Naunga Mkono Simba kujitoa Ligi Kuu!

Naunga Mkono Simba kujitoa Ligi Kuu!

Saa nyingine tumia walahu momemnt of silence kutafakari ili usionekane mjinga na kituko mbele za watu, Simba jana imecheza na Azzam mechi ya Ngao ya hisani kuashilia uzinduzi wa ligi kuu sasa wewe sijui nikusaidiaje ili utoke usingizini!!??

Mkuu hawa jamaa wanadanganywa na huyu ex mfungwa Maaragwe wanavimba vichwa. Chezea Al Shaababu wewe?? Mtauzwa wote na jezi zenu....
 
Kunya anaye kuku akinya bata kaharisha!
Msimu ulioisha Rage ndio alikuwa wa kwanza kuwashawishi Coastal Union wakate rufaa dhidi ya Yanga kwa kumchezesha Cannavaro katika mnchezo wa Tanga!

Rage alijitolea kulisimamia hilo mapema mara tu baada ya mechi na kupewa muda wa kuongea na Redio Cloudz juu ya sheria za ligi kuu, hatua iliyopelekea kesho yake Rage na Makamu mwenyekiti wa Azam kuitisha kikao cha ghafla cha kamati ya ligi na kuipoka Yanga point3.

Hapop wanamsimbazi walifurahia sana pamoja na Azam kwa kuikomoa Yanga!

Sasa leo Mgongolwa kuwaidhinisha Yondani na Twite kuchezea Yanga ndio kunaifanya Simba itangaze kuhama ligi kuu na kuhama Zanzibar?

Rage alichemsha katika kusajili hivyo lawama msimpe Mgongolwa, kaeni mjipange upya
WAPE WAPE UKWELI WAO, WALICHEKA NA AZAM WAKATUKOMOA VIBAYA SANA ,SASA TUMEJIPANGA NJOONI TUWAPE CHA MOTO.:shetani:
 
juzi juzi kamati ya sheria na hadhi za wachezaji ilishutumiwa kwa kuweka ushabiki badala ya kufata kanuni.Maamuzi yaliyotolewa kuhusu utata wa usajili wa wachezaji kelvin yondani na Mbuyi Twite kwa kiasi kikubwa yameonyesha huenda madai hayo yana ukweli ndani yake.Kelvin aliidhinishwa kuchezea yanga na simba kuambiwa waende polisi ili kuthibitisha uhalali wa sahihi yake lakini wakati wa mashindano ya kagame Tff walimuidhinisha kuchezea yanga kwa madai mkataba aliosaini simba unaonyesha unaanza kutumika desemba 2012 kwanini tff wanakuwa na kauli mbili tofauti lakini kama wamewaambia simba waende polisi wao wamethibitishaje kwamba sahihi iliyopo siyo ya yondani.Pia yanga wameambiwa walipe pesa ambazo simba ilimpatia mbuyi twite wakati inajulikana kabisa aliyepokea pesa ni Twite wala siyo yanga hii inazidi kuishushia heshima kamati za tff na kuwafanya wapenzi wa soka wapoteze imani na chombo hicho
Hapo kwenye REd acha umbea wewe... soma hapa
Mbuyu Twite
Kwa mujibu wa Ibara ya
18(3) ya Kanuni za Hadhi na Uhamisho wa Wachezaji wa Kimataifa za FIFA, Yanga ilifuata taratibu zote katika kumsajili Mbuyu Twite, hivyo ni mchezaji wake halali. Hata hivyo, kwa vile Yanga imekiri kuwa mchezaji huyo alichukua dola 32,000 za Simba na kukiri kuzirejesha, kwa msingi wa kanuni ya Fair Play, Kamati imeipa Yanga siku 21 iwe imelipa fedha hizo Simba.

Kelvin Yondani
Kwa mujibu wa Ibara ya
44(3) ya Kanuni za Uhamisho wa Wachezaji za TFF, Yanga ilifuata taratibu zote katika kumsajili Kelvin Yondani, hivyo ni mchezaji wake halali.

Kwa vile Simba imesema mchezaji huyo vilevile alisaini mkataba na klabu yao, imetakiwa kupitia mamlaka nyingine kuthibitisha hilo, na baada ya uthibitisho iwasilishe malalamiko yake kwenye Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji, au mamlaka zozote za kisheria kwa mujibu wa madai/lalamiko husika.

My Take...........
T
atizo mlishaamini Rage ni kila kitu hivyo akili zenu mmeziweka kando na hamfikirii tena...akisema mkataba wa Yondani Yanga ni Toilet Paper mnaamini...eti anajua sheria hata usajili wa twite kachemsha anajua sheria gani? Simba acheni uvivu wa kufikiri shughulisheni akili zenu



 
Swali alilouliza ni la msingi ila kwa kuwa hujaelewa au una akili kama za Rage hutaelewa. Kwani Simba ina mchezaji mmoja?

