Nawaelewa Wapentekoste/Walokole wanapofurahia kuketi moja meza na wakuu. Free Pentecost

Nawaelewa Wapentekoste/Walokole wanapofurahia kuketi moja meza na wakuu. Free Pentecost

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
57,243
Reaction score
90,302
Wapentekoste waliingia Tanganyika zamani sana miaka ya kati ya 1900's. Free Pentecostal Church of Tanzania (FPCT) walianza kuwepo Tanzania mwaka 1932, hata hivyo hawakuweza kupata mafanikio makubwa mpaka miaka ya mwishoni ya 1980 na mwanzoni miaka ya 1990. Walipoanza kuingia kwa nguvu katika jamii walionekana watu wavurugaji tu na wapiga kelele hadi wakabatizwa jina la kejeli la "walokole".

Hata hivyo kadri muda ulivyoendelea waliendelea kuvuna wafuasi kutoka Katoliki, Lutheran, Anglican hadi na Uislamu, taratibu nao wakaanza kuchukuliwa kwa uzito na heshima kubwa katika jamii, mwishowe wakaweza kupenya hadi kwa watawala wa nchi na kuwa sehemu muhimu ya ushiriki wa siasa za nchi, wakapewa kipaumbele katika viti vya mbele vya nchi na hadi sasa kufikia kuwa karata turufu ya kisiasa katika nchi. Kwa safari hii ndefu na mahangaiko mikubwa sana waliyopitia ni vigumu wao kujiondoa katika karamu kutoka meza kuu kwa sasa, tuwavumilie na kuwaelewa tu, ni wakati wao wa kula nao.
 
Nimependa ulipoeleza neno walokole. Watu wengi hawaelewi asili ya neno hili, hudhani ulokole ni dini, dhehebu na imani, kumbe ilikuwa ni neno la kejeli, dhihaka na dharau kwa wapentekoste. Huwa nashangaa sana mpentekoste kuitwa na kujiita mlokole, kumbe ni neno la kejeli tu
 
Nimependa ulipoeleza neno walokole. Watu wengi hawaelewi asili ya neno hili, hudhani ulokole ni dini, dhehebu na imani, kumbe ilikuwa ni neno la kejeli, dhihaka na dharau kwa wapentekoste. Huwa nashangaa sana mpentekoste kuitwa na kujiita mlokole, kumbe ni neno la kejeli tu
Ndio, "mlokole" ni neno la kejeli kwa Wapentekoste baada ya kuanza harakati za nguvu za kuinjilisha na kuchukua wafuasi kutoka makanisa mengine traditional, ila baadaye ni kama hata wenyewe walikuja kulikubali hili neno kama brand yao. Ni kama vile Marekani ambavyo blacks walikuja kukubali neno 'nigger" kati yao kama swaga yao.
 
Ila hapo mkuu hebu fafanua vizuri historia ya upentekoste Tanzania, maana hiyo FPCT ni jina jipya la miaka ya hivi karibuni hata miaka thelani nadhani haijafika tangu lianzishwe. Anzia Free Swedesh katika Tanganyika uje mpaka UMPT halafu FPCT. Usisahau AG kulikotokea TAG na EAGT mpaka wakatokea hawa kina FGBF, KLPT, CAG (Ndani ya CAG kuna Arise and Shine) maliza na hawa wengine wenye mrengo wa kipentekoste japo wanakataliwa na wapentekoste asilia, hawa mitume na manabii walioibuka na huduma zao huku wakiwa na elementi za upentekoste
 
Ndio, "mlokole" ni neno la kejeli kwa Wapentekoste baada ya kuanza harakati za nguvu za kuinjilisha na kuchukua wafuasi kutoka makanisa mengine traditional, ila baadaye ni kama hata wenyewe walikuja kulikubali hili neno kama brand yao. Ni kama vile Marekani ambavyo blacks walikuja kukubali neno 'nigger" kati yao kama swaga yao.
mzee Kulola alilikejeli na kulidhihaki sana neno hili mlokole, alisema mlokole ni mtu asiye na imani thabiti na hana msimamo, anabebwa na kupeperushwa na kila upepo wa imani feki uvumao, anatangatanga, leo yuko hapa kesho yuko kule, hana msimamo wa imani
 
