WABHEJASANA
JF-Expert Member
- Jun 22, 2011
- 4,225
- 869
Wanajamvini siku moja baada ya mechi kati ya Yanga na Simba kulitokea mabishano mengi kati ya mashabiki wa pande zote mbili,huku kila mmoja akiwalaumu waamuzi kwamba ndio waliosababisha timu yao ishindwe kuibuka na ushindi.
Binafsi nishuhudia mechi hiyo LIVE na haya hapa niliyoyasema.
1:Mshika Kibenderea namba mbili Ephrony Ndissa yule aliyekuwa akinyoosha mara kwa mara kibendera kuashiria wachezaji wa Yanga wameotea ni lazima amsababishie Mwamuzi wa kati Methew Akrama kutoka mwanza matatizo,
2:Mwamuzi Akrama kutompatia kadi nyekundu 'BOBAN'kadi nyekundu kwa rafu mbaya aliyomcheea kelvine Yondani lazima Imcost.
3:Mwamuzi Akrama kutomwadhibu Mbuyu Twite wa yanga kwa kumuangusha Christopher kwenye eneo la hatari,na kuipatia simba penati,na kadi ambayo ingemsababishia Twite kadi ya pili na hivyo kutolewa nje kwa kadi nyekundu lazima imsababishie matatizo tena makubwa.
Sasa hebu angali taarifa hii iliyotolewa na Msemaji wa TFF Boniphace Wambura halafu ujihoji
Kamati ya Ligi imewaondoa waamuzi watatu wa Ligi Kuu ya Vodacom(VPL) kwa kushindwa kumudu michezo waliyopangiwa. Waamuzi hao ni Mathew Akramawa Mwanza aliyechezesha mechi namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati yaYanga na Simba iliyochezwa Oktoba 3 mwaka huu.
Wengine ni Paul Soleji wa Mwanza aliyechezesha mechi kati ya Simbana Tanzania Prisons, na mwamuzi msaidizi namba mbili kwenye mechi hiyo MwarabuMumbi wa Morogoro. Pia mwamuzi msaidizi namba mbili wa mechi ya Yanga na Simba,Ephrony Ndissa wa Dar es Salaam amepewa onyo.
Kamishna wa mechi namba 28 kati ya Yanga na African Lyon, PiusMashera ameondolewa kwenye orodha ya makamishna wa ligi hiyo kwa kuchelewakufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (Pre match meeting) na uwanjani.
Vilevile Mashera kwenye ripoti yake aliwasilisha malalamiko dhidiya msimamizi wa kituo cha Dar es Salaam, na kwa vile suala hilo ni la kinidhamuametakiwa alipeleke kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
Nayo Simba imepigwa faini ya jumla ya sh. 600,000 kwa kuchelewakufika kwenye pre match meeting ya mchezo wao dhidi Tanzania Prisons (sh.100,000) na kwa washabiki wake kuwatupia chupa za maji waamuzi wa mechi hiyo(500,000).
Pia Kamati ya Ligi imeagiza kuwa kwa vile suala la kipa ShabaniKado wa Mtibwa Sugar kudaiwa kumpiga kiongozi mmoja wa Ruvu Shooting mara baadaya mechi kati ya timu hizo iliyochezwa Uwanja wa Azam Complex ni la kinidhamulipelekwe kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikishola Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Binafsi nishuhudia mechi hiyo LIVE na haya hapa niliyoyasema.
1:Mshika Kibenderea namba mbili Ephrony Ndissa yule aliyekuwa akinyoosha mara kwa mara kibendera kuashiria wachezaji wa Yanga wameotea ni lazima amsababishie Mwamuzi wa kati Methew Akrama kutoka mwanza matatizo,
2:Mwamuzi Akrama kutompatia kadi nyekundu 'BOBAN'kadi nyekundu kwa rafu mbaya aliyomcheea kelvine Yondani lazima Imcost.
3:Mwamuzi Akrama kutomwadhibu Mbuyu Twite wa yanga kwa kumuangusha Christopher kwenye eneo la hatari,na kuipatia simba penati,na kadi ambayo ingemsababishia Twite kadi ya pili na hivyo kutolewa nje kwa kadi nyekundu lazima imsababishie matatizo tena makubwa.
Sasa hebu angali taarifa hii iliyotolewa na Msemaji wa TFF Boniphace Wambura halafu ujihoji
Kamati ya Ligi imewaondoa waamuzi watatu wa Ligi Kuu ya Vodacom(VPL) kwa kushindwa kumudu michezo waliyopangiwa. Waamuzi hao ni Mathew Akramawa Mwanza aliyechezesha mechi namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati yaYanga na Simba iliyochezwa Oktoba 3 mwaka huu.
Wengine ni Paul Soleji wa Mwanza aliyechezesha mechi kati ya Simbana Tanzania Prisons, na mwamuzi msaidizi namba mbili kwenye mechi hiyo MwarabuMumbi wa Morogoro. Pia mwamuzi msaidizi namba mbili wa mechi ya Yanga na Simba,Ephrony Ndissa wa Dar es Salaam amepewa onyo.
Kamishna wa mechi namba 28 kati ya Yanga na African Lyon, PiusMashera ameondolewa kwenye orodha ya makamishna wa ligi hiyo kwa kuchelewakufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (Pre match meeting) na uwanjani.
Vilevile Mashera kwenye ripoti yake aliwasilisha malalamiko dhidiya msimamizi wa kituo cha Dar es Salaam, na kwa vile suala hilo ni la kinidhamuametakiwa alipeleke kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
Nayo Simba imepigwa faini ya jumla ya sh. 600,000 kwa kuchelewakufika kwenye pre match meeting ya mchezo wao dhidi Tanzania Prisons (sh.100,000) na kwa washabiki wake kuwatupia chupa za maji waamuzi wa mechi hiyo(500,000).
Pia Kamati ya Ligi imeagiza kuwa kwa vile suala la kipa ShabaniKado wa Mtibwa Sugar kudaiwa kumpiga kiongozi mmoja wa Ruvu Shooting mara baadaya mechi kati ya timu hizo iliyochezwa Uwanja wa Azam Complex ni la kinidhamulipelekwe kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikishola Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)