KAMATI ya Utendaji ya Simba SC inatarajiwa kukutana kesho katika kikao cha dharula, kupanga tarahe ya Mkutano Mkuu kwa lengo la kuomba Baraka za wachama wake kujitoa kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kutokuwa na kutokuwa na imani na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Zacharia Hans Poppe, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, amekiambia Chanzo chetu usiku huu kwamba, kutokana na mwenendo huo wa TFF wameona hawatendewi haki na sasa wanaona bora tu wajitoe ili shirikisho hilo licheze ligi na timu inazozipenda.
Hatua hiyo inafuatia Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF, chini ya Mwenyekiti wake, Alex Mgongolwa, kuwaidhinisha Mbuyu Twite na Kevin Yondan kuchezea Yanga katika msimu ujao wa Ligi Kuu, unaoanza mwishoni mwa wiki.
Kikao cha Kamati hiyo, kilichomalizika hivi karibuni, pamoja na maamuzi hayo, kimeipa Yanga siku 21 kulipa dola 32,000 ambazo Simba SC ilimlipa Twite ili ajiunge nao, lakini baadaye akaghairi na kusaini na kuhamia Yanga.
Kanuni zipo wazi, klabu inapotaka kumsajili mchezaji lazima kwanza izungumze na klabu yake, lakini katika usajili wa Yondan, Yanga hawakufanya hivyo,alisema Hans Poppe.
Uamuzi wa Kamati hiyo leo, unafuatia kikao cha pamoja baina ya Simba na Yanga Jumatatu iliyopita kuvunjika bila kufikia makubaliano kuhusu mustakabali wa wachezaji hao.
CHANZO: GUMZO LA JIJI