertmsandolegal.com with comments on the documents.

Regards.
 
Unajua CDM walivuruga kura za BAWACHA kiasi kwamba hizo kura unazosema zikawa-nullified.
Walitengeneza vigezo vyao ambavyo yawezekana hizo fomu za CDM wilaya hazikuwa na kazi tena.

All we need to do here ni kumpa Msando a helping hand au changamoto zitakazo boresha kesi yake coz huyu mdudu anaitwa "viti maalum" upatikanaji wake umejaa kasoro si kwa CCM pekee bali vyama vya upinzani pia.

Baadhi ya dada zetu wanajikuta hawana uwezo wa kusema NO kwa walioshika funguo za kuwapeleka bungeni.

RM,

There we go again. Utaratibu wa kuwapata Viti Maalumu. Unajua ukweli ni kwamba hata sisi kama CDM tulipata tabu sana. Bado kuna manung'uniko ya chini kwa chini kwa baadhi ya wanachama. Bado kuna baadhi wanajiuliza kama Leticia alivyoondoka ni sahihi au si sahihi. Sasa nashangaa baadhi ya watu wanataka tusubiri mpaka 2014 mwezi december ndio tuanze kuhoji mambo ya msingi.

Nasema hapana. tutahoji sasa hivi na sheria lazima iweke wazi vigezo, utaratibu na sifa za mtu kuwa Mbunge wa Viti Maalumu. Huyu anakuwa ni Mwakilishi wa Kina mama na sio mwakilishi wa chama peke yake. Utaratibu wa sasa unawafanya Viti Maalumu wajione wao ni mali ya chama na kila wanachoambiwa wanafanya (baadhi lakini wengi). Wengi wanakuwa wako tayari kuuza utu wao kisa tu nafasi zao zinaonekana ni za kupewa.

Siwezi na sitaweza kamwe kuvumilia. Imefika mahali aidha tunafuta viti maalumu au upatikanaji wao tunauangalia upya. Turudishe heshima ya wanawake na pia tuwe na output ya uhakika kutoka kwao la sivyo hizo nafasi ni mzigo kwa taifa hili masikini wakati wengine ndio wanapata watu wa 'kuishi' nao kipindi cha bunge.
 
Msonda, jitahidi usiwe Distracted from tha Main Issue, Ujue kwenye "Home of Great Thinkers" na Mataahira Wachache hawakosekani utawatambua kwa Kauli zao.
Back to Real Business, kuna Mambo machache naomba Unifafanulie, Kisheria na Kisiasa.
1. Baada Madiwani kula kiapo, Je, Kikao kilichokaa kumjadili Chatanda mpaka wajumbe wa CDM wakaamua Kutoka hakiwezi kuwa Termed kuwa ndio Kikao cha Kwanza?
2. Chatanda hakuwa NOMINATED na UWT Tanga, kwa Mujibu wa Katiba ya CCM, Jumuiya za Chama hicho hazina Mamlaka ya ku NOMINATE Wabunge wa Viti maalum, UWT, VIJANA, nafasi za Vyuo Vikuu na Walemavu, wanafanya Hatua ya Mwanzo ya Mchakato kwa kupiga Kura za Maoni, Maoni hayo yanapelekwa Kamati Kuu ya Taifa (CC), Kamati Kuu nayo pia HaiNOMINATE kama ifanyavyo Chadema kwa Mujibu wa Katiba yake, bali Hupeleka Mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu Taifa (NEC)kwa ajili ya hiyo NOMINATION. Kwa hiyo Chatanda na Viti Maalum wenzake wote Walikuwa NOMINATED na Halmashauri hiyo ambayo iliketi Mjini Dodoma, sasa Je, wote hao Wakaingie Halmashauri ya Dodoma?
3. Hivi kwa CDM kuandamana Barabarani hadi Watu Kufa kwa Kupinga uhalali wa Chatanda wakati Yenyewe Ina Chatanda wawili (Lucy Owenya na Grace Kiwelu) mungependa Tuwaelewe vipi?

Buhry,

I will be honest, umefanya vitu viwili kwa pamoja. Kwanza umenisababisha nicheke niliposoma hii post. Kwamba CHADEMA tuna Chitanda wawili. Hii kiboko.

Back to issues;

1. Baada ya Madiwani kula kiapo ubishi ukaanza. Kwa utaratibu Mwenyekiti wa Mkutano anasoma agenda (dondoo) wajumbe wanazipitisha then mkutano unafunguliwa. Ndio maana agenda ya kwanza ni kufungua mkutano.

Kwa Arusha hawakufika huko. Baada ya kiapo yakaanza majadiliano. Yalipokwama fujo ikatokea wakaihirisha. Muda wote huo madiwani wa CDM hawajasaini daftari la mahudhurio ya Mkutano. Kwa hiyo naamini kwamba mkutano haukuanza tarehe 17/12/2010.

2. Nashukuru sana kwa taarifa kuhusu katiba ya CCM na utaratibu wanaotumia. Kwa ulichosema ni wazi basi kwamba nomination inaanzia chini kabisa. Na mwanzo ni kura za maoni za wanaUWT tanga au UVCCM. Ukisoma sheria tena (usichoke tafadhali kuisoma kwa kurudia rudia) utaona maneno 'whose nomination originated from'....

Tutahitaji mahakama itoe tafsiri ya maneno hayo. Kwa uelewa wangu uteuzi unaanzia chini unakamilika kwenye ngazi ya taifa.

Thanks.
 