Leo hii ndio mnajua kanuni, eti? Wakati Azam inapokwa points zake msimu uliopita na kuambiwa irudie mechi kwa makosa ambayo si yao hamkuona taratibu zimekosewa?

Mwaka wenu huu, mtanuna mpk muote vigimbi kwenye moyo muwasumbue madaktari kwa operesheni za roho
Wewe ndio kabisa huelewi unachouliza; suala la Azam ulitaka lishughulikiwe na Simba? Kwani Simba na Azam zote mmiliki ni mmoja au??????????????? Hivi wewe ulishasikia sheria inaamuliwa kwa kura?????????? Kama Simba walikuwa na haki na Yanga alikuwa na haki pia, basi Yondani alikuwa na kosa hivyo ili kutenda haki anapaswa kufungiwa. Kuipa timu moja haki ya kumtumia katika mazingira hayo ni kutoitendea haki timu pinzani. That's is not fair. Hivyo kwa msingi huo unaonyesha wazi mapenzi ya kamati hiyo kwa Yanga na hivyo Simba haiwezi kupata haki ndani ya hiyo kamati ni vema kutafuta ufumbuzi mwingine hata ikibidi kwenye mahakama za kiraia kama TFF itashindwa kusimamia haki.
 
Utatuzi si kujitoa ligi, hiyo itakuwa staili ya chadema ya kususa-susa, wakipewa kahawa na kashata wanaacha kususa. Huo ni utoto.

Simba wafate sheria na kanuni za TFF kama zimekiukwa wakate rufaa, ni ngazi mbili tu kabla hawajakata rufaa FIFA na siku hizi hakuna ukiritimba lazima rufaa isikilizwe haraka na maamuzi yatolewe within 30 days.
 
thread nzima imejaa wanazi wa yeboyebo
sorry mzee usitake kutokwa na mapovu vumilia wakati yanga atakapowapiga goli nne tuu 4-0 halafu utamaliza hasira zako.yanga oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee:a s 465::a s 465::a s 465::a s 465::a s 465::a s 465::a s 465::a s 465::a s 465::a s 465:
 
Mimi ni mpenzi wa Simba na kusema ki ukweli yatubidi tujitafakari kwa manufaa ya club yetu badala ya kubisha kishabiki. Hawa watani wetu wanayosema ni ya kweli! Kiongozi wetu mkuu Ndg Rage nadiriki kusema ni tapeli tena wa kutupwa! Nipashe wameandika vizuri kabisa wala Tusijifanye wabishi lazima tuhoji mambo yanapokwama badala ya kuhamishia lawama kwa kamati mara TFF. Watu na usomi wetu mtu anatufanya wajinga bwana! Tuamkeni for the betterment of our team! Mwenyekiti wetu ni hopeless! Mpenda sifa
 
Yanga ndio mkombozi wenu jamaani simba amkeni ,rage anataka simba isusie ligi alafu iende zanzibar kuanza cha ndimu heeehee ,mtaenda kwa ndege au meli unajua tena hizo meli haziaminiki hata kidogo ni kama rage vile... Kaa chonjo gari kubwa linakuja (yangaaa)
 
Kweli soka letu litazidi kurudi na kamwe halitasonga mbele. No wonda kila siku tunazidi kudidimia ktk viwango wa fifa. Inatia aibu na haiingii akilini kamati ya sheria ya tff kutofuata sheria na kanuni walizoziweka wenyewe. Yondani amesini mikataba miwili iko dhahiri kabisa iweje aidhinishwe kuichezea Yanga tena kuwa kupiga kura na wajumbe wa kamati?? Sheria inasemaje?? Hivi kama haya yanaonekana dhahiri mwanzoni hata ligi bado haijaanza je! Uko mbele itakuwaje? Au ndo yale ya refa Oden Mbaga kuchezesha mechi 3 mfululizo zinazoihisisha Yanga tena pale taifa 2! naunga mkono mkutano mkuu uitishwe tupate baraka za wanachama tukafungue kesi ktk mahakama ya kiraia ili tff itufungie na fifa iwafungie tff ili tuanze upya. Othawise tukikata rufaa kwa kamati hiyohiyo ya mgongolwa mambo yatakuwa yaleyale 2.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

mi naona hata kwenye ngao ya jamii wangeanzia kujitoa kuonesha msisitizo na sio kwenda kucheza na hayo ni maneno ya kumpa habari bin zubeiry ili apate la kuongea na watu wake wa yanga na hakun uwezo wa kujitoa na kama akijitoa na sie tutataka hiyo ngao ya jamii iwe upande wetu ni hayo tu..

JB19 tz streka ever..
 
Thank GOD mawazo "USHUZI" haya yalitoka wakati sikuwa na access na Jukwaa,otherwise.....
 
Back
Top Bottom