Me hata selewii kaka,

Maake Kuna TAG, FPCT, EFATHA, MASHAHIDI WA JEHOVAH, KUNA HIZI MINISTRIES WOTE NI WALOKOLE NA KILA MMOJA UKIMUULIZ ANASEMA YEYE NI BORA KULIKO MWINGINE!!
Mashahidi wa Yehova sio Wapentekoste wala Walokole, pombe wanakunywa na hawaamini katika nafsi tatu za Mungu.
 
Mashahidi wa Yehova sio Wapentekoste wala Walokole, pombe wanakunywa na hawaamini katika nafsi tatu za Mungu.
wale hata wapentekoste huwaona si kundi lao, huwaona ni wapotoshaji na wamepotea
 
Ila hapo mkuu hebu fafanua vizuri historia ya upentekoste Tanzania, maana hiyo FPCT ni jina jipya la miaka ya hivi karibuni hata miaka thelani nadhani haijafika tangu lianzishwe. Anzia Free Swedesh katika Tanganyika uje mpaka UMPT halafu FPCT. Usisahau AG kulikotokea TAG na EAGT mpaka wakatokea hawa kina FGBF, KLPT, CAG (Ndani ya CAG kuna Arise and Shine) maliza na hawa wengine wenye mrengo wa kipentekoste japo wanakataliwa na wapentekoste asilia, hawa mitume na manabii walioibuka na huduma zao huku wakiwa na elementi za upentekoste
Ilijulikana kama Pentecostal Free Mission
 
Me hata selewii kaka,

Maake Kuna TAG, FPCT, EFATHA, MASHAHIDI WA JEHOVAH, KUNA HIZI MINISTRIES WOTE NI WALOKOLE NA KILA MMOJA UKIMUULIZ ANASEMA YEYE NI BORA KULIKO MWINGINE!!
Ninachofahamu kuhusu ministries..na hivyo vinavyoitwa vituo vya maombezi ni kusajiliwa chini ya mwamvuli wa kanisa fulani. Mara nyingi uanza kusajiliwa chini ya kanisa fulani hasa ya kipentecost kanla ya kujitegemea.
 
Ninachofahamu kuhusu ministries..na hivyo vinavyoitwa vituo vya maombezi ni kusajiliwa chini ya mwamvuli wa kanisa fulani. Mara nyingi uanza kusajiliwa chini ya kanisa fulani hasa ya kipentecost kanla ya kujitegemea.
Oooh mfano mwamposa naona anatumia Calvary nn na Arise and shine ni nn Tena ?

Au mlima wa moto alikuwa TAG lakini akotelewa inakuaje 🤔
 
Nimependa ulipoeleza neno walokole. Watu wengi hawaelewi asili ya neno hili, hudhani ulokole ni dini, dhehebu na imani, kumbe ilikuwa ni neno la kejeli, dhihaka na dharau kwa wapentekoste. Huwa nashangaa sana mpentekoste kuitwa na kujiita mlokole, kumbe ni neno la kejeli tu
Si kweli mkuu!
Chanzo cha neno "Kuokoka" si katika lugha zetu za Tanzania japo upo muingiliano wa maneno kutokana matumizi ya lugha za Kibantu katika ukanda wetu wa Maziwa Makuu (The African Great Lakes).

Movement ya watu "Waliookoka" (Walokole - East African Revival) ilianza muda mrefu (1929-1970) hasa katika nchi ya Uganda kisha Rwanda na Burundi kisha movement hiyo ilizidi kuenea hadi Tanzania.
Kulokoka = Kuokoka
Abalokole = watu Waliookoka.
 