Kuhusu Chadema na utaratibu uliotumika kuwapata wabunge wa viti maalumu. Ni kweli kwamba utaratibu wa CDM ni tofauti na ulitumika na CCM. CCM Mbunge wao alikuwa nominated by UWT Tanga. UWT ni party organ na ni tawi la Tanga. Kwa hiyo my argument is (which you seem to agree) Mary Chitanda is disqualified from being a member in Arusha.

CDM wabunge wao wameteuliwa na Kamati Kuu ya Taifa. KKT ni party organ ambayo mamlaka yake ni nchi nzima. Kuna pengo katika sheria hapo. Hivyo CDM walichokuwa wansema ni kwamba kutokana na KKT kuwa ni chombo chake chenye mamlaka kitaifa basi wana haki ya kuwapangia wabunge wao popote nchini. Naamini kwamba mwanasheria wa CDM atakayechukuwa jukumu la kutetea ujumbe wa Grace na Lucy ataliona hilo. Lakini, ni suala la mahakama kutoa mkanganyiko huo na Bunge kwenda kupitisha sheria inayoeleweka bila taabu.
Je nielewe CDM wako salama....!? kama wewe ni CDM, Mwanasheria na Diwani kupitia CDM huko juu umesema “Mtu wa kwanza kumpigia simu na kumjulisha nia yangu njema alikuwa ni Mh. Grace. Anafahamu vizuri sana kwanini nimeamua kusimamia hili. Maneno ya kuchonganisha hayana nafasi kwa sasa na Chadema itaendelea kuwa imara na salama.” je hukuwasiliana na chama chako juu ya uamzi huu...au hakukuwa na umehimu wa kuwasiliana na chama chako na kama uliwasiliana nao wanasemaje hapo kwenye nyekundu


so far watu wameshindwa kukudefeat kwa wamebaki kutoa mitusi, wakijifanya ni wana cdm kumbe wengine ni ccm. Kila la kheri kaka
Nimejaribu kupitia sijaona matusi mkuu....
 
Bro Msando,
Well done...keep it up. Ushauri wangu mkubwa ni kwamba usipoteze sana muda wako wa kujibizana na baadhi ya mijitu humu ambayo haisomi kabla kazi kukurupuka na kuanza kuandika bila kuelewa nini kimo ndani ya maandishi. Binafsi nilipoona title nilipata wasiwasi, nikamwambia jamaa angu nini tena Albert? Lakini nikaanza kusoma mwanzo mpaka mwisho nikagundua points zako.

It needs some political maturity kuelewa jinsi Msando alivyojenga hii hoja tana kimkakati ambapo itatusaidia kama taifa.

Ni rahisi sana kugundua watanzania wengi (si wote) huwa tunashabikia tu mambo bila kuangalia na kuchambua kwa makini. Hili ni tatizo kubwa sana ndo maana utasikia mtu anakubali au kusupport kitu eti tu kwa sababu kimetolewa na mtu wa upande anaoamini na wala si kwa sababu kina mantiki fulani. Tufike mahala tuwe independent in our minds.
 
Je nielewe CDM wako salama....!? kama wewe ni CDM, Mwanasheria na Diwani kupitia CDM huko juu umesema "Mtu wa kwanza kumpigia simu na kumjulisha nia yangu njema alikuwa ni Mh. Grace. Anafahamu vizuri sana kwanini nimeamua kusimamia hili. Maneno ya kuchonganisha hayana nafasi kwa sasa na Chadema itaendelea kuwa imara na salama." je hukuwasiliana na chama chako juu ya uamzi huu...au hakukuwa na umehimu wa kuwasiliana na chama chako na kama uliwasiliana nao wanasemaje hapo kwenye nyekundu



Nimejaribu kupitia sijaona matusi mkuu....

Crashwise,

Pitia tena taratibu. Na tusi si lazima liwe kiungo cha siri au kitendo kinachoshirikisha viungo hivyo.

Kuhusu kushauriana na viongozi wangu wa chama usijali. All is taken care of. Nadhani utakubaliana nami kwamba hujasikia tamko lolote kuhusu hili kutoka chamani. Pia sijapokea barua yoyote ya kunitaka nitoe amelezo kwa nini hatua za kinidhamu zisichukuliwe dhidi yangu. endapo nitapokea barua hiyo nitashangaa sana. Lakini CDM kuna nafasi kubwa ya mawazo binafsi na kushauriana.
 
Msando kuwa mkweli kwanini napokutajia namalok sokoine umuongeze hautaki , au umeshapiga mahesabu kesi uliyoivungua kupinga matokeo ya moshi vijijini una nafasi kubwa ya kushinda sasa unataka kiwelu arudi moshi vijijini ili uchaguzi ukirudiwa ujihakikishie ushindi kwa sababu uchaguzi uliopita ulibwagwa kwa kura moja:A S 13:
 
Crashwise,

Pitia tena taratibu. Na tusi si lazima liwe kiungo cha siri au kitendo kinachoshirikisha viungo hivyo.

Kuhusu kushauriana na viongozi wangu wa chama usijali. All is taken care of. Nadhani utakubaliana nami kwamba hujasikia tamko lolote kuhusu hili kutoka chamani. Pia sijapokea barua yoyote ya kunitaka nitoe amelezo kwa nini hatua za kinidhamu zisichukuliwe dhidi yangu. endapo nitapokea barua hiyo nitashangaa sana. Lakini CDM kuna nafasi kubwa ya mawazo binafsi na kushauriana.
Umesomeka mkuu, mafanikio mema....
 
Back
Top Bottom