Nawaomba mniombee msamaha kwa mke wangu!

Yaah hata kama unafanya mzaha ili utuchore hili ni jambo ambalo lipo ktk jamii zetu. Naomba kwa njia hii wanaumme wajifunze umuhimu kuwaheshimu wake wa ujana wao. Kwako wewe bwana Luimbo kwanza kapime VIRUSI kwani mkeo kwanza anaogopa KUFA kwani kwa story hii umejirusha na wanawake kibao? hakikisha majibu anayapata ya uhakika. Mbili Mrudie Muumba kila kitu kitakuwa Bomba
 
Na utataabika mpaka basi,nyie ndio wale msiojua thamani ya uliyenaye mpaka atakapokuwa mbali nawe au atakapokwenda kwa mwingine.
Ulichezea shilingi chooni sasa cjui kama utaipata tena.
 
naona umevuna ulichopanda-,mara zote thaman ya ktu huioni unapokuwa nacho..inaonyesha mkeo alvumilia sana,tena wewe ukawa unafanya makusudi,bila sababu yyote-
Namuombea mkeo afanikiwe zaid na zaid huko aliko
 
Imekula kwako jamaa angu!uwii, aisee arifu ni kitu gani unaleta hapa? We ni ndezi kweli mnama! Ulifikiri nini wakati unamfanyia yote hayo? Au ni hela ya machimbo ilikuzingua chalii angu, ulaa kafie mbali mwache mmama wa watu alisongeshe ati. Kibo chande
 
Mr nichukue fursa hii kumpa mkeo pole kwa kuamua kuweka furaha yake rehani ktk kipindi chote ulichomfanyia vituko na vibweka...
Pili nikupe pongezi kwa kukiri kua mkeo alikua jembe na kufika mlipo mchango wake ni mkubwa sana...
Baada ya hayo nashindwa nikuambie nini maana hata nikikulaumu haitasaidia kitu maana km ni akili yako ama ndugu walikutumia kumnyanyasa mtu ulotoka naye mbali nawe bila kutumia kichwa chako ukaingia basi pole sana ndugu...Sijui ni kitu gani umesahau kwa binti masikini uliyem prone usichana wake na kumpoka ujana wake na baadae kumfukuza km mbwa! Kwanini usimsaidie kwa kumwacha auguze majeraha na makovu mengi uliyomsababishia? Kwanini unageuza maisha yake ya majaribio! Why? Huoni kukuepuka ni km Mwenyezi Mungu kamnusuru na balaa kubwa ambalo lingempata yumkini?
 
jamani NAOMBENI MNISAMEHE NIMEKOSA, ukiona mtu mzima analia mbele za watu ujue kuna jambo
 
ni mwana jf mwenzetu na moja kati ya 2 ya id zake ni "lonely heart"


Je, wewe mwenyewe umeshajaribu kumuomba msamaha kwa mabaya yote mliyomtendea wewe na ndugu zako na kumuahidi kwamba hamtayarudia tena? Kama uliwahi kumuomba samahani je aliipokea samahani hiyo au la? Na kama hujawahi kufanya hivyo basi kwa maoni yangu inabidi umuombe samahani na kuahidi kwamba hutarudia manyanyaso uliyomfanyia na utahakikisha pia ndugu zako wanamuheshimu na hawatamnyanyasa wala kumtukana tena katika siku za usoni.
 
Jamani huyu mtu kashafunzwa, jambo la msingi kama alivyoomba ni kumpa ushauri na si kuzidi kumponda.Mwenye ushauri ampe afanyeje?

~tHE aLpHA nawasilisha~
 
Pole sana lakini iwe fundisho na kwa wanaume wengine. Mimi sioni sababu ya kukuonea huruma utatupa evidence ipi kama tabia uliyokuwa nayo imebadilika au ni kwa kuwa uko alost sasa? Yaani imenisikitisha sana kama mwanamke kumbe huwa mnatake advantage tu. Muache apate atakayempenda kama alikuonyesha mapenzi na uvumilivu wote na bado ukamdharau tena mbaya zaidi na familia yako pia..huoni kama ni ngumu sana aje aanziye wapi sasa. Let her find the one will care and love her.
 
Yaah hata kama unafanya mzaha ili utuchore hili ni jambo ambalo lipo ktk jamii zetu. Naomba kwa njia hii wanaumme wajifunze umuhimu kuwaheshimu wake wa ujana wao. Kwako wewe bwana Luimbo kwanza kapime VIRUSI kwani mkeo kwanza anaogopa KUFA kwani kwa story hii umejirusha na wanawake kibao? hakikisha majibu anayapata ya uhakika. Mbili Mrudie Muumba kila kitu kitakuwa Bomba
asante sana kwa ushauri wako nitaufanyia kazi
 
wape contacts NN, Buji na wengineo
ili ujue kuwa ndoa inapaswa kuheshimiwa.
 
Back
Top Bottom