Natamani kupaza sauti kuhusu uonevu huu ila...

Ndebile

JF-Expert Member
Sep 14, 2011
7,237
9,871
Nipo kibaruani mchana wa leo (nimerudi kazini awamu ya sita baada kama nilivyohaidi), nimempokea mama na kichanga chake ambaye amejifungulia kazini kwenye kiwanda cha Mchina (sehemu sitaitaja) ila ni mazingira mabaya kujifungulia binadamu, mama hana kadi ya kliniki na bahati nzuri alikuja kuanza kliniki ijumaa saa kumi akakuta huduma zimeishafungwa (jiulize ilikuwaje mama aanze kliniki na mimba kubwa karibia na kujifungua, hii haihitaji akili kubwa bila shaka hakuna ruhusa kazini) kwahiyo zile huduma kama vipimo vya wingi wadamu, magonjwa ya zinaa na ukimwi nk. na hivyo maisha ya huyu mtoto yapo hatarini!

Jamaa waliomsindikiza kwenye tax huyu mama ni wanaume watatu hakuna jisia ya kike! Walipofika wakahudumiwa wakataka kulipia staff aliyekuwepo akasema huduma za mama na mtoto ni bure, na hapo waksema wanazo 200,000/ mchina kawapa kwa ajili ya matibabu ya huyu mama na wakasema anahitaji risiti, wakauliza kama tunaweza kufanya mbinu ili risiti ipatikane .....kwa ufupi hatukuwapa risiti na badala yake yule mama alipewa sh.40,000 hela iliyobaki wasema wanaenda kutafta namna ya kupata risiti...tuachane na mambo ya pesa maana mimi sio lengo langu la kuleta uzi hapa JF,

Kitendo cha huyu mama kutohudhulia kliniki, kujifungulia kazini, nk kinaleta picha ya kuwepo na manyanyaso kwenye hiki kiwanda, nilitamani huyu mama awe mfano kwa akina mama na watu wote wanaoteswa na kunyimwa haki zao makazini...nilitamani kuripoti unyama huu ila....HII NCHI WAPENDA HAKI HAWATAKIWI KABISA, ukiangalia kesi za wenye pesa kama wale wezi wa mafuta Kigamboni ambapo serikali wapo kimya, nk nikijifanya kuingia anga za hawa wachina wanaoshirikiana na watanzania wenzangu yanaweza kunikuta ya kunikuta na kubaki peke yangu na historia isinikumbuke!
Tuendelee kuangalia pingamizi lililowekwa kwa Diamond Platnumz aondolewe kwenye tuzo za BET maana hiki ndicho waliowengi miongoni mwetu tunaweza sana!

 
Kiukweli sijaelewa.

Kama ni clinic kuna wanawake kibao bado wanajifungulia nyumbani kwa imani zao
 
FUNGUKA MKUUKIWANDA GANI, KIKO WAPI.N.K!..KAMA HUWEZI KWENDA POLISI AMA DAWATI HUSIIKA HATA KUWEKA HAPA KILA KITU UNAOGOPA?
Polisi hawa hawa wanaopigana risasi wakigombea kiti cha gari cha mbele? Mh, ngoja nisubiri maoni ya wadau wengine!
 
Kiukweli sijaelewa.

Kama ni clinic kuna wanawake kibao bado wanajifungulia nyumbani kwa imani zao
Mkuu rudia kusoma kidogo, mama kajifungulia kiwandani ambapo ni kazini kwake, kiwanda cha mwekezaji wa kichina!
 
Ulipomuhoji alijibu nini? Hapa naona unapiga ramli chonganishi
Kasema alizuiliwa kuondoka, kwakuwa huwa wanafanyuwa ukaguzi kabla ya kutoka nje ya kiwanda...mkaguzi alikuwa mbali ndipo akajifungua akisaidiwa na wafanyakazi wenzake. Mkuu acha kashfa, Nina kiapo cha fani yangu, Mimi sio mwanasiasa
 
Wachina wamekuja kuwekeza ila ni kilio kwa jamii wanayoitumia, wao wanacheza na wakubwa huko juu wanawapoteza maboya hata hawawezi kuwafikiria wananchi wao na shida zao kuhusu hao wachina na ukipeleka kesi mswahili ndio unaonekana jau... ***** zao viongozi wanaowalea wachina
 
Ushauri:
Tafuta mwanaharakati mmoja muombe appointment ili ufikishe kilio chako kama unaogopa kuweka wazi hili jambo. Jitahidi kama utakubaliwa kwenda na vielelezo
 
Watu kama nyie ndio matatizo, wewe baadaa ya kushuhudia hilo tukio na sheria zipo wazi maternity leave inaanza lini.

