Wiyelelee
JF-Expert Member
- Nov 9, 2012
- 1,071
- 347
Ndugu zanguni wana JF, natumaini nyote ni wazima wa afya!
Juzi, nilikua na maongezi ya muda mrefu na mfanyakazi mwenzangu. Katika maongezi, nikagundua kwamba yeye, kama nilivyo mimi, anaumia sana. Aliponieleza shida yake, nilimwambia wazi kwamba nami nateseka na mawazo kama wewe.
Hivyo nikashindwa kumpa ushauri maana tatizo lake linafanana na langu. Mawazo yenu yatasaidia nijue la kufanya, na yeye akiyasoma atapata uamuzi afanye nini.
Mimi, kabla sijaokoka nilikua na mahusiano na mke wa mtu. Nilibahatika kuzaa nae mtoto wa kike. Mme wake yupo ila huyu mwanamke tulipendana sana ila hatukubahatika kuoana. Alipoolewa, na hata mimi baada ya kuoa, mahusiano yetu yaliendelea tena vibaya sana.
Mwaka juzi mwanzoni tulishauriana tuache maana tulikua tunatenda dhambi ila tuliamua kuwa na mtoto awe ukumbusho wetu. Na kweli tukabahatika kumpata mtoto huyu wa kike.
Kwa huyu bwana, kama ilivyo kwangu, huyu nimtoto wa kike pekee. Ninao watoto wakiume 3. Yeye anao watoto wa kiume wawili na alivyoona huyu amwezaliwa, alimweleza mke wake kwamba wanatosha. Anampenda sana mtoto huyu wa kike.
Sasa mi naumia sana. Siku moja nikiwa na mke na watoto wangu supermarket mmoja ya hapa, niliwaona wao pia wakiwa katika heka heka ya shopping wakiwa na mtoto wangu. Niliumia sana. Sasa nataka nifanye harakati nimchukue mtoto wangu. Nifanyeje jamani nisaidie.
Mfanyakazi mwenzangu yeye alimpa binti wakati anasoma na bila kujua, binti alikua mchumba wa mtu.
Alipoolewa aliolewa na ujauzito wa jamaa. Yeye alipata mtoto wa kiume na mme wa huyo mwanamke hajui lolote kwamba analea mtoto wa mwenzake. Na yeye anataka afanye harakati amchukue mtoto wake.
Najutia dhambi niliyoifanya na nimbaya sana. Lakini mtoto wangu namtaka nawaombeni msaada. Nimejutia dhambi hivyo naomba ushauri tu na sio matusi.
Juzi, nilikua na maongezi ya muda mrefu na mfanyakazi mwenzangu. Katika maongezi, nikagundua kwamba yeye, kama nilivyo mimi, anaumia sana. Aliponieleza shida yake, nilimwambia wazi kwamba nami nateseka na mawazo kama wewe.
Hivyo nikashindwa kumpa ushauri maana tatizo lake linafanana na langu. Mawazo yenu yatasaidia nijue la kufanya, na yeye akiyasoma atapata uamuzi afanye nini.
Mimi, kabla sijaokoka nilikua na mahusiano na mke wa mtu. Nilibahatika kuzaa nae mtoto wa kike. Mme wake yupo ila huyu mwanamke tulipendana sana ila hatukubahatika kuoana. Alipoolewa, na hata mimi baada ya kuoa, mahusiano yetu yaliendelea tena vibaya sana.
Mwaka juzi mwanzoni tulishauriana tuache maana tulikua tunatenda dhambi ila tuliamua kuwa na mtoto awe ukumbusho wetu. Na kweli tukabahatika kumpata mtoto huyu wa kike.
Kwa huyu bwana, kama ilivyo kwangu, huyu nimtoto wa kike pekee. Ninao watoto wakiume 3. Yeye anao watoto wa kiume wawili na alivyoona huyu amwezaliwa, alimweleza mke wake kwamba wanatosha. Anampenda sana mtoto huyu wa kike.
Sasa mi naumia sana. Siku moja nikiwa na mke na watoto wangu supermarket mmoja ya hapa, niliwaona wao pia wakiwa katika heka heka ya shopping wakiwa na mtoto wangu. Niliumia sana. Sasa nataka nifanye harakati nimchukue mtoto wangu. Nifanyeje jamani nisaidie.
Mfanyakazi mwenzangu yeye alimpa binti wakati anasoma na bila kujua, binti alikua mchumba wa mtu.
Alipoolewa aliolewa na ujauzito wa jamaa. Yeye alipata mtoto wa kiume na mme wa huyo mwanamke hajui lolote kwamba analea mtoto wa mwenzake. Na yeye anataka afanye harakati amchukue mtoto wake.
Najutia dhambi niliyoifanya na nimbaya sana. Lakini mtoto wangu namtaka nawaombeni msaada. Nimejutia dhambi hivyo naomba ushauri tu na sio matusi.