Kwanza niwaambie tu kama raia lazima ulinde uhuru wa nchi yako. Kuruhusu hawa wazungu waingilie mambo ya ndani ya hawana cha kupoteza kwa lolote. Pale Libya kwa mfano walipofanikiwa kuwaingia raia baada ya kushidwa kulinda uhuru wao hadi sasa mnajua yaliyopo la sivyo tunataka kuugawa uhuru wetu.
Hii kitu inayoendelea haiwezi fanywa na wazungu iwapo kila mtanzania ataamua kulinda uhuru wa nchi.
Kuna wanasiasa ukiwaangalia kabisa hawafai hata kuingia mlango wa ikulu ama wa bungeni maana wanainajisi nchi yetu na wanashindwa kulinda uhuru wa nchi yetu kwa sasabu za njaa zao.
Baada ya kupata uhuru mwaka 1961 sasa ni zamu ya kujenga nchi. Kila mmoja anajua jinsi sasa hivi nchi yetu inajitahidi kujenga miundo mbinu ya uchumi hapa hakuna wa kupinga maana kazi inapigwa kweli kweli. Cha mshingi tujenge nchi.
Pili baada ya uchaguzi wa 2015 ifahamike kwamba ccm iligawanyika sana - Timu Lowasa na Timu Membe zilimtesa sana JK na baada ya JPM kuingia madalakani kila mmoja alijua hataiweza ccm. Ni kweli kwamba JPM amejitahi sana kwa kiasi cha kukimudu kiti cha uenyekiti ambapo JK alikuwa anapotezea bila kuchukua hatua. Sasa hivi ccm bado inapitia kwenye kipindi cha 2015 - Timu Membe na Timu Lowasa bado zinatamani zipate urais eiza kupitia wenyewe moja kwa moja ama zitumie mwamvuli wa majina ya hao wawili.
Pamoja na mapungufu ya aliyo nayo JPM lakini anatimiza yale aliyotuahidi wapiga kura wake mwaka 2015 -- Mlioshindwa subirini 2020 mje muuze sera zenu tumuache Rais atufanyie kazi. Pigeni kelele bungeni.
Naamini JPM atamilizana na Wazungu na ataendeleea naujenzi wa nchi bila kuyumbishwa.
Mungu ibariki TZ.
Niulinde uhuru wa nchi yangu?? Tanzania ipo chini ya mkoloni mweusi. Watanzania hawapo huru tena
Ningekuona wa maana kama ungeleta hoja zilizotolewa na EU na kuchambua moja baada ya nyingine.
Eti unasema JPM anatekeleza yale aliyowaahidi watanzania. Yaap??
Hiyo ilani ya CCM aliyokuwa anainadi haifuati na anaikana sasa ivi.
Kwenye ilani Mliahidi kusomesha wanafunzi wa kike waliopata ujauzito, leo mnaikana.
Mliwaahidi watanzania katiba mpya kwenye ilani yenu, leo mnasema sio kipaumbele chenu.
Ni wakati muafaka sasa wagombea wote wa urais kupiwa ugonjwa wa akili kabla hawajaingia kwenye kinyang'anyiro.
Huwezi kunishawishi kutetea kiongozi anaevunja misingi ya kidekrasia na haki za binadamu pamoja na katiba aliyoapa kuilinda eti kwa kisingizio cha uzalendo.
PATRIOTISM IS TO STAND WITH THE COUNTRY ,NOT WITH THE PRESIDENT.
AND I CHOSE TO STAND WITH THE COUNTRY.
Hoja za zote EU zina mantiki zifanyiwe kazi. RAIS HAWEZI KUSHINDANA NA WAZUNGU wenzetu wameshikilia mpini. Ile ni EU sio CHADEMA wale🤣
Umeona wapi masikini akamtukana tajiri na akapewa msaada?. Na bado!