Oooh mfano mwamposa naona anatumia Calvary nn na Arise and shine ni nn Tena ?

Au mlima wa moto alikuwa TAG lakini akotelewa inakuaje 🤔
Mbona rahisi tu...Kwa wa Pentecoste mara nyingi Hawa entertain Ile organization ya mtu Mmoja kuwa juu ya wengine so wanatengeneza diversity lakini iliyokuwa coordinated...Wakati makanisa ya litrujia kama RC, KKKT, Anglican Yana organization yenye Mkuu ambaye anaweza ku decide Kwa makanisa yao yote wa Pentecostal haiwezekani, wao makanisa yao ya mahali pamoja yapo na autonomy kubwa lakini wanakuwa na msingi ambao ni common Kwa makanisa yote.

Ukifuata mfano RC unakuta labda Kanisa la St. Peters ndiyo Kanisa haiwezi kupokea amri kutoka Kwa Papa japo Papa au askofu anaweza kuwa ni coordinator kuwaleta pamoja katika mambo ya msingi...

Hii ilifanywa kusudi Ili kuwe na counter balance kwenye power and control ya Imani...Mfano hatari iliyopo Kwa RC ni mfano Papa amekuwa recruited kwenye cult inamaana RC Dunia nzima wanaingizwa bila kupinga kwakua wao Kila kitakachosemwa na Papa ni Yes and Amen...Kwa Pentecost hii siyo possible maana Kanisa au huduma inaweza kukataa na kujitenga na hiyo coordination likajisajili kirahisi ki vyake.

Kwa mfano huo huo Kuna makanisa mengi ya Calvary Assemblies of God hayaamini katika kukata keki, kuuza mchanga na maji lakini Bado ni CAG sawa sawa na Arise and Shine. Wala Askofu Mkuu hawezi kuingilia huduma ya Arise and Shine kwamfano, isipokuwa kumshauri mwenye huduma hiyo na kuendelea kumwombea, akizidisha sana wanamtenga. Anaweza fundisha Somo kama Hilo la kuonya kwenye Mkutano Mkuu wa Kanisa lenyewe la CAG.

Kwa uchache nafahamu Askofu Mkuu wa CAG na mwanzilishi mwenzake ambaye ni marehemu (Bishop Zefania Ryoba) ni watu wenye hekima sana, hata kama hawaamini kitu huwa siyo judgemental lakini hawaachi kuonya Kwa ustaarabu. Kwa kipekee Askofu Mkuu wa CAG Yupo simple sana lakini deep rooted kwenye Imani. I used to doubt him lakini baada ya kumfuatilia niligundua ana moyo wa kichungaji, he gives it time na ameweza kuliweka Kanisa nje ya politics Kwa muda mrefu sana...Ila Sasa wanapoanza kuacha Ile misingi ya awali ataanza kuharibu Imani na kujikuta anaingiia kwenye manipulation ambazo aliweza kukaa nazo kando Kwa muda wote tangu walipianzisha huduma hadi kufanikiwa kujenga taasisi imara yenye wasomi wengi huku akiendelea kushirikiana na Kila mwenye Imani na ideology yake pasipo kujifungamanisha nao.

Pamoja na yote hayo, hata hivyo hutaisikia CAG katika mambo yakutangaza miujiza wala kuchangamana na siasa, this is the first experience namwombea tu Askofu Mkuu wa CAG awe makini sana asijepoteza credibility yake aliyoijenga Kwa muda mrefu. Yeye mwenyewe alivyokuwa powerful kama angekuwa mtu asiyejengwa kwenye misingi imara ya imani angekuwa maarufu sana huku Tanzania na tajiri sana sana, lakini ni mtu wakujizuia sana, lakini si mnyonge, anaijua nafasi yake katika Kristo na huduma aliyopewa kuionhoza ya CAG. Imagine watoto wake wa kiroho wengi ni maarufu sana including huyu wa hiyo huduma na wengine wengi wenye makanisa imara lakini na maarufu sana...wengi wa CAG origional hawajajitangazi ki binafsi na wanafanya kazi ya Mungu Kwa uaminifu wote.
 
Mbona rahisi tu...Kwa wa Pentecoste mara nyingi Hawa entertain Ile organization ya mtu Mmoja kuwa juu ya wengine so wanatengeneza diversity lakini iliyokuwa coordinated...Wakati makanisa ya litrujia kama RC, KKKT, Anglican Yana organization yenye Mkuu ambaye anaweza ku decide Kwa makanisa yao yote wa Pentecostal haiwezekani, wao makanisa yao ya mahali pamoja yapo na autonomy kubwa lakini wanakuwa na msingi ambao ni common Kwa makanisa yote.

Ukifuata mfano RC unakuta labda Kanisa la St. Peters ndiyo Kanisa haiwezi kupokea amri kutoka Kwa Papa japo Papa au askofu anaweza kuwa ni coordinator kuwaleta pamoja katika mambo ya msingi...

Hii ilifanywa kusudi Ili kuwe na counter balance kwenye power and control ya Imani...Mfano hatari iliyopo Kwa RC ni mfano Papa amekuwa recruited kwenye cult inamaana RC Dunia NJ zima wanaingizwa bila kupinga kwakua wao Kila kitakachosemwa na Papa ni Yes and Amen...Kwa Pentecost hii siyo possible maana Kanisa au huduma inaweka kukataa na kujitenga na hiyo coordination likajisajili kirahisi ki vyake.

Kwa mfano huo huo Kuna makanisa mengi ya Calvary Assemblies of God hayaamini katika kukata keki, kuuza mchanga na maji lakini Bado ni CAG sawa sawa na Arise and Shine. Wala Askofu Mkuu hawezi kuingilia huduma ya Arise and Shine kwamfano, isipokuwa kumshauri mwenye huduma hiyo na kuendelea kumwombea, akizidisha sana wanamtenga. Anaweza fundisha Somo kama Hilo la kuonya kwenye Mkutano Mkuu wa Kanisa lenyewe la CAG.

Kwa uchache nafahamu Askofu Mkuu wa CAG na mwanzilishi mwenzake ambaye ni marehemu ni watu wenye hekima sana, hata kama hawaamini kitu huwa siyo judgemental lakini hawaachi kuonya Kwa ustaarabu. Kwa kipekee Askofu Mkuu wa CAG Yupo simple sana lakini deep rooted kwenye Imani. I used to doubt him lakini baada ya kumfuatilia niligundua ana moyo wa kichungaji, he gives it time na ameweza kuliweka Kanisa nje ya politics Kwa muda mrefu sana...Ila Sasa wanapoanza kuacha Ile misingi ya awali ataanza kuharibu Imani na kujikuta anaingiia kwenye manipulation ambazo akiweza kukaa nazo kando Hadi kujenga taasisi imara yenye wasomi wengi lakini akiendelea kushirikiana na Kila mwenye Imani yake pasipo kujifungamanisha nao.

Pamoja na yote hayo, hata hivyo hutaisikia CAG katika mambo yakutangaza miujiza wala kuchangamana na siasa, this is the first experience Namwombea tu awe makini sana asijepoteza credibility yake aliyoijenga Kwa muda mrefu. Yeye mwenyewe alivyokuwa powerful kama angekuwa mtu asiyejengwa kwenye misingi imara ya imani angekuwa maarufu sana huku Tanzania na tajiri sana sana, lakini ni mtu wakujizuia sana, lakini si mnyonge, anaijua nafasi yake katika Kristo na huduma aliyopewa kuionhoza ya CAG. Imagine watoto wake wa kiroho wengi ni maarufu sana including huyu wa hiyo huduma na wengine wengi wenye makanisa imara lakini na maarufu sana...wengi wa CAG origional hawajajitangazi ki binafsi na wanafanya kazi ya Mungu Kwa uaminifu wote.
Nimekupata vyema Asante
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom