Usimtolee mfano huyo aliyetelekeza mke na watoto akakimbilia kwa kimada mke wa mtu.
Huyo sio mfano bora kwenye jamii, uliza watoto wa mchepuko wake huo anawasomesha wapi?
Nyie mnadhani yule mama mwl kuamua kususa vigora ni mchezo? Hamumjui Pombe Nyie na vituko vyama!
Sijui inawezekana wapi mtu aliyeshindwa kutunza familia yake akaaminiwa kutunza taifa.
Katika moja ya vitabu vitakatifu imeandikwa: "Asiyewajali wa nyumbani mwake ni m-baya kuliko asiyeamini (Mungu)."
Masikini wanaoshabikia FISIEMU, wana kiu na haja ya kuona watoto wao wanasimamishwa masomo kwa kukosa michango ya shule ambayo ni mikubwa kuliko ada.
Wanapenda sana kuchangia mwenge.
Wanaburudika vilivyo kuhangaika kutafuta maji mchana na usiku, wala nishati ya umeme kwao si muhimu.
Wanafurahia kabisa watoto wao wanapobambikizwa kesi na kutupwa magerezani.
Maskini hao hufarijika sana mwaka wanapovuna mazao mengi yakaozea ghalani kwa kukosa masoko kwani serikali ya FISIEMU haitaki mazao yauzwe nje ya yeyote isipokuwa mafisadi walio ndani yake. Maskini hawa wanatamani sana umwagaji damu (kwa amani na utulivu) unaochagizwa na FISIEMU kati ya wafugaji na wakulima.
Maskini hawa washabiki wa FISIEMU wanapenda kugawiwa vivazi na fedha mwaka huu wa uchaguzi na hivyo wamesahau mateso yote yatakayowakabili kwa miaka mitano. Kutukanwa na kupuuzwa kwa wazee ni wimbo unaowaburudisha vilivyo hawa maskini, pamoja na udhalilishaji wanaoupata wagonjwa na hasa akina mama wajawazito hospitalini.
Maskini hawa wanaoshabikia FISIEMU watapata wapi burudani za harufu mbaya ya majitaka yanayotiririrka ovyo na magonjwa kama "kipinduapindu" yaliyotamalaki hasa jijini Dar es Salaam bila FISIEMU yao? Tena watakosaje uhondo wa kupita kwenye barabara zenye mahandaki zilizotengenezwa kwa fedha lukuki na mara kuharibika kwa kutekwa na makandarasi wahujumu wakiongozwa na mgombea wao? Ni lini watacheka maishani bila kuambiwa wapige mbizi kama hawana nauli za vivuko? Au wakojoe kama wanataka maji? Ni lini watasikia vitisho masikoni mwao kwa utumwa waliouzoea miaka zaidi ya hamsini? Nayo raha ya kuvunjiwa nyumba bila fidia wakaipate wapi bila kushabikia FISIEMU?
Mkuu usisahau kama hao maskini, moja ya faraja kubwa ni pale maskini anapodai haki yake, kesi yake ikapigwa kalenda miaka nenda miaka rudi. Angejuaje kazi za mahakama maskini kama huyu bila kwenda huko mara kwa mara na kutoa chochote? Pia kuna ile sifa kwa maskini ambao ndugu zao wanawekwa mahabusu kwa miaka na miaka wakingojea kesi zao zisikilizwe. Wakose yote haya, mmh mbona watakonda ndio maana wanaishabikia FISIEMU.
Ee bwana wee, maskini hawa wanaoshabikia FISIEMU, hawajachoka ahadi hewa. Si umejionea mwenyewe ahadi za yule "Zaifu" zinatolewa tena na huyu changudoa wa kiume? Yeye zake zinazidi trilioni 70 (yaani mara tatu na ushee ya bajeti ya mwaka huu ya serikali) lakini wamo tu hawa maskini. Zile za "Zaifu" maskini hawa walishasahau. Kama unabisha katoe ahadi ya kuhamia Dodoma uone jinsi watakavyoshangilia.
Wamesahau kuwa kwa uzembe wa serikali ya FISIEMU ambayo badala ya kuweka akiba chakula kingi kilichopatikana mwaka jana, mwaka huu njaa imetamalaki. Watakubali wapi kukosa udhalilishaji wa kugawiwa kilo moja kwa kila familia kwa wiki mbili au mwezi?
Maskini mashabiki masikini wa FISIEMU!