Badala ya hilo swala kulipeleka serikalini na kwenye vyombo vya habari unalileta kimafumbo hata huyo Mwajiri umtaji.

Wahusika wakipita hapa unategemea wachukue hatua gani wakati jina la mwajiri hawana, wala la muajiriwa na tukio lenye limetokea wapi katika kilometre mraba za Tanzania.

Tuanze sisi tunapoona makosa au mambo yanayotukera kutoa report kwa wahusika.
 
Watu kama nyie ndio matatizo, wewe badala ya kushuhudia hilo tukio na sheria zipo wazi maternity leave inaanza lini.

Badala ya hilo swala kulipeleka serikalini na kwenye vyombo vya habari unalileta kimafumbo hata huyo Mwajiri umtaji.

Wahusika wakipita hapa unategemea wachukue hatua gani wakati jina la mwajiri hawana, wala la muajiriwa na tukio lenye limetokea wapi katika kilometre mraba za Tanzania.

Tuanze sisi tunapoona makosa au mambo yanayotukera kutoa report kwa wahusika.
Bila shaka hii ni chai ya jioni. Haiwezekani health worker ashindwe hata kuandika historia ya mgonjwa. Na pia haelewi/ameshindwa kusimamia muongozo wa kazi yake. Ameleta contradiction tupu mfano huyo mama alishindwa vipi kuhudhuria clinic kwa miezi yote 9?, alikuwa na mkataba wa aina gani?, alipata uchungu wa ghafla? Maswali ni mengi mengi
 
Bila shaka hii ni chai ya jioni. Haiwezekani health worker ashindwe hata kuandika historia ya mgonjwa. Na pia haelewi/ameshindwa kusimamia muongozo wa kazi yake. Ameleta contradiction tupu mfano huyo mama alishindwa vipi kuhudhuria clinic kwa miezi yote 9?, alikuwa na mkataba wa aina gani?, alipata uchungu wa ghafla? Maswali ni mengi mengi
Kuna matatizo ya kimfumo kwenye maswala ya safeguarding; sio kwenye afya sehemu nyingi tu zinazohusika na social services.

Health worker, walimu, ustawi wa jamii na taasisi zingine zinazotoa huduma za jamii hao wafanyakazi ni askari wa mbele kwa serikali kwenye kusimamia sheria, kupambana kupunguza maswala ya unyanyasaji kinyume na sheria na kadhalika.

Nchi za wenzetu frontline workers wana sign mkataba wa duty of care kuripoti mambo ambayo watakayoona ‘ndivyo sivyo’ ni jukumu lao na sehemu zingine unashitakiwa for negligence usipofanya ivyo mtu akapata madhara wakati wewe ulikuwa na information ambazo ukuzitoa watu wachunguze na kuchukua hatua.

Mtu anakutana na mjamzito anaona kabisa process zake za kumpatia huduma hazikuwa sahihi kutokana na restrictions za mwajiri wake ambazo ni kinyume cha sheria badala ya kupeleka concerns kwa wahusika anakuja hapa kulalamika sasa hayo matatizo yataisha vipi kama wenye mamlaka awapelekewi habari na watu wanaoshuhudia ili kuchunguza na kuchukua hatua.
 
Kuna matatizo ya kimfumo kwenye maswala ya safeguarding; sio kwenye afya sehemu nyingi tu zinazohusika na social services.

Health worker, walimu, ustawi wa jamii na taasisi zingine zinazotoa huduma za jamii hao wafanyakazi ni askari wa mbele kwa serikali kwenye kusimamia sheria, kupambana kupunguza maswala ya unyanyasaji kinyume na sheria na kadhalika.

Nchi za wenzetu frontline workers wana sign mkataba wa duty of care kuripoti mambo ambayo watakayoona ‘ndivyo sivyo’ ni jukumu lao na sehemu zingine unashitakiwa for negligence usipofanya ivyo mtu akapata madhara wakati wewe ulikuwa na information ambazo ukuzitoa watu wachunguze na kuchukua hatua.

Mtu anakutana na mjamzito anaona kabisa process zake za kumpatia huduma hazikuwa sahihi kutokana na restrictions za mwajiri wake ambazo ni kinyume cha sheria badala ya kupeleka concerns kwa wahusika anakuja hapa kulalamika sasa hayo matatizo yataisha vipi kama wenye mamlaka awapelekewi habari na watu wanaoshuhudia ili kuchunguza na kuchukua hatua.
Mkuu naelewa unachoongea, Mimi senior staff, miaka 20+ pamoja na miiko, maadili, nk ya utumishi ila hayo yapo kwenye makaratasi tu, ona dhahama wanayopata watetea haki kutoka kwa watu wenye pesa...labda kama unaishi nje ya Tanzania!
 
Back
Top Bottom