Hii mada yako ingewafaa Sana wanalumumba wenzako kuliko huku. Naona umejikita Sana kwenye chama chako na kulazimisha yaliyomo humo kuwa ya kitaifa badala ya kichama. Hii inatokana na papara katika ubongo wako.
Niseme tu, Kati ya WAPUUZI wengi mlioko Lumumba nawe umo licha ya kutomfikia Elitwege au Jingalao au JohntheBaptist.
Hii Ni nchi ya Watanzania, sii nchi ya CCM. Wananchi wa nchi hii wako Huru kwa sababu walipewa Uhuru kutokana na kutawaliwa, otherwise tusingetawaliwa tungeendelea kuwa Huru. Kuwa Huru hakumaanishi kuishi in Isolation, Jamii ya kmataifa iliyostaarabika imeweka standard norms ambazo tunapaswa kuzifuata kwani kila Binadamu zinamfaa. Unapozikiuka, lazima Jamii ya Kimataifa ikushangae na kukuonya. Hii tu inaondoa kabisa dhana ya kuwa tuna Absolute Freedom/ Sovereignty. Kwa hiyo huo upumba.vu wenu mnaouimba huko kwenu HAUPO!
Hivi mnajionaje mko huru ilihali Bajeti yenu inawategemea hao mnaowaita Mabeberu?
Mnajionaje mko huru ilihali hamuwezi kununua ARVs, Condoms na Nets za mbu!
Hivi hao mnaowaita Mabeberu kwenye uwekezaji walikuja Kama nzi au mliwaleta ninyi?
Walianza kuiba lini? Nyie mkiwa wapi?
Unajua tofauti ya kulinda UHURU WA NCHI YAKO vs kulinda Serikali ya CCM? CCM sii nchi, na msitafute huruma ya Wananchi kwa kulikoroga na kuja na kisingizio Cha Uhuru wa nchi. Tunaifahamu mipaka Kati ya Nchi/ Taifa dhidi ya Serikali( nenda Shule ili nawe uone tofauti).
Watanzania tutalinda Uhuru wetu dhidi ya yeyote anaetufanya watumwa na anaeminya Uhuru wetu. Serikali ya Magufuli imeshindwa kulinda Uhuru wetu, imekuwa mminyaji wa Uhuru wetu, halafu unataka tumuunge mkono? Never! Ameligawa Taifa akijifikiria yeye, leo analihitaji Taifa liungane, linaanzia kuungania wapi? Ulipoligawa ulitegemea?