Obhusegwe
JF-Expert Member
- Dec 28, 2008
- 231
- 28
Jamani habari za mvua?
Leo wakazi wa dsm tumepata mvua, nadhani wengi wamefurahi, mbali na kuwa kuna kero mbalimbali associated with it.
Leo nilikuwa mjini mapema sana asbh, nikapaki gari ''somewhere" nikaenda kwny shughuli zangu. Nilivyorudi nikakuta gari zima limezungukwa na dimbwi la maji yaani hakuna jinsi ya kuingia mpaka nikanyage kwenye maji!! Jamani imenipa mtihani, mwisho nikajitoa muhanga nikayakanyaga maji ndo nikaweza kuingia kwny gari.
Sasa la kutia hasira!! Kabla sijawasha gari, akaja dada amevaa koti la NPS, akakinga mkono anataka pesa, nikamuuliza pesa ya nini, akasema ''ya parking'', nikamwuliza parking gani kwny dimbwi? akasema yeye hajali alimradi gari limesimama, anachotaka ni pesa!! Du!! nikashangaa!!
Nililoamua ni kuwasha gari na kuondoka bila kulipa kwani bado nilikuwa na hasira jinsi nilivyochafuka kutokana na hilo dimbwi!! sasa sijui watanitafuta au la!! Najua naweza kuwa nimevunja sheria, lakini tujiulize yafuatayo;
Je NPS kazi yake ni kukusanya pesa za parking tuuuu au inao wajibu pia wa kuhakikisha parking zinapatikana kirahisi na zinakuwa na hadhi ya kutosha?
Je ni haki kulipia huduma ambayo ubora wake ni almost zero? Au watanzania tumeshazoea kutoa hela tu(hata kama ni ndogo) bila kuuliza alimradi mtu amesema lete hela?
Ni maeneo mangapi hapa mjini NPS au tuseme halmashauri za manispaa zetu zimeyadesign mahususi kwa ajili ya parking(nimeona la pale karibu na PPF house ambalo nalo ni matope matupu!!) au wanasubiri tu watu wakishajenga majengo then wao wanaweka P kuubwaa!! mbele ya jengo na kusubiri watu waegeshe nao wadai 300?
Jamani huu si wizi????? Tunaibiwa tukiwa macho!! Watch out!!!
Leo wakazi wa dsm tumepata mvua, nadhani wengi wamefurahi, mbali na kuwa kuna kero mbalimbali associated with it.
Leo nilikuwa mjini mapema sana asbh, nikapaki gari ''somewhere" nikaenda kwny shughuli zangu. Nilivyorudi nikakuta gari zima limezungukwa na dimbwi la maji yaani hakuna jinsi ya kuingia mpaka nikanyage kwenye maji!! Jamani imenipa mtihani, mwisho nikajitoa muhanga nikayakanyaga maji ndo nikaweza kuingia kwny gari.
Sasa la kutia hasira!! Kabla sijawasha gari, akaja dada amevaa koti la NPS, akakinga mkono anataka pesa, nikamuuliza pesa ya nini, akasema ''ya parking'', nikamwuliza parking gani kwny dimbwi? akasema yeye hajali alimradi gari limesimama, anachotaka ni pesa!! Du!! nikashangaa!!
Nililoamua ni kuwasha gari na kuondoka bila kulipa kwani bado nilikuwa na hasira jinsi nilivyochafuka kutokana na hilo dimbwi!! sasa sijui watanitafuta au la!! Najua naweza kuwa nimevunja sheria, lakini tujiulize yafuatayo;
Je NPS kazi yake ni kukusanya pesa za parking tuuuu au inao wajibu pia wa kuhakikisha parking zinapatikana kirahisi na zinakuwa na hadhi ya kutosha?
Je ni haki kulipia huduma ambayo ubora wake ni almost zero? Au watanzania tumeshazoea kutoa hela tu(hata kama ni ndogo) bila kuuliza alimradi mtu amesema lete hela?
Ni maeneo mangapi hapa mjini NPS au tuseme halmashauri za manispaa zetu zimeyadesign mahususi kwa ajili ya parking(nimeona la pale karibu na PPF house ambalo nalo ni matope matupu!!) au wanasubiri tu watu wakishajenga majengo then wao wanaweka P kuubwaa!! mbele ya jengo na kusubiri watu waegeshe nao wadai 300?
Jamani huu si wizi????? Tunaibiwa tukiwa macho!! Watch out